Vipengele vya Katiba unavyodhani haviko sawa na mapendekezo yako

Kuwepo na kipengele cha kuhakikisha Wakuu wa nchi wastaafu wanadhibitiwa kisheria. Ili wale waliopungukiwa hikma na busara wanapo jaribu kutaka kwa mlango wa uwani kupenyeza agenda zao wakwame. Hii itasaidia hata wasaidizi wa Rais aliye madarakani wajiamini katika kutenda kazi kwao. Sio hii ya sasa ambayo inawafanya wachanganyikiwe ima wamsikilize aliye madarakani au wawafurahishe wastaafu wasije wakapenyezewa fitina tonge likaingia mchanga.
 
Umemaliza ongezea hapo atakaegunduluja kafisadi anyongwe jumatatu pale kwa mkapa iwe siku maalum na vyombo vya habari virushe live
 
iingizwe Adhabu ya kifo kwa wala rushwa na Mafisadi.
Adhabu ya kifo ni kinyume na haki za binadamu. Lengo la adhabu ni "deterrence", yaani kumfanya mkosaji ajutie kosa na asirudie.

Ukishamuua lengo la adhabu linapotea kwa kuwa anakuwa hayupo tena kwa kujifunza
 
Adhabu ya kifo ni kinyume na haki za binadamu. Lengo la adhabu ni "deterrence", yaani kumfanya mkosaji ajutie kosa na asirudie.

Ukishamuua lengo la adhabu linapotea kwa kuwa anakuwa hayupo tena kwa kujifunza
Itakuwa fundisho kwa atakayeshuhudia na atafanya akijua lazima aende na maji hio adhabu ni sawa kabisa tena irushwe live pale uwanja wa Uhuru CCM waaache kutuchezea
 
Kiweke kipengele kinacho taja dira ya uchumi ya Taifa ambayo itakuwa inapitishwa na Bunge kila baada ya miaka 25. Vile vile kuwe na kipengele kinachomzuia Rais kutekeleza dira/ miradi yake binafsi au dira ya chama chake.

Hii itazuia mambo kama haya ambayo Mwendazake ameyafanya kujenga Airport kijinini kwake au alivyoacha kuendeleza mradi wa gesi ya Mtwara na kwenda kukata miti ya Selous Game reserve kwa ajili ya umeme wa 2100 megawatt
 
Mahakama, bunge na tume ya uchaguzi zijitegemee.

Kiandaliwe chombo Cha kuchagua Jaji mkuu, mkurugenzi wa time ya uchaguzi na jinsi ya kupata spika ikiwezekana atoke nje ya vyama vyenye wabunge ndani ya bunge.

Rais asiteuwe wakuu was mihimili inayojitegemea.
 
MI NAOMBA TANZANIA IUNDWE UPYA KUWA MOJA. KATIBA MOJA, RAIS MMOJA, BUNGE MOJA NA MAHAKAMA MOJA. CHINI YAKE NI MAJIMBO. KIFUP KUSIWEPO BARA NA VISIWAN AU TANGANYIKA NA ZANZIBAR
 

Mkuu umehitaji maoni huru bila kuvaa jezi wakati wewe umesheheni maoni lukuki ukiwa umevaa jezi.

Ya Kenya umeyapotosha kwa maslahi ya jezi ulilovaa.

Kwa kuyatambua mapungufu hayo ya dhahiri, itoshe sasa kukupa baadhi ya mapungufu ya wazi ya katiba iliyopo, ambayo yanaweka umuhimu na dharura ya katiba mpya hasa kwa mtanzania yule wa kawaida:

1. Katiba iliyopo haiwawajibishi baadhi ya watendaji wakuu kwa kuikiuka, na hii ni kwa mujibu wa katiba yenyewe.
2. kwa katiba iliyopo pana watu hata kama wakiiba, wakipora, wakiuwa, wakidhulumu nk hiyo ni halali kwa mujibu wa katiba yenyewe.
3. katiba iliyopo inawapa baadhi ya watu mamlaka ya kujifanyia lolote bila kuhojiwa au hata kuwajibishwa tu.
4. Katiba iliyopo haitoi haki sawa kwa watu wote ndani ya nchi.
5. Kuna mianya mingi katika katiba hii ambayo inaweza kuifanya mihimili mingine hata kupoteza uhuru wake wa kiutendaji kwa mujibu wa katiba yenyewe.
6. Kuna utitiri wa nafasi za uongozi wasio na tija wala ridhaa ya wananchi ambao pia ni mzigo mkubwa kwa mlipa kodi.
7. Kuna utitiri wa vigogo wenye mapato yasiyoakisi tija, wala kuwa na ridhaa ya wananchi na wasiolipa kodi wanaopata uhalali kwenye katiba hii.
8. Kwa katiba hii polisi wanaweza mshikilia mtu kwa kumbambikizia kesi hata kwa miaka kadhaa. Mhanga akaja kuachiliwa bila ya wahusika kuwajibika kwa lolote. Hili likihalalishwa na katiba hii.
9. Nk.Nk.

Yako mengi ila umevaa jezi mkuu yaani hata kuandikia ni ukakasi mtupu!

Hata hivyo, kwenye mazingira haya hudhani kuwa mwananchi wa kawaida anaihitaji zaidi katiba mpya kuliko hata hao wanasiasa?

Kwamba, hudhani kuwa anayedhani hahitaji katiba mpya ni kwa sababu tu ya ujinga wake au kukosa elimu au kuwa na uelewa mdogo tu?

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Katiba itamke wazi kwamba hayupo aliye juu ya sheria, raia wote wako sawa mbele ya sheria......rais akiiba kuku ashtakiwe sawa na kijana wa uswazi aliyekwiba kuku. Hizo kinga walizowekeana hadi kina ndugai ziondolewe, tutambue kwamba aliye juu ya sheria ni Mungu Mwenyezi pekee. Ikiwa Mungu anaweza kuapa kwa jina lake kuu na asiende kinyume na kiapo chake, itakuwa binadamu bhanaa............

Kingine, endapo rais amefariki au ameshindwa kufanya majukumu yake, jaji mkuu akaimu nafasi kwa kipindi kisichozidi miezi sita na uchaguzi mwingine ufanyike......
 
Umeambkwa vipengele gani umekimbilia u-DC. U DC ni kipengele? Pumbavu!!!

Anapewa vipengele vya nini aliyeomba maoni huru bila kuvaa jezi wakati yeye kasheheni maoni lukuki yasiyo huru, huku dhahiri akiwa katupia jezi ya kijani kama mburumundu tu?!
 
Wewe ni mzima au umekimbia matibabu? Mbona unatukana watu hovyo wakati mleta mada kimsingi kataka maoni.
Mtoa mada kaulizia "vipengele". Huyo niliyemjibu Kuna kipengele kakionesha? Pumbavu!
 
Rangi ya katiba iwe kijani au njano kama timu ya wananchi
 

Ile Rasimu ya warioba ilikuwa KONKI sana...Waipitishe ile tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…