hb Mujahideen
Senior Member
- Nov 23, 2019
- 152
- 164
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Demu bar akishakwambia ninunulie bia kimbia mbio.Demu mnunulie bia bila ye kuomba akikuomba jua hayo ni matapeli mdo kazi zaoUmaskini wa hali ya juu.
Ndio zangu unaweza sema huyu bwana karukwa na akili.Yaaah nakuwaga bubu[emoji23][emoji23][emoji23] ukijidai muungwana jiji hili la dar hawakuachi
Sent using Jamii Forums mobile app
Ni yule wa waterboard?Mwana jana kabananishwa uhamiaji alipojifanya yeye ni afisa takukuru..Alichokipata hatakaa akisahau..lakini kabla ya hapo sijui kapiga wangapi
Sent using Jamii Forums mobile app
Hahahaha huyo huyo.. Huyu hapA.. Kasababisha wana wamepigwa chiniNi yule wa waterboard?
Dah !!! Ila ww mshikaji nimecheka sn hii atory tamu we weka uzi wako watu wafurahUnauziwa nguo usiku, kesho ukirudi lile eneo wamepanga viazi
Niliwahi fanya ujinga huu kigoma ujiji, sijisifii lakini kila siