Vipi kauli ya Kagame kuwa Rwanda ingekuwa na bandari kama ya Dar, huduma zote Rwanda zingekuwa bure?

Vipi kauli ya Kagame kuwa Rwanda ingekuwa na bandari kama ya Dar, huduma zote Rwanda zingekuwa bure?

Sio nchi ya majaribio hii. Hayo majaribio endeleeni kufanya huko kwenye ndoa zenu.
Hakuna sayansi isiyo na majaribio.Huwezi kujua matumizi ya ugunduzi wa zana yoyote mpya mpaka ujaribu.Damper usitu aminishe kama hukwenda shule!
 
Wanasiasa Ni porojo Tu,Kikwete nae husema kama Tz ingekuwa ndogo kama Rwanda,tungekuwa mbali mno kiuchumi.

Usiumize kichwa bure kwa vitu ambavyo huwezi vibadili as an individual!Hata kama Upinzani ukishika dola 2015 hakuna lolote litakalobadilika rushwa imekita mizizi mpaka level ya family.
 
Sir magdalena kazi nafanya kwa bidii lakini ujira hautoshi mahitaji yangu niambie kama umeme juu mafuta juu dawa juu chakula juu nyumba juu sasa hapa nita achaje kuandamana???Amani ya Bwana iwe nawe Sr!

Sr. Magdalena jibu uzi huu tafadhali
 
Last edited by a moderator:
Vyombo mbalimbali vya habari viliripoti kuhusu kauli hii ya Raisi wa Rwanda Paul Kagame kuwa Kuwepo kwa Bandari ya Dar Tanzania ilipaswa kupaa kabisa kiuchumi hasa kutokana na kuzungukwa na nchi kadhaa zinazo tegemea kusafirisha mizigo yake.

Zipo nchi nyingi duniani ambazo kwa bandari pekee zimepata kupaa kiuchumi miongoni mwao ikiwamo Hongkong ,Singapore,Uholanzi nk.Lakini kwanini Tanzania Hatuoni mabadiliko ya kiuchumi yakiwa dhahiri kutokana na bandari hii?

Miradi mingi ya kiuchumi ni mikopo toka kwa wahisani.Barabara kama ya DOM-IRINGA ni mkopo toka Benki ya Africa,na miradi mingi ni mikopo toka kwa wahisani kiasi sasa kila Mtanzania mpaka mtoto mdogo anadaiwa zaidi ya Tsh 450000(laki nne na nusu).Fedha za mapato kama ya bandari hii huenda wapi?Kuna harufu ya ufisadi wa mapato ya bandari kwa kiasi kikubwa.

Napata shaka kuona kuna benk kama M Benki imbayo tawi lake limo ndani ya jengo la ofisi za mapato.Mtu analipia pale na document yake ni halali palepale na mzigo unatoka.

Hii benki niya nani?Benki zingine ukilipia document yake mpaka mpaka iende hazina ku verify ndipo uchukue mzigo.

Naona kama mafisadi wananjia zao za kuchota hela kirahisi kama kupitia benki hii,labda ndiyo maana hatuoni mabadiliko yoyote ya kiuchumi.

Gari moja ndogo inayo pita kwenda nchi nyingine hulipia sichini ya 3000000/=(milioni tatu) na gari pale zinapita kama maji tu.Pita barabara ya Dar-Tunduma uone gari zenye number ya IT utapata picha ya hoja hii pata picha ya 300.

Kagame yupo sawa. Hii nchi pamoja na makusanyo ya kodi na Ushuru machache lakini nyingi zinaishia mikononi mwa wajanja.
 
