Vipengele vya Katiba unavyodhani haviko sawa na mapendekezo yako

Vipengele vya Katiba unavyodhani haviko sawa na mapendekezo yako

Tupunguze madaraka ya rais,anasema mmoja.
Tufute vyeo vya RC na DC, anasema mwingine.
Ukipunguza madaraka ya rais. unaongeza madaraka ya RC.
In fact,nimeamka asubuhi hii nimeota RC amemtuma mesenja kuniambia niondoke kwenye Mkoa huu.
 
kifungu cha 37 sehemu ya 5 tusipokuwa makini kifungu 37 sehemu ya 5 itakuja kutuletea matatizo huko mbeleni

Pia cheo cha Makamu wa Rais kifutwe makamu wa Rais awe Rais wa Zanzibar kwa maana Rais akiwepo nchini kazi za makamu wa Rais unaweza hata usizijue leo waziri mkuu ana kazi zenye mashiko kuliko makamu wa Rais , Rais wa Zanzibar akija Bara anakuja kama mjumbe wa baraza la mawaziri why wakt yeye ni Rais wa Upande mwingine why asiwe makamu wa Rais na ikitokea Rais wa Muungano amefariki au kushindwa kutimiza majukumu yake yeye anachukia madaraka kwa muda wa miezi 3 kwa ajili ya kuandaa uchaguzi akichaguliwa Rais yeye anarudi kwenye umakamu wake nasema hvyo naweza onekana chizi lakini kwa roho ya watanzania kupenda madaraka Mungu apishe mbali tunaweza pata makamu wa Rais mwenye tamaa siku moja akashirikiana na maadui wakamuhujumu Rais tukajikuta tunazika kwa maaana anajua kabla ya mazishi yeye ndo anakuwa Rais.

Kinachowafanya makamu wengi wa Kiafrika kuto hujumu marais wao ni kutokujua hatma yake baada ya msiba kwa maana wenye kuvaa nguo za mabaka mabaka wanaweza fanya yao hilo tu.. lakini wakiona kumbe inawezekana na transition of power inafanyika smoothly ni hatari sana.

Faida ya Rais wa Zanzibar kuwa makamu wa Rais kwanza muungano utaimalika zaidi pili huyu hawezi kuhujumu kwa maana anajua hawezi kuwa Rais hata ikitokea Rais aliepo kufa au kushindwa kutimiza majukumu .Hapa ndo kazi ya Tiss kuhakikisha hawa viongozi wetu wanafanyiwa upembuzi hakinifu tusiruhusu tu watu kupata madaraka ovyo ovyo wanaweza kututia hasara siku moja kwa tamaa zao .
Tutamruhusu vipi Rais wazanzibar ambaye hakuchaguliwa na na watanzania bara kutawala Tanzania yote!!??
Huoni kama atakosa legitimacy

Pili itakuwaje iwapo rais wa SMZ atakuwa tofauti kiitikadi na Rais wa Muungano!!???
Namaanisha mfano rais wa Zanzibar angekuwa Saif - Act wazalendo, then Rais wamuungano Jpm-ccm akafariki, huoni kungekuwa na ukakasi !!??
Ni hayo tu
NB; naunga mkono katiba mpya
 
Itakuwa fundisho kwa atakayeshuhudia na atafanya akijua lazima aende na maji hio adhabu ni sawa kabisa tena irushwe live pale uwanja wa Uhuru CCM waaache kutuchezea
Dunia isiyo starabika HAIKUBALIANI na unyama huo. Hasa hasa kwa mifumo ya haki na Sheria ya Afrika ilivyo MIBOVU, watu wengi wasio na hatia watanyongwa na kukosa fursa ya rufaa.

Mahakimu wetu wanakosea sana. Angalia mfano wa Hakimu Thomas Simba akiyewahukumu kina Mbowe na wenzie kwenye kesi ya Akwilina
 
Mifuko ya Hifadhi ya jamii hasa sekta binafsi kama NSSF isisimamiwe na Serikali.

