Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

mimi ndo hata mlango wa airport sijauona nna miaka kadhaa sijaelekea ukonga[emoji23], ndege naziona angani tu!!!
na kwenye movie na media!!!

umasikini mbaya sana!!
 
mimi ndo hata mlango wa airport sijauona nna miaka kadhaa sijaelekea ukonga[emoji23], ndege naziona angani tu!!!
na kwenye movie na media!!!

umasikini mbaya sana!!
Usijali mrembo, faza haus analeta vyombo vingine vi4 vya maana mbona ntakukatia tu tiketi one day.

Mkoani kwako ni wapi? Kama kwenu Mkuranga imekula kwako
 
Naomba tushee experiences siku yako ya kwanza kupanda ndege ilikuwaje?
-inapoanza kukimbia kwenye run way
-inapo take off
-inapokuwa mawinguni
-inaposhika

Ulipokuwa ndani ulijishughulisha na nini?
Nina safari ya Angola, roho ina ninduda dunda hapa!
Unapanda ndege ya shirika gani? Mi niliona kawaida ila ikiwa angani (mawinguni) kuna wakati inakuwa kama umepanda gari linalopita kwenye mashimo, hali hiyo kwenye denge wanaita turbulence. Inaogopesha kama ni mara yako ya kwanza.
 
mimi ndo hata mlango wa airport sijauona nna miaka kadhaa sijaelekea ukonga[emoji23], ndege naziona angani tu!!!
na kwenye movie na media!!!

umasikini mbaya sana!!
Usihuzunike kwa kutopanda ndege,Bombadia zipo utaondoa huo ushamba
 
Mimi ilikuwa 2007 nilipata ride ya kwenda serengeti, nikapiga suti na scaf; kuingia kwenye ndege (hizi ndogo za watu 12) nakuta watu wamevaa simple sana kwa kuwa wanaenda bush; nilijisikia vibaya sana...
hahahahahhah
 
Mi wala sikuwa na mcheche. Nadhani kwavile haikuwa ukubwani, hahahhhaaaa!!!. Ila kuna siku tunatoka site (mgodini), kuna jamaa yangu alikuja kwenye interview. Kwahiyo siku anaondoka na mimi ndiyo naenda likizo. Tukapanda wote kindege cha watu 12 toka site. Hichi kindege (huwa nakiita kibajaji) sometimes mkiwa hewani kinajiachia kama pangaboi limezimika vile. Lazima ung'ang'anie siti mazee. Basi jamaa yangu ilikuwa full kung'ang'ania siti. Akinicheki mi nimeuchapa usingizi mwanzo mwisho. Ile karibia tufika Dar akaniuliza ''we jamaa umewezaje kulala?''. Mi nikabaki nacheka.
 
Hahaha sitosahau siku nilozunguka OR TAMBO karibia nusu saa nzima maan nilipotezana na wenzangu kwenye lain ambayo tulikuwa ndege moja wacha nizunguke mle ndani mpk nabahatika kuona pale pa kuchukua ticket ilikuwa nishachoka yaan naingia tu kweye ndeg nimekaa muda kidog tu ndege ikaanza kuondoka ningeachwa maan ilikuwa hata matangazo siyasikii kweli ushamba mzigo
 
Sitasahau siku hiyo nimepanda kwa mara ya ndege tukafika kwenye tabaka la OZONE kuchimba dawa ,aiseeee ilikuwa patashika.
 
Nimefarijika sana na huu Uzi na kujiona Mimi Nina nafuu kidogo. Mi kwa Mara ya kwanza nimepanda last month kwenda Mwanza na precision na kabla ya kuanza niligonga mvinyo kidogo ili kupata ujasiri lakini kale kamngurumo kikali wakati ndege inapaa plus zile style zake za kukata kona angani na ule mtetemeko mawinguni kulinimalizia stimu zangu zote aisee. Ila mambo mengine kama kufunga mkanda au kufungua viti vya kuweka msosi niliona kawanda sana
 
binafsi naendelea kujipanga siku naoa honeymoon niende na mke wangu kwenye VISIWA VYA VANUATU hukoo
 
aisee ndege bado naitafakari iweje dude zito vile lipae hewani masaa kadhaa bila kuanguka. Shikamoo Mkoloni mweupe.
 
Dah! ndege ina speed jamani nilipanda AURIC AIR toka Njombe to Iringa ile naingia tu nasogea kwenye siti yangu ili nikae naambiwa "wa kushuka Iringa",nikadata nauliza wa kushuka Iringa mnamaanisha nini,yule kaka akasema tushafika Iringa,sikuonja hata siti ya ndege ikanibidi nishuke maana tuliisha fika Iringa,duh! ndege inakimbia jamani!
Hizi sound... braza[emoji3] [emoji3] [emoji3]
 
Sasa unaturingishia kwamba umepanda sana ndege?Kweli ushamba mzigo.

Nakumbuka ilikuwa Mwaka 2008 mwezi Juni nilikuwa naenda kikazi Lusaka, Zambia basi sijui hili wala lile kwenye tiketi iliandikwa saa ya ndege kuondoka saa 12 asubuhi (ndege ndo inapaa) mimi nikajipa kama dakika 20 kutoka home Tabata mpaka Airport, nikidhani ni kama Mabasi ya Mkoani pale Ubungo stendi duuh ile kufika nikaambiwa muda umeisha daah! Nilichokaje. But taratibu nikajifunza muda wa kufika airport, vitu visivyoruhusiwa kubeba kwenye ndege.

**NEW DEVELOPMENT
Mwezi Juni 2015 nilipata safari ya kwenda CAMEROON (kwa hisani ya Watu wamarekani USAID) sasa tukiwa huko tukalipwa posho kwa hela ya huko Central African Franc sasa nikazibana nije kubadilishia Bongo nafika bongo Bureau De Change zote hawabadilishi hizi pesa yaani nmepagawa sijui nikazitupe Coco maana....


****MPYA ya 2016
Mwezi Januari nilienda NEW DELHI duuh pale airport hakuna sijui kutangaza wala nini ni KIMYA KIMYA tu ukisubiri matangazo utastukia ndege ishakuacha.



HAKIKA USHAMBA MZIGO!
 
Back
Top Bottom