Vipengele vya Katiba unavyodhani haviko sawa na mapendekezo yako

Vipengele vya Katiba unavyodhani haviko sawa na mapendekezo yako

The Phylosopher

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2015
Posts
1,968
Reaction score
2,957
Kwa kadri joto la kudai katiba mpya linavyozidi ndivyo ninavyojiuliza maswali mengi sana.

Maswali haya yanatokana na kwamba tulishuhudia jirani zetu Kenya walitunga katiba mpya kwa mbwembwe nyingi sana, kwa kuaminishwa kwamba wamepata muarobaini wa demokrasia.

Hata hivyo muda mfupi baadae walianza kuilalamikia hiyo katiba mpya kiasi cha kuibuka upya kwa vuguvugu linalodai mabadiliko mengine ya katiba ambayo hata raisi yuko upande wa walalamikaji.

Kwa uelewa wangu wa kawaida, kwa nchi zetu za kiafrika katiba nzuri ni ile inayompendelea mhusika kwenye maslahi yake.

Tuache kuzolewa na upepo wa wanasiasa naomba tutoe maoni huru kabla ya kuvaa jezi ya chama chochote ni kipengele kipi na kipi unadhani hakipaswi kuwepo kwenye katiba na kwa sababu zipi?
 
Madaraka ya rais ni makubwa iwepo check and balance rais awajibishwe kwa kutofuata katiba, jinai, Wizi na ufisadi hata akiwa madarakani.

Kazi za mahakama ziachwe zifanywe na mahakama kama kupatikana kwa Majaji, jaji mkuu, mwanasheria mkuu wa serikali!

Kuondoa utitili wa vyeo kama

Mkuu wa wilaya

Mkuu wa mkoa

Wabaki wakurugenzi

Wabaki wabunge

Wabaki madiwani na meya ndiye awe bosi wa wilaya na achaguliwe na wananchi

Wabunge wagombee wawili yaani mwanamke na mwanaume na lisiwe jimbo iwe kwa kila wilaya

Muda wa kuwa mbunge au waziri uwe mwisho miaka 10

Waziri mkuu na mawaziri wasiwe wabunge wawe wasomi na wapitishwe na bunge na mahakama kwa kufanyiwa vetting na kuangaliwa juu ya record zao za uko nyuma.

Sera ya Elimu iwekwe kwenye katiba hata aje kichaa gani watanzania waweze kusoma bure elimu ya msingi na sekondani na elimu yote i-base kwenye technical education.

Afya tuwe na Sera ya bima kwa watu wote iwe ni lazima kwa kila mtu utengenezwe mfumo wa kila raia kuwa na bima ya bei nafuu na tuwatambue masikini wote wanaoishi chini ya dollar moja kwa siku bima wapewe bure ndani ya katiba.

Ni hayo tu wengine watasema mengine!!
 
kifungu cha 37 sehemu ya 5 tusipokuwa makini kifungu 37 sehemu ya 5 itakuja kutuletea matatizo huko mbeleni

Pia cheo cha Makamu wa Rais kifutwe makamu wa Rais awe Rais wa Zanzibar kwa maana Rais akiwepo nchini kazi za makamu wa Rais unaweza hata usizijue leo waziri mkuu ana kazi zenye mashiko kuliko makamu wa Rais , Rais wa Zanzibar akija Bara anakuja kama mjumbe wa baraza la mawaziri why wakt yeye ni Rais wa Upande mwingine why asiwe makamu wa Rais na ikitokea Rais wa Muungano amefariki au kushindwa kutimiza majukumu yake yeye anachukia madaraka kwa muda wa miezi 3 kwa ajili ya kuandaa uchaguzi akichaguliwa Rais yeye anarudi kwenye umakamu wake nasema hvyo naweza onekana chizi lakini kwa roho ya watanzania kupenda madaraka Mungu apishe mbali tunaweza pata makamu wa Rais mwenye tamaa siku moja akashirikiana na maadui wakamuhujumu Rais tukajikuta tunazika kwa maaana anajua kabla ya mazishi yeye ndo anakuwa Rais.

Kinachowafanya makamu wengi wa Kiafrika kuto hujumu marais wao ni kutokujua hatma yake baada ya msiba kwa maana wenye kuvaa nguo za mabaka mabaka wanaweza fanya yao hilo tu.. lakini wakiona kumbe inawezekana na transition of power inafanyika smoothly ni hatari sana.

