Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

aiseee haya mambo ya ndege ni vema hata ku-google au kuchek kwenye YOUTUBE ili kujiridhika kabla mtu mzima hujaaibika ndegeni
 
Shukrani zimuendee PRINCE kwa kuwekeza kwenye FASTJET angalau na sisi tunakwea pipa kwa bei nafuu.
 
Hata kama utakuwa rubani huwezi kufikisha masaa laki moja

Wandugu Masanja....kuna pilot mmoja mkongwe sana alikuwa anaitwa Mazura huyu kafanya kazi muda mlefu sana toka miaka ya 60s enzi hizo kwenye mgodi wa Almas wa Williamson Diamnds Shinyanga...nae baadae miaka ya 80s kitu kama akaamia ATC.Kwa muda uliosemwa wa masaa yale yapatayo miaka 11...Kwa mtu kama Mzee Mazura yule anaweza kuwa nusu ya umri wake ameuendesha akiwa angani.Ndio kusema Mzee yule anaweza kuwa ametumia miaka 35 akiwa ni Pilot.Ni mmoja wa Mapilot wakongwe na wazuri sana Nchini Tanzania.

Kwa waliozaliwa Williamson ndege haikuwa kitu cha ushamba kwa walio wengi...manake siku nyingine mapilot mara kwa mara inasemekana walikuwa wanakusanya watoto mitaani na kwenda kuwapakia kwenye ndege na kuzunguka nao...maeneo kama Mwanza kisha kuwarudisha Willimson-Mwadui.
 
ungekuwa kikojozi ungekoma ubishi

Siziga hata Leo hii uki check inn counter pale Na ukapotea kwenye lounge ndege haiondoki!! Hadi wakupate! Maana upo close by Na confirmed unasafiri Na umesha book seat !! Ukiwa last counter!!!
 
Ndege ni kitu ambacho kwa kweli kila nikiwaza napata raha ya ajabu ikitokea ndo nasafiri na ndege yaani hata njaa sisikii kabisa, usingiz ndo sipati
 
mi naitamani sana KLM aisee mara nyingi huwa nalionaga pale KIA likitua na kupaa Nalitamani nilipande siku moja nikiwa naenda huko mbali sana sijui RUSSIA sijui wapi huko, yaani hapa najichanga tu nizushe trip ili mradi nikwee dude la KLM, wazungu wanafaidi sana aisee

Kama wale waliopanda ndege ya Malaysia,kama angetokea mmoja sidhani km ungetamani kupanda ndege tena;Japo utajipa moyo ILIKUWA NI AJALI,we acha kiherehere;mbona hata kupanda bus ni raha tu
 
Jamanii ata mimi sijawah naomba mnielekeze kuanzia airport nn kinatakiwa na kip haitakiwi mkanda unafungwaje namba za siti zimeandikwa wapi

Nenda kwenye maofisi ya mashirika ya ndege utajua taratibu;kwa ujumla maelekezo yote yanatoka ndani ya ndege ukipanda
 
Siziga hata Leo hii uki check inn counter pale Na ukapotea kwenye lounge ndege haiondoki!! Hadi wakupate! Maana upo close by Na confirmed unasafiri Na umesha book seat !! Ukiwa last counter!!!
Sio haiondoki. Utatafutwa kwa kutangaziwa kwenye spika mara 3. Usipoitikia/onekana wanaondoka.
 
Ilikuwa 2012 ndo kwa mara ya kwanza napanda ndege niko kwenye FASTJET ya kutoka MWANZA kuja DAR, nilikuwa na mihemuko balaa, niliiwazia hii safari kwa muda wa wk 2, nakumbuka nilipiga picha kila sehemu nilipopata Aiport, nje ya ndege na ndani ya ndege mpaka leo zipo nimezihifadhi kwa ajili ya wanangu, wajukuu na vitukuu.

View attachment 245577


Kali zaidi tulipokuwa hewani ndani ya NDEGE nikamwita mhudumu nimwulize wapi TOILET, akanionyesha, nikaenda japo sikuwa na haja yoyote nikaishia kutema mate kwenye sink la chooni , kuflash, nikanawa mikono, nikasukutua mdomo na kutoka zangu.

View attachment 245578

Tulipotua pale JKNIA asubuhi saa 09:40 akili ndo ikazidi kupagawa baada ya kuyaona yale MADEGE mengine makubwa makubwa yanapaa na kutua, nikaashangaa kama dakika 15 hivi na kutoka zangu nje, pale nje sasa madereva TAX full kushupalia, wapi kaka, twende na hii, bei poa tu, kwenda kuuliza bei toka pale mpaka TEGETA sh ngapi eti naambiwa elfu 35, nikajisemea moyoni shwaiiiiinnn sana, wakati nimetoka Mwanza mpaka Dar nauli elfu 32 tena kwa NDEGE halafu kutoka hapa mpaka TEGETA elfu 35, nikaachana nao na kwenda kupanda zangu daladala kwa nauli ya sh 950 ila nyumbani niliingia 13hr shauri ya foleni.

View attachment 245515

Daah umetisha sana aisee huna mchezo na pesa
 
KWELI IMETOKEA
Mshikaji mmoja alikuwa anamzimia sana Bob Nester marley. Mshkaji anajihusisha na uchimbaji wa madini alikuwa ameahidi hata kama hana kiwanja nyumba gari ila akipata tu mkwanja lazima a fly kwenda kuzuru kaburi la mzee mzima. Mungu akambariki mwaka juzi kavuta bingo msela kakwea pipa hadi jameca.

Nakutia moyo wewe mwenye ndoto za kukwea pipa yote yanawezekana usikate tamaa angali bado unapumua. Mungu kwanza na mengine yanawezekana.
 
usiombe ukutane na mwanafunzi/bitoz ndo siku ya kwanza kupanda ndege (fastjet), niliwahi kiupanda na toz mmoja na kidemu chake pale KIA ndo wamefunga shule wanarudi Dar, yaani jamaa earphone masikioni, huku kamkumbatia demu wake, picha kila dakika hadi kero
 
Hivi kwa nini Madereva taxi pale JNIA fastjet ikitua wala hawaangaiki kuwauliza abiria kama wanachukua taxi? jamani bure mbaya sana iaseee!
 
bado cjawahi kupanda pipa sijui itakuweje ngoja nifatilie ushamba ntapata somo kidogo,
 
Jambo sana ndugu zangu.Kuna mtu anae jua gharama za kusafiri kwa fast jet from Dar to mwanza.Msaada please,
 
Jambo sana ndugu zangu.Kuna mtu anae jua gharama za kusafiri kwa fast jet from Dar to mwanza.Msaada please, hasanten
 
Back
Top Bottom