Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

Bibi alpiniambia nifumbe macho. Kabla ya kupaa kuna maneno aliyasema. Nikamuuluza bibi mbona ndege ni ndogo watu ni wengi?
Bibi akanicheka sana.
Lakini ulikuwa ni ushamba. Ila kwa sasa naruka hadi NIGERIA peke yangu.
 
Bibi alpiniambia nifumbe macho. Kabla ya kupaa kuna maneno aliyasema. Nikamuuluza bibi mbona ndege ni ndogo watu ni wengi?
Bibi akanicheka sana.
Lakini ulikuwa ni ushamba. Ila kwa sasa naruka hadi NIGERIA peke yangu.
Daaah Hongera saaana
 
Mimi ilikuwa 2007 nilipata ride ya kwenda serengeti, nikapiga suti na scaf; kuingia kwenye ndege (hizi ndogo za watu 12) nakuta watu wamevaa simple sana kwa kuwa wanaenda bush; nilijisikia vibaya sana...

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Tuseme UKWELI bila UnAFIKi ATCL imetupatia HESHIMA kubwa sana. Leo hii inatua OR Tambo International Airport daah tumetoka mbali aisee. HEKO HEKO HEKO!
 
Tuseme UKWELI bila UnAFIKi ATCL imetupatia HESHIMA kubwa sana. Leo hii inatua OR Tambo International Airport daah tumetoka mbali aisee. HEKO HEKO HEKO!
Heshima ya karne. Sasa wanatua BUKUMBURA, OR Tambo, Mumbai, Moroni, Comoros, na punde Gatwick, Guanzhou, London. Inshallah JF Kennedy, Sydney, Berlin, Muscat, Madinna, Mecca, Dubai na Rome.
 
Mara ya kwanza kusafiri nilikuwa naenda Sehemu hivi kupitia Paris. Ila siku hiyo ndege ya Air France ikawa imeharibika na hivyo ikaja ndege ya Madagascar Airlines Boeng 747, mzinga wa pipa.

Uzuri ni kuwa nilipigwa shule nyumbani nzuri sana jinsi ya kufunga mkanda, kulaza kiti na kukirudisha, kufungua headphones na kuzitumia na wapi zipo tundu za kuchomeka.

Ila nakaa, pembeni kuna Dada wa Kiganda na Mudhungu wake, akawa anahangaika jinsi ya kufunga mkanda, bwana wake akamsaidia kufunga. Sijui siku hizi anajisikiaje akikumbuka ushamba huo wa siku ya kwanza.

Kasheshe ilikuwa wakati wa kula. Ila Mungu bariki nilishaambiwa kuwa kuna vikaratasi vya kufuta uso na asubuhi mnaletewa taulo za motomoto kufuta uso pia. Msosi kufika, maajabu matupu kwani nusu ya vyakula navifahamu na nusu sivifahamu. Mie na kundi langu lote tukawa tumekubaliana tutakula kila kitu na hatubakizi hata kama watakuwa CHURA wa Kifaransa maana hawa jamaa WALA VYURA hawakawii kumlisha mtu nyama zao.
Kila kitu kilienda safi ila ikawa kasheshe kuzila OLIVE ila nikajikaza nikazila. Kulikuwa na nyama nyeusi nyeusi, sikujali ni nini, nikazila bila huruma. Mwisho vikabaki vipaketi vitatu. Kimoja kukifungua ni Sukari, nikaibugia. Kingine kufungua ni jibini, nikaila bila huruma. Cha mwisho kufungua (nilikuwa nafahamu unafungua kwa kuvunja ncha iliyochomoza) ikawa kumbe maziwa ya kwenye kahawa ambayo nilishaimaliza mapema sana bila sukari wala maziwa. Basi nikaangalia kushoto kulia hakuna anayeangalia, nikabugia. Mwisho nikasema hata kama Mjinga fulani kaniona, sijali maana hatakuja kuniona tena. Mwisho sahani yote ikawa tupu na wakaja akina dada kuchukua makasha matupu.

Kuna jamaa alikuwa anawasumbua akina dada kuagiza pombe basi ilipofika saa 9 usiku, wakamuita na kumuonyesha Friji la Pombe lilipo na wakaenda kulala. Jamaa alipofika Paris, alikuwa anatambaa kutoka ndani ya ndege.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nilisafiri na bibi kizee toka Kigoma kuja Dar, njia nzima alikuwa analalamika bora wamshushe, alilaani kitendo cha kupakiwa kwenye ndege, moja ya sentesi aliyosema ni kuwa wanawe bora wangemuua kwa sumu kuliko kumuua kwa ndege, tuliposhuka Dar baba mmoja alikuwa anamsikia akilalamika juu ya usafiri wa ndege, akamtania akamwambia bibi umesahau kanga kwenye kiti chako ndani ya ndege, akamjibu akamwambia wacha iende naweza kurudi humo ndani kuchukua nguo, wao wakaondoa ndege ghafla waanze kunizungushazungusha angani,
[emoji23][emoji23][emoji23] da nimecheka sana,bibi anaokiona kifo laivu
 
Duuh ulifikiri ndege ni mabasi ya mkoani. Mimi nakumbuka nilibebda manukato (perfume) kwenye begi basi kwenye ukaguz nikaambiwa hairuhusiw kusafiri na perfumes kwa kiwango hicho nikaambiwa niache hapo. Anyway ndo kujifunza huko.
Manukato hayo wale wakaguz waliondoka nayo kwao
 
Mimi ilikuwa 2007 nilipata ride ya kwenda serengeti, nikapiga suti na scaf; kuingia kwenye ndege (hizi ndogo za watu 12) nakuta watu wamevaa simple sana kwa kuwa wanaenda bush; nilijisikia vibaya sana...
Ha ha haaa boss umeua
 
Back
Top Bottom