Faida ya Rais wa Zanzibar kuwa makamu wa Rais kwanza muungano utaimalika zaidi pili huyu hawezi kuhujumu kwa maana anajua hawezi kuwa Rais hata ikitokea Rais aliepo kufa au kushindwa kutimiza majukumu .Hapa ndo kazi ya Tiss kuhakikisha hawa viongozi wetu wanafanyiwa upembuzi hakinifu tusiruhusu tu watu kupata madaraka ovyo ovyo wanaweza kututia hasara siku moja kwa tamaa zao .
 
Tume ya uchaguzi iwe ni taasisi inayohusisha watu wenye taaruma hiyo na waajiriwe kama wafanyakazi wengine wa umma mfano hakimu, dakitari mwalimu n.k na isiwe tume yenye watendaji wanaochaguliwa na rais au na kiongozi yeyote anayetokana na chama.
 
Kwa kadri joto la kudai katiba mpya linavyozidi ndivyo ninavyojiuliza maswali mengi sana.

Maswali haya yanatokana na kwamba tulishuhudia jirani zetu Kenya walitunga katiba mpya kwa mbwembwe nyingi sana, kwa kuaminishwa kwamba wamepata muarobaini wa demokrasia.

Hata hivyo mda mfupi baadae walianza kuilalamikia hiyo katiba mpya kiasi cha kuibuka upya kwa vuguvugu linalodai mabadiliko mengine ya katiba ambayo hata raisi yuko upande wa walalamikaji.

Kwa uelewa wangu wa kawaida, kwa nchi zetu za kiafrika katiba nzuri ni ile inayompendelea mhusika kwenye maslahi yake.

Tuache kuzolewa na upepo wa wanasiasa naomba tutoe maoni huru kabla ya kuvaa jezi ya chama chochote ni kipengele kipi na kipi unadhani hakipaswi kuwepo kwenye katiba na kwa sababu zipi?
Naona umeanza kuiponda katiba ya Kenya ili kukidhi utashi wako. Kwa taarifa yako, katiba ya Kenya inayolalamikiwa na baadhi ya Wakenya ni bora mara elfu kuliko hii ya kwetu. Hayo malalamiko ni kutaka iboreshwe zaidi.

Hata hivyo maoni yetu mengi tuliyaweka kwenye tume ya Jaji Warioba, na yalikuwa bora zaidi kuliko hii katiba mbovu iliyopo. Eneo la madaraka ya urais ni tatizo kubwa, toka Magufuli hajawa rais, na alipokuwa rais udhaifu huo ukadhibitika zaidi. Kwanza kabisa rais asiwe na kinga ya makosa, awapo madarakani au akiwa ametoka. Rais asiteue Jaji mkuu, wala viongozi wa taasisi za kimamlaka kama atakavyo. Kazi ya rais iwe ni kumuapisha tu. Mkuu wa majeshi na vyombo vingine vya usalama wajiteue wenyewe kwa vigezo watakavyojiwekea, na kazi ya rais iwe kumuapisha tu.

Wabunge mwisho miaka 10, haya ni kwa uchache.
 
Madaraka ya rais ni makubwa iwepo check and balance rais awajibishwe kwa kutofuata katiba, jinai, Wizi na ufisadi hata akiwa madarakani.

Kazi za mahakama ziachwe zifanywe na mahakama kama kupatikana kwa Majaji, jaji mkuu, mwanasheria mkuu wa serikali!

Kuondoa utitili wa vyeo kama

Mkuu wa wilaya

Mkuu wa mkoa

Wabaki wakurugenzi

Wabaki wabunge

Wabaki madiwani na meya ndiye awe bosi wa wilaya na achaguliwe na wananchi

Wabunge wagombee wawili yaani mwanamke na mwanaume na lisiwe jimbo iwe kwa kila wilaya

Waziri mkuu na mawaziri wasiwe wabunge wawe wasomi na wapitishwe na bunge na mahakama kwa kufanyiwa vetting na kuangaliwa juu ya record zao za uko nyuma.

Sera ya Elimu iwekwe kwenye katiba hata aje kichaa gani watanzania waweze kusoma bure elimu ya msingi na sekondani na elimu yote i-base kwenye technical education.