NSSF isimamiwe na vyama vya wafanyakazi

FAO LA KUJITOA iwe haki ya mfanyakazi
😂😂😂😂 nimecheka sana asee
Yani hawa TUCTA, TUGHE, CWT n co wasimamie nssf.
Unautani na mafao ya wastaafu wetu wewe
 
Tutamruhusu vipi Rais wazanzibar ambaye hakuchaguliwa na na watanzania bara kutawala Tanzania yote!!??
Huoni kama atakosa legitimacy

Pili itakuwaje iwapo rais wa SMZ atakuwa tofauti kiitikadi na Rais wa Muungano!!???
Namaanisha mfano rais wa Zanzibar angekuwa Saif - Act wazalendo, then Rais wamuungano Jpm-ccm akafariki, huoni kungekuwa na ukakasi !!??
Ni hayo tu
NB; naunga mkono katiba mpya
Kwani kwa hivi sasa Rais wa Zanzibar akiwa anatoka ACT wazarendo itakuwaje sikia muungano hauongozwi na chama muungano unaongozwa na sheria na katiba kumbuka Katiba ya Zanzibari inasema makamu wa rais wa kwanza anatoka chama cha pili kupata kura nying hilo ni takwa la kikatiba kabisa

Kifungu 37 /5 kinawataja makamu wa Rais ,Jaji mkuu au Spika wa Bunge wanaweza kuwa Marais endapo Rais alie madarakani amekufa au kashindwa kutekeleza makujumu yake sasa spika au jaji amemchagua nani?

Swala la Rais wa Zanzbari kuto chaguliwa huku bara ni swala la kimfumo na kikatiba linaweza badilishwa kwani si yapo mambo ya Muungano ambayo ni 11 mbona Samia anafanya mambo ambayo si ya muungano kama Rais wakati ni Mzanzibari?
 
Nafasi zote kubwa na muhimu anazoteua Rais ziridhiwe na zithibitishwe na kamati husika za bunge.Hizo nafasi ni pamoja na mawaziri wote, jaji mkuu na majaji wengine, DPP, CAG,Mkuu wa Usalama wa Taifa na IGP
 
Madaraka ya rais ni makubwa iwepo check and balance rais awajibishwe kwa kutofuata katiba, jinai, Wizi na ufisadi hata akiwa madarakani.

Kazi za mahakama ziachwe zifanywe na mahakama kama kupatikana kwa Majaji, jaji mkuu, mwanasheria mkuu wa serikali!

Kuondoa utitili wa vyeo kama

Mkuu wa wilaya

Mkuu wa mkoa

Wabaki wakurugenzi

Wabaki wabunge

Wabaki madiwani na meya ndiye awe bosi wa wilaya na achaguliwe na wananchi

Wabunge wagombee wawili yaani mwanamke na mwanaume na lisiwe jimbo iwe kwa kila wilaya

Muda wa kuwa mbunge au waziri uwe mwisho miaka 10

Waziri mkuu na mawaziri wasiwe wabunge wawe wasomi na wapitishwe na bunge na mahakama kwa kufanyiwa vetting na kuangaliwa juu ya record zao za uko nyuma.

Sera ya Elimu iwekwe kwenye katiba hata aje kichaa gani watanzania waweze kusoma bure elimu ya msingi na sekondani na elimu yote i-base kwenye technical education.

Afya tuwe na Sera ya bima kwa watu wote iwe ni lazima kwa kila mtu utengenezwe mfumo wa kila raia kuwa na bima ya bei nafuu na tuwatambue masikini wote wanaoishi chini ya dollar moja kwa siku bima wapewe bure ndani ya katiba.

Ni hayo tu wengine watasema mengine!!
Safi sana!

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
Bunge liinzinishe Teuzi zote za Rais za viongozi wakuu wakiwemo Mawaziri, Katibu wakuu, wakurugenzi angalau hadi ngazi ya wakuu wa mikoa maana they are equivalent to Naibu Waziri.

Kuwepo kisheria kwa tume ya maadili ya wagombea nafasi za kisiasa ishuhulike mpaka ngazi ya madiwani.

Wakurugenzi wa wilaya pamoja na vetting lakini kazi zao waombe kama ajira nyingine. Rais aachiwe kuwatumbua tu.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nimecheka sana asee
Yani hawa TUCTA, TUGHE, CWT n co wasimamie nssf.
Unautani na mafao ya wastaafu wetu wewe
Hayo ni mawazo na hakuna kinachoshindikana baada ya jambo ilo kujadiliwa kwa kina.hivyo vyama sasa tunaviona ni vibovu kwasababu ya mfumo mbovu uliopo hivi sasa.
 
