Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

Mara ya kwanza ilikuwa from mtwara to dar zamani kidogo sasa siku hyo hali ya hewa ilikuwa mbaya sana bonge la mvua nipo na broo hapo tukiwa hewani tukaskia rubani anatangaza hali ya hatari hapo ni full mtikiso ndani kama vile kuna mashimo barabarani kila mtu anaomba mungu tena, nilijuta hata kuwa na kiherehere cha kupanda ndege namchek bro wanakata wine na mzungu mmoja iv wanagonga cheers kabisa mpaka watu wanawashangaa........lakini tulifika salama na ilinichukua muda sana kukubali tena kupanda ndege niliamini ule ndo utaratibu na haikuwa salama. Bt nw nshazoea
 
Dah! ndege ina speed jamani nilipanda AURIC AIR toka Njombe to Iringa ile naingia tu nasogea kwenye siti yangu ili nikae naambiwa "wa kushuka Iringa",nikadata nauliza wa kushuka Iringa mnamaanisha nini,yule kaka akasema tushafika Iringa,sikuonja hata siti ya ndege ikanibidi nishuke maana tuliisha fika Iringa,duh! ndege inakimbia jamani!

Haaahaa haikimbii inapaaaa
 
Me bwana nilipanda ndege inaitwa leina tours.dar kahama.
 
Kiukweli natamani sana kupanda ndege yaani ni raha tupu na vile vidada vya kwenye ndege ndo balaa vinatamanisha hasa.
 
ilikuwa mwaka jana tu mwishoni natoka arusha kwenda dar na fashtjet, nikaandaa elfu 10 angu nimnunulie mama angu matunda pale koogwe,haaaa kutahamaki dk 50 mbele tuko kipawa hatujapitia kununua matunda!dah kwei ushamba mzigo!!
 
safari za ndege tamu hasa za ruti ndefu,emirate airlines,turkish,qatar na egypt airways
 
mi naitamani sana KLM aisee mara nyingi huwa nalionaga pale KIA likitua na kupaa Nalitamani nilipande siku moja nikiwa naenda huko mbali sana sijui RUSSIA sijui wapi huko, yaani hapa najichanga tu nizushe trip ili mradi nikwee dude la KLM, wazungu wanafaidi sana aisee
 
Ndugu BLESSINGS umeniacha hoi kwa jinsi unavyolitamani Li-KLM jipange tu siku utalipanda.
 
secrete naitamani haswaa KLM maana naionaga tu pale KIA full Wazungu ndo wanakwea humo, nasikia likitoka KIA linatua tena DAR kabla halijapaa tena mpaka AMSTERDAM daah! kwa kweli ndege raha sana
 
Nakumbuka ilikuwa Mwaka 2008 mwezi Juni nilikuwa naenda kikazi Lusaka, Zambia basi sijui hili wala lile kwenye tiketi iliandikwa saa ya ndege kuondoka mimi nikajipa kama dakika 20 hivi ndo niwe Airport duuh ile kufika nikaambiwa muda umeisha daah! Nilichoka. But taratibu nikajifunza muda wa kufika airport, vitu visivyoruhusiwa kubeba kwenye ndege.

HAKIKA USHAMBA MZIGO!
Ulikuwa mzembe wa kusoma hukuiona reporting time.
 
Back
Top Bottom