Afya tuwe na Sera ya bima kwa watu wote iwe ni lazima kwa kila mtu utengenezwe mfumo wa kila raia kuwa na bima ya bei nafuu na tuwatambue masikini wote wanaoishi chini ya dollar moja kwa siku bima wapewe bure ndani ya katiba.

Ni hayo tu wengine watasema mengine!!
Umeambkwa vipengele gani umekimbilia u-DC. U DC ni kipengele? Pumbavu!!!
 
Wewe unaishi ulimwengu gani? Vipengere vyote vyenye matatizo, kamati ya Katiba ya Warioba ilimaliza hiyo kazi. Unajua kamati ulitumia muda gani kuzunguka nchi nzima? Wewe umepanga kutumia muda gani kukusanya maoni hapa JF? Katafute report ya Warioba.
 
Kwa kadri joto la kudai katiba mpya linavyozidi ndivyo ninavyojiuliza maswali mengi sana.

Maswali haya yanatokana na kwamba tulishuhudia jirani zetu Kenya walitunga katiba mpya kwa mbwembwe nyingi sana, kwa kuaminishwa kwamba wamepata muarobaini wa demokrasia.

Hata hivyo muda mfupi baadae walianza kuilalamikia hiyo katiba mpya kiasi cha kuibuka upya kwa vuguvugu linalodai mabadiliko mengine ya katiba ambayo hata raisi yuko upande wa walalamikaji.

Kwa uelewa wangu wa kawaida, kwa nchi zetu za kiafrika katiba nzuri ni ile inayompendelea mhusika kwenye maslahi yake.

Tuache kuzolewa na upepo wa wanasiasa naomba tutoe maoni huru kabla ya kuvaa jezi ya chama chochote ni kipengele kipi na kipi unadhani hakipaswi kuwepo kwenye katiba na kwa sababu zipi?
SUALA LA KATIBA LILIISHA ISHA, WARIOBA ALIMALIZA KAZI YAKE YA KUKUSANYA MAONI TANZANIA NZIMA. USITURUDISHE HUKO
 
Madaraka ya rais ni makubwa iwepo check and balance rais awajibishwe kwa kutofuata katiba, jinai, Wizi na ufisadi hata akiwa madarakani.

Kazi za mahakama ziachwe zifanywe na mahakama kama kupatikana kwa Majaji, jaji mkuu, mwanasheria mkuu wa serikali!

Kuondoa utitili wa vyeo kama

Mkuu wa wilaya

Mkuu wa mkoa

Wabaki wakurugenzi

Wabaki wabunge

Wabaki madiwani na meya ndiye awe bosi wa wilaya na achaguliwe na wananchi

Wabunge wagombee wawili yaani mwanamke na mwanaume na lisiwe jimbo iwe kwa kila wilaya

Waziri mkuu na mawaziri wasiwe wabunge wawe wasomi na wapitishwe na bunge na mahakama kwa kufanyiwa vetting na kuangaliwa juu ya record zao za uko nyuma.

Sera ya Elimu iwekwe kwenye katiba hata aje kichaa gani watanzania waweze kusoma bure elimu ya msingi na sekondani na elimu yote i-base kwenye technical education.

Afya tuwe na Sera ya bima kwa watu wote iwe ni lazima kwa kila mtu utengenezwe mfumo wa kila raia kuwa na bima ya bei nafuu na tuwatambue masikini wote wanaoishi chini ya dollar moja kwa siku bima wapewe bure ndani ya katiba.

Ni hayo tu wengine watasema mengine!!
je haya yote yamo katika ile rasimu ya warioba?
ninachojua kiasi ni kwamba katiba mpya itakuja kuendelea pale mchakato ulipoishia
 
Madaraka Makubwa kwa Rais baadhi yahamishiwe na kufanywa na jopo la watu watakao aminiwa watenda haki na kweli. Rais achiwe kwenye mambo ya kuamrisha Majeshi na ya aina hiyo.

Uchaguzi wa Rais uhojiwe mahakamani kama liko tatizo kwenye kura. Hii itamfanya Rais aliye chaguliwa ajue kwamba cheo ni dhamana na asijione MunguNtu.

Uwepo utaratibu wa kidemokrasia, haki na kisheria unaotekelezeka wa kumuimpeach Rais. Sio huu wa sasa ambao mpaka Yesu arudi hauwezi kufanikisha lengo lililokusudiwa.
 