Kwani kwa hivi sasa Rais wa Zanzibar akiwa anatoka ACT wazarendo itakuwaje sikia muungano hauongozwi na chama muungano unaongozwa na sheria na katiba kumbuka Katiba ya Zanzibari inasema makamu wa rais wa kwanza anatoka chama cha pili kupata kura nying hilo ni takwa la kikatiba kabisa

Kifungu 37 /5 kinawataja makamu wa Rais ,Jaji mkuu au Spika wa Bunge wanaweza kuwa Marais endapo Rais alie madarakani amekufa au kashindwa kutekeleza makujumu yake sasa spika au jaji amemchagua nani?

Swala la Rais wa Zanzbari kuto chaguliwa huku bara ni swala la kimfumo na kikatiba linaweza badilishwa kwani si yapo mambo ya Muungano ambayo ni 11 mbona Samia anafanya mambo ambayo si ya muungano kama Rais wakati ni Mzanzibari?
Asante na naomba nijibu kama ifuatavyo.
Kwani kwa hivi sasa Rais wa Zanzibar akiwa anatoka ACT wazarendo itakuwaje?
Kwa sasa kutakuwa hakuna tatizo maana raisi wa Zanzibar siyo makamu wa rais hivyo atabaki kuwa mjumbe wa baraza la mawaziri kama ilivyo.
Pili ndiyo muungano hauongozwi na chama bali katiba na sheria ambazo ndani yake zimetaja kuwa Rais lazima awe mwanachama wa chama cha siasa kilicho sajiliwa haikuishia hapo ikaenda mbali zaidi kuwa lazima awe ameungwa mkono/kuchaguliwa na watu walio wengi/ simple majority. Sasa consern yangu ni anapofariki Rais kutoka ccm unamchukuaje rais kutoka Zanzibar ambaye chama chake ni cha upinzani huku bara, na ataendesha vipi serekali!???
Na huoni itakuwa ni kunyang'anya haki ya chama kilichopata kura nyingi kwenue uchaguzi mkuu ndo concept ya Legitimacy inapokuja.

Mwisho mambo ya muungano yapo 22 na sio 11 kama unavyosema rejea Jedwali la pili la katiba ya JMT. Samia ni Rais wa JMT na mzanzibar hivyo pia ni mtanzania na kwa majukumu yake anafanya mambo yote ya muungano.
 
Hayo ni mawazo na hakuna kinachoshindikana baada ya jambo ilo kujadiliwa kwa kina.hivyo vyama sasa tunaviona ni vibovu kwasababu ya mfumo mbovu uliopo hivi sasa.
Ujie hii nchi sio kisiwa huwezi kuja na preposition ambayo haijatestiwa popote duniani ika apply hapa.
Au utupe mfano ni wapi duniani trade unions zinahodhi securities funds
Ulisikia wapiiii
 
Rais anao wigo mpana sana wa kuteua, anaowaapisha ni wengi sana na sio rahisi kuusimamia ufanisi wa kazi zao. Taasisi nyingi sana zinasimamiwa moja kwa moja na ofisi ya rais. Huu ni udhaifu ambao unajionyesha ikiwa rais hana sifa ya kufuatilia kila kitu yeye mwenyewe kwa nguvu ile ile.

Udhaifu wa kuhodhi madaraka ulijionyesha pale mtu asiye na sifa alipopewa kazi ya kuongoza sekta ya mafuta wakati mtaalam Mataragio akiwepo, baadae usiku yule dogo akaondolewa na barua ya Msigwa ikaandikwa upya.

Kuna wabunge wa viti maalum, hawa kazi yao ni kutengeneza fitina kwa wale wenye majimbo, matokeo yake ni uwepo wa fitina zisizoisha kati ya mbunge mwenye jimbo na wa viti maalum. Wigo wa wanaolipwa pesa ya walipa kodi ni mkubwa sana kulinganisha na ule wigo wa mataifa yanayofadhili bajeti zetu.

Gharama za maisha ya mbunge anayefanyia kazi Washington nyingi ni za kwake binafsi. Mlipa kodi haumizwi na siasa za Marekani. Kwa Tanzania na haswa nchi nyingi za kiafrika tabaka la wanasiasa ni mzigo kwa mwananchi wa kawaida.
 
Kwenye kuajiliwa hapa nakupinga,kwa hiyo waajiliwe maafisa wa tume watakao sambazwa nchi nzima wakati majukumu yao makubwa yako kila baada ya miaka mitano na inapotokea kufanyika uchaguzi mdogo ambao nao mi emergence.Je huo mshahara na masilahi ya kuwalipa wote hao vinatoka wapi? Huo si ndo uhujumu uchumi namba moja?
Kazi ya tume ya uchaguzi si kusimamia uchaguzi tu Kuna kuandikisha wapiga kura wapya na kutoa waliokosa sifa eg kufa na kuhama. Inaweza pia kuomgezewa majukumu mengine Kama mipaka, sensa nk
 
Mawaziri wasiwe wabunge na kamwe wizara zisizidi 15 na wakishateuliwa na rais wafanyiwe vetting na kamati za bunge kabla ya kuidhinishwa na bunge na baadaye kuapishwa na jaji mkuu mbele ya rais.