Mtowa mada upumbavu wako umeelekeza kwenye siasa ukamwambie huyo kagame wako abadili uraia nchi ya rwanda ukubwa kama mkowa wa daresalam mbona akuitaja kenya kaitaja tanzania
 
Acheni kukariri wote hakuna aliyefika Rwanda sanasana mnaona katikati ya mji kwenyetv fanyeni utafiti msikalie tu kunywa viroba na kusikia ya kuwaambiwa. Hakuna nchi kama Tanzania ktka bara la afrika kusini mwa jangwa la sahara
 
Acheni kukariri wote hakuna aliyefika Rwanda sanasana mnaona katikati ya mji kwenyetv fanyeni utafiti msikalie tu kunywa viroba na kusikia ya kuwaambiwa. Hakuna nchi kama Tanzania ktka bara la afrika kusini mwa jangwa la sahara
Hakuna nyingine katika nini? mkuu uwe specific.Unatakwimu gani?
 
Hakuna maendeleo yasiyo na mipango na uwajibikaji kwa yale mnayoyapanga.watanzania hata tutatamani rais awe nani kama hatutawajibika kufanya kazi kwa ufanis bila kuwaza kuwa hakuna huduma isiyoambatana na rushwa tutaendelea kutoa mifano tu.
 
Huyo ---- anajisifia ujinga, amepata mafanikio kidogo ya dhulma kwa kuuwa waCongomani na kuiba raslimali zao. Jehanam inamsubir kwa hamu. Thanks JWTZ wanastruggle kuikomboa DRC.
 
uholanzi, hongkong, singapore,,, usitolee mfano TZ na hizi nchi, rudi nyuma 1700 t0 1800 uone hawa walikuwa wapi na sisi tulikuwa wapi.

unapoongelea tz jaribu, kuifananisha na nchi nyingine, za africa.. tanzania ni ya 13 kwa GDP kwa africa kenya ni ya 12. hiyo ghana ulioitaja ni ya 9 huyo kagame na ruanda yake uliowataja wako chini huko. (rejea hizi taarifa kwenye mitandao utaona)
ni kweli tanzania inasumbuliwa na ufisadi kama zilivyo nchi zote za africa (hii ni tabia ya waafrica, ambayo bila shaka hata wewe unayo).
KAGAME ni mtu ambaye amefanya yakwake kwa nchi yake na sio yote amefanya KIGALI, tena kwa msaada aliopewa na jumuia ya kimataifa wakati wa GENOCIDE.(huu ni msaada alipewa na sio mkopo kwa ajili ya kuijenga RWANDA) kwa hiyo asijisifie kabisa kwani hii ni sawa na wale wanaopewa mitaji na baba zao halafu ukawacompare na wale wanaofight wenyewe. nafikili unasikia jinsi gani watu wanavyoikimbia RWANDA.
Kama watanzania tunatakiwa tuwape viongozi pressure mda wote (waafrica, hatuwapi direct pressure watawala, tunaishi kinafiki sana).

mkuu omba upate nafasi ya kuzungukia nchi nyingi za africa, utaona jinsi gani tunavyofanana kimaisha na kiuchumi, ni uongo mtu kusema kuna nchi ya africa (ukiondoa waarabu na s/africa kuna sababu zake) imeendelea wote tuko sawa utapoongelea umasikini wa tanzania, unaongelea umasikini wa AFRICA. Tutakiwa wote tuwe wazalendo kwa africa, tufanye kazi kwa bidii, tuache unafiki, tuwape watawala direct force ya kufikia malengo.
 
Hakuna nyingine katika nini? mkuu uwe specific.Unatakwimu gani?

Kama hujafika ni wewe, Mkuu Kagame anamapungufu yake ila kwenye mazuri lazima tuseme. Kwenye suala la uchumi na uwekezaji Yuko vizur. Na mengi anatumia sera za huku huku. Mfano aliiga kwetu uanzishaji wa One stop center na kafanikiwa saana tofauti na kwetu, usimamizi wa bodaboda na sheria ya leseni za biashara za usafiri kwa njia ya bodaboda kafanikiwa sana. Sisi SUMATRA hii sheria imewashinda kupractic. Tz tunamipango na sera nyingi zisizotekelezeka tofauti na wao. Anaebisha aende na ubabaishaji wenu. Binafsi nimevutiwa sana na mazingira ya uwekezaji ya Rwanda.
 
Back
Top Bottom