Madaraka ya rais ni makubwa iwepo check and balance rais awajibishwe kwa kutofuata katiba, jinai, Wizi na ufisadi hata akiwa madarakani.

Kazi za mahakama ziachwe zifanywe na mahakama kama kupatikana kwa Majaji, jaji mkuu, mwanasheria mkuu wa serikali!

Kuondoa utitili wa vyeo kama

Mkuu wa wilaya

Mkuu wa mkoa

Wabaki wakurugenzi

Wabaki wabunge

Wabaki madiwani na meya ndiye awe bosi wa wilaya na achaguliwe na wananchi

Wabunge wagombee wawili yaani mwanamke na mwanaume na lisiwe jimbo iwe kwa kila wilaya

Waziri mkuu na mawaziri wasiwe wabunge wawe wasomi na wapitishwe na bunge na mahakama kwa kufanyiwa vetting na kuangaliwa juu ya record zao za uko nyuma.

Sera ya Elimu iwekwe kwenye katiba hata aje kichaa gani watanzania waweze kusoma bure elimu ya msingi na sekondani na elimu yote i-base kwenye technical education.

Afya tuwe na Sera ya bima kwa watu wote iwe ni lazima kwa kila mtu utengenezwe mfumo wa kila raia kuwa na bima ya bei nafuu na tuwatambue masikini wote wanaoishi chini ya dollar moja kwa siku bima wapewe bure ndani ya katiba.

Ni hayo tu wengine watasema mengine!!

You are not only "technically" but "technically sound". Safi sana!!!!
 
Kuwepo na sheria ya opinion polls ambazo zitaendeshwa kwa mujibu wa sheria na kuheshimiwa. Maendeleo ya tekelinalokujia hii inawezekana. Kukitokea jambo lenye sintofahanu liamuliwe kwa maoni ya wananchi wenyewe kupitia mfumo huu. Kazi hii ikasimishwe kwa tume ya uchaguzi ili wasile mishahara rahisi rahisi baada ya uchaguzi mkuu.
 
Kwa kadri joto la kudai katiba mpya linavyozidi ndivyo ninavyojiuliza maswali mengi sana.

Maswali haya yanatokana na kwamba tulishuhudia jirani zetu Kenya walitunga katiba mpya kwa mbwembwe nyingi sana, kwa kuaminishwa kwamba wamepata muarobaini wa demokrasia.

Hata hivyo muda mfupi baadae walianza kuilalamikia hiyo katiba mpya kiasi cha kuibuka upya kwa vuguvugu linalodai mabadiliko mengine ya katiba ambayo hata raisi yuko upande wa walalamikaji.

Kwa uelewa wangu wa kawaida, kwa nchi zetu za kiafrika katiba nzuri ni ile inayompendelea mhusika kwenye maslahi yake.

Tuache kuzolewa na upepo wa wanasiasa naomba tutoe maoni huru kabla ya kuvaa jezi ya chama chochote ni kipengele kipi na kipi unadhani hakipaswi kuwepo kwenye katiba na kwa sababu zipi?
Wandugu,
Kazi kubwa ilikwishafanyika na Tume ya Warioba, tuanzie hapo
 

Attachments

Kwa kadri joto la kudai katiba mpya linavyozidi ndivyo ninavyojiuliza maswali mengi sana.

Maswali haya yanatokana na kwamba tulishuhudia jirani zetu Kenya walitunga katiba mpya kwa mbwembwe nyingi sana, kwa kuaminishwa kwamba wamepata muarobaini wa demokrasia.

Hata hivyo muda mfupi baadae walianza kuilalamikia hiyo katiba mpya kiasi cha kuibuka upya kwa vuguvugu linalodai mabadiliko mengine ya katiba ambayo hata raisi yuko upande wa walalamikaji.

Kwa uelewa wangu wa kawaida, kwa nchi zetu za kiafrika katiba nzuri ni ile inayompendelea mhusika kwenye maslahi yake.

Tuache kuzolewa na upepo wa wanasiasa naomba tutoe maoni huru kabla ya kuvaa jezi ya chama chochote ni kipengele kipi na kipi unadhani hakipaswi kuwepo kwenye katiba na kwa sababu zipi?
Muungano upitiwe upya , twende na serikali tatu, Tanganyika iludi, wa Sasa hapana, Tanganyika imemezwa
 
Back
Top Bottom