Spika na naibu wake wasitokane na chama chochote cha siasa na wasitumikie kwa awamu zaidi ya mbili na wasiwe na mamlaka ya kumfukuza mbunge kutoka bungeni.

Kusiwepo na wabunge wa viti maalum ila kila mkoa utoe wabunge wawili akina mama na wachaguliwe na wananchi kwa njia ya kura pia wawepo wabunge na madiwani wa kujitegemea.

Wabunge/madiwani walipwe mishahara tu na posho zisiwepo ili kuzuia watu wasifanye ubunge/udiwani kuwa njia ya kujitafutia kipato.

Halmashauri ziwe huru kuajiri watendaji wake wote na kuwawajibisha inapobidi.

Mgombea mwenza wa rais ndiyo awe kiongozi wa shughuli za serikali bungeni, waziri mkuu asiwepo ni kuongeza gharama zisizo za lazima.

Wakuu wa mikoa wachaguliwe na wananchi na kamwe wasijihusishe na siasa ila utawala tu na wasitokane na vyama vya siasa ila wakuu wa wilaya wafutwe hawana maana na shughuli zao zifanywe na ma Das ambao watafanyiwa vetting hapo hapo mkoani kabla ya kuajiriwa.

"Kila Raia" nchini awe chini ya sheria na akikosea tu sheria ichukue mkondo wake mara moja na itambulike rasmi kwamba hakuna raia muhimu kuliko wengine ila wote ni sawa mbele ya sheria.

Tume ya majaji iwe na mamlaka ya kuunda kikosi kazi kuchunguza kadhia yoyote ya uvunjwaji mkubwa wa sheria ila walio kwenye kikosi kazi wasiruhusiwe kusimamia kesi waliochunguza.

Wadhifa wowote ule unaopatikana kutokana na kupigiwa kura na watu, mtu asiitumikie kwa vipindi zaidi ya viwili. Nk Nk.
 
Madaraka ya rais ni makubwa iwepo check and balance rais awajibishwe kwa kutofuata katiba, jinai, Wizi na ufisadi hata akiwa madarakani.

Kazi za mahakama ziachwe zifanywe na mahakama kama kupatikana kwa Majaji, jaji mkuu, mwanasheria mkuu wa serikali!

Kuondoa utitili wa vyeo kama

Mkuu wa wilaya

Mkuu wa mkoa

Wabaki wakurugenzi

Wabaki wabunge

Wabaki madiwani na meya ndiye awe bosi wa wilaya na achaguliwe na wananchi

Wabunge wagombee wawili yaani mwanamke na mwanaume na lisiwe jimbo iwe kwa kila wilaya

Muda wa kuwa mbunge au waziri uwe mwisho miaka 10

Waziri mkuu na mawaziri wasiwe wabunge wawe wasomi na wapitishwe na bunge na mahakama kwa kufanyiwa vetting na kuangaliwa juu ya record zao za uko nyuma.

Sera ya Elimu iwekwe kwenye katiba hata aje kichaa gani watanzania waweze kusoma bure elimu ya msingi na sekondani na elimu yote i-base kwenye technical education.

Afya tuwe na Sera ya bima kwa watu wote iwe ni lazima kwa kila mtu utengenezwe mfumo wa kila raia kuwa na bima ya bei nafuu na tuwatambue masikini wote wanaoishi chini ya dollar moja kwa siku bima wapewe bure ndani ya katiba.

Ni hayo tu wengine watasema mengine!!
Safi kabisa mkuu
 
Spika na naibu wake wasitokane na chama chochote cha siasa na wasitumikie kwa awamu zaidi ya mbili na wasiwe na mamlaka ya kumfukuza mbunge kutoka bungeni.
Kwa hiyo wabunge wakifanya upuuzi bungeni nani awatoe?
 
Katiba iwe na Kipengele Cha kuruhusu wagombea binafsi ili kuwapa nafasi na wale ambao hawana Imani na vyama vya siasa waweze kugombea nafasi ya Urais, Ubunge na Madiwani .
 
Back
Top Bottom