Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

cc: Tembele... ukitaka kubatasamu usiache pitia huu uzi
 
Last edited by a moderator:
Ha ha pale airport wanashuhudiaga vitimbi aisee kuanzia wasindikizaji mpaka wasafiri hususani wa fastjet
 
kuna siku nimeenda kumchukua mshua usiku nikakuta jamaa wamekuja na DCM mbili na matalumbeta wamekuja kumpokea ndugu yao kwi kwi kwi kwi kwi kwi mimi nilipata ushamba kwenye vile vitololi kumbe unatakiwa ukibonyeze ndio kitembee sasa mimi nilikomaa kusukuma hivyo hivyo hadi kwenye gari da niliteseka kinoma
 
Wale jamaa wanaokagua huwa wanafaidigi sana perfume za watu pia ukizubaa wanachomoa pesa kwenye wallet wakati umeweka kwenye kile kisinia
 
baada ya gradu yangu chuo.Tukarudi mkoa na maza. Fastjet ndo imeanza.Nı mara yetu ya kwanza wote.
1. Mama anataka kukaa akakuta juu ya siti sehemu ya mizgo kuna mtu kashaweka wake.Akatia,"wee kondaa,we kondaa wéeh,hebu njoo kwanza"

2. Nikajaribu kwenda choóni japo sijabanwa alimradi tu nione pakoje

3.Facebuk page yangu iliomba poo. Mara checkin in at JKİ Airport. Mara nitupie picha alimradi kila mtu ajue.

4. Tulivofika madreva tax wakaanza kututukana eti "hamna lolote nyie mtakuwa fastjet tu" hapo kisa ni baada ya wao wanatugombania sie hatuna time tunaenda kwny daladala.

5. Jioni napokea simu toka kwa mjomba: "ah mjomba nimeamini ushamba mzigo wa mwiba".Nkamuuliza kwanini? Akasema,"leo sina raha. mama yako kutwa nzima anantambia kwny simu kisa kapanda ndege"
Hahaha mkuu umetisha, dah maza anaita konda kwenye ndege! Dah nimecheka sana
 
Mie siku napanda arusha to Dar za ardhini inaitwa ngorika ilivyokuwa inakimbia nilidhani tunaenda kwa ISRAELI kila akitaka ku overtake nafunga macho.

Chakula cha mombo kiliniondoa stress kwani sikutegemea kula wali nyama wa 2000 wenye nyama ya ukweli. Muda si mfupi tumeanza safari tumbo likaanza nilitamani wanishushe nimalizie kwa miguu nilipoambiwa utashushwa wami nilijikaza kisabuni
Mkuu mimi hii ndege ya chini nilipanda kipindi kile ngorika inafukuzana na buffalo, gari za kwanza asubuhi. Wacha kabisa! Nilipofika korogwe nilishuka mwenyewe
 
Mkuu mimi hii ndege ya chini nilipanda kipindi kile ngorika inafukuzana na buffalo, gari za kwanza asubuhi. Wacha kabisa! Nilipofika korogwe nilishuka mwenyewe

Shukuruni Mungu ajali hazikuwa nyingi kama sasa mngeshasahaulika.
 
Mara ya kwanza nilipanda KLM. Sikuthubutu kula hata kunywa maji kwani nilikuwa naogopa kwenda chooni. Kweli ushamba mzigo. Sikujua hata jinsi ya kupunguza fen baridi ilipozidi. Duh! Acha tu. Halafu safari ilikuwa ya kwenda London.
 
Hivi kwa nini airport KIA unacheck in kwanza alafu ndio unapita security check, kwa hiyo kama una liquid ya zaidi ya 100mls ndani ya begi usioingia nalo kwenye ndege inapita. Airport ya Dar tofauti. Kabla ya kucheck in lazima upitie security.

Hapo mls 100 unaziacha hata kama zipo kwa check in bag. Kwa nini kuna hii tofauti?
 
Mimi mwaka 2013 natoka Kia/dar,..sisahau ile ndege inaruka tu nilihisi km utumbo unageuka..ilinitoka tu Mungu wangu we..,jamaa pembeni kanipiga jicho hilo nikajifanya ile mungu wangu km nilisahau kitu airport kumbe mchechetu,huko juu ndo balaa maana sikuwahi na amani hd inashuka Dar ..dah ushamba bana.
 
Hivi kwa nini airport KIA unacheck in kwanza alafu ndio unapita security check, kwa hiyo kama una liquid ya zaidi ya 100mls ndani ya begi usioingia nalo kwenye ndege inapita. Airport ya Dar tofauti. Kabla ya kucheck in lazima upitie security. Hapo mls 100 unaziacha hata kama zipo kwa check in bag. Kwa nini kuna hii tofauti?

Wa Dar wezi tu wanazichukua wao,inatakiwa vilokuwemo ndani Ya cargo vipite tu isipokuwa vya mkononi utakavyoingia navyo ndani,Dar wezi sana wanajifanya wa mjini.
 
Mara ya kwanza kusafiri nilikuwa naenda Sehemu hivi kupitia Paris. Ila siku hiyo ndege ya Air France ikawa imeharibika na hivyo ikaja ndege ya Madagascar Airlines Boeng 747, mzinga wa pipa.

Uzuri ni kuwa nilipigwa shule nyumbani nzuri sana jinsi ya kufunga mkanda, kulaza kiti na kukirudisha, kufungua headphones na kuzitumia na wapi zipo tundu za kuchomeka.

Ila nakaa, pembeni kuna Dada wa Kiganda na Mudhungu wake, akawa anahangaika jinsi ya kufunga mkanda, bwana wake akamsaidia kufunga. Sijui siku hizi anajisikiaje akikumbuka ushamba huo wa siku ya kwanza.

Kasheshe ilikuwa wakati wa kula. Ila Mungu bariki nilishaambiwa kuwa kuna vikaratasi vya kufuta uso na asubuhi mnaletewa taulo za motomoto kufuta uso pia. Msosi kufika, maajabu matupu kwani nusu ya vyakula navifahamu na nusu sivifahamu. Mie na kundi langu lote tukawa tumekubaliana tutakula kila kitu na hatubakizi hata kama watakuwa CHURA wa Kifaransa maana hawa jamaa WALA VYURA hawakawii kumlisha mtu nyama zao.
Kila kitu kilienda safi ila ikawa kasheshe kuzila OLIVE ila nikajikaza nikazila. Kulikuwa na nyama nyeusi nyeusi, sikujali ni nini, nikazila bila huruma. Mwisho vikabaki vipaketi vitatu. Kimoja kukifungua ni Sukari, nikaibugia. Kingine kufungua ni jibini, nikaila bila huruma. Cha mwisho kufungua (nilikuwa nafahamu unafungua kwa kuvunja ncha iliyochomoza) ikawa kumbe maziwa ya kwenye kahawa ambayo nilishaimaliza mapema sana bila sukari wala maziwa. Basi nikaangalia kushoto kulia hakuna anayeangalia, nikabugia. Mwisho nikasema hata kama Mjinga fulani kaniona, sijali maana hatakuja kuniona tena. Mwisho sahani yote ikawa tupu na wakaja akina dada kuchukua makasha matupu.

Kuna jamaa alikuwa anawasumbua akina dada kuagiza pombe basi ilipofika saa 9 usiku, wakamuita na kumuonyesha Friji la Pombe lilipo na wakaenda kulala. Jamaa alipofika Paris, alikuwa anatambaa kutoka ndani ya ndege.
We kiboko dohhh....umebugia jibini na sukari teh nimecheka sana!!
 
Ningekuwa na uwezo ningewapiga marufuku wale wafanyakazi wanaoelekeza jinsi ya kufanya in case of emergence..makes you feel like you are one step from death...hates vindege vidogo vya Dar-Mwanza visivyogawa pombe...gotta be intoxicated enough kutowaza kifo safari nzima

Can easily understand Denis Bergkamp
 
teh teh teh uwiiiii mbavu zangu mie mtoto wa marehemu!!!!

Mie nilikusanya vitambulisho vyote mpk vya drs la saba, birth certificate mpk death certificate za wazazi wng nikidhania ukifika kwenye mlango wa ndege unakaguliwa!!

Nikajisemea moyoni wakikataa hiki natoa hiki!!! mweeee ama kweli ushamba mzigo...
 
Mimi mara ya kwanza mwaka 2004 nlipanda precision air.

Sasa tylipokuwa angani nikaenda chooni. Nlivoingia nikaanza kujiuliza " hivi hiki choo ni cha kukaa au kuchuchumaa?". Duh! Akili zangu za uswazi zikanambia chuchumaa.. basi nikaparamia sinki na kushusha mzigo... duh.. noma kweli!

Return trip ndo nlifigure out kuwa ni cha kukaa.. hii sijawahi kumsimulia mtu yoyote... huwa nikikumbuka nacheka sana..
 
Mie siku napanda arusha to Dar za ardhini inaitwa ngorika ilivyokuwa inakimbia nilidhani tunaenda kwa ISRAELI kila akitaka ku overtake nafunga macho.

Chakula cha mombo kiliniondoa stress kwani sikutegemea kula wali nyama wa 2000 wenye nyama ya ukweli. Muda si mfupi tumeanza safari tumbo likaanza nilitamani wanishushe nimalizie kwa miguu nilipoambiwa utashushwa wami nilijikaza kisabuni

Nimeipenda sn hii aisee
 
Mimi mwaka 2013 natoka Kia/dar,..sisahau ile ndege inaruka tu nilihisi km utumbo unageuka..ilinitoka tu Mungu wangu we..,jamaa pembeni kanipiga jicho hilo nikajifanya ile mungu wangu km nilisahau kitu airport kumbe mchechetu,huko juu ndo balaa maana sikuwahi na amani hd inashuka Dar ..dah ushamba bana.
Hiyo ni Kama mm Pemba to Unguja 2007 ndo Mara ya kwanza achaga tu maana nilikuwa kituko kwa wataliii hewani kutangatanga c unajua kule bahari mkiruka tu kisiwa unajiona kiiiiiiileeeee knazd kilobyte ukubwa ue Na moyo babakoo la sivyo wazungu waliokuwapo nahisi nilikuwa center ya tourism
 
Back
Top Bottom