The Phylosopher
JF-Expert Member
- Mar 11, 2015
- 1,968
- 2,957
Kwa kadri joto la kudai katiba mpya linavyozidi ndivyo ninavyojiuliza maswali mengi sana.
Maswali haya yanatokana na kwamba tulishuhudia jirani zetu Kenya walitunga katiba mpya kwa mbwembwe nyingi sana, kwa kuaminishwa kwamba wamepata muarobaini wa demokrasia.
Hata hivyo muda mfupi baadae walianza kuilalamikia hiyo katiba mpya kiasi cha kuibuka upya kwa vuguvugu linalodai mabadiliko mengine ya katiba ambayo hata raisi yuko upande wa walalamikaji.
Kwa uelewa wangu wa kawaida, kwa nchi zetu za kiafrika katiba nzuri ni ile inayompendelea mhusika kwenye maslahi yake.
Tuache kuzolewa na upepo wa wanasiasa naomba tutoe maoni huru kabla ya kuvaa jezi ya chama chochote ni kipengele kipi na kipi unadhani hakipaswi kuwepo kwenye katiba na kwa sababu zipi?
Maswali haya yanatokana na kwamba tulishuhudia jirani zetu Kenya walitunga katiba mpya kwa mbwembwe nyingi sana, kwa kuaminishwa kwamba wamepata muarobaini wa demokrasia.
Hata hivyo muda mfupi baadae walianza kuilalamikia hiyo katiba mpya kiasi cha kuibuka upya kwa vuguvugu linalodai mabadiliko mengine ya katiba ambayo hata raisi yuko upande wa walalamikaji.
Kwa uelewa wangu wa kawaida, kwa nchi zetu za kiafrika katiba nzuri ni ile inayompendelea mhusika kwenye maslahi yake.
Tuache kuzolewa na upepo wa wanasiasa naomba tutoe maoni huru kabla ya kuvaa jezi ya chama chochote ni kipengele kipi na kipi unadhani hakipaswi kuwepo kwenye katiba na kwa sababu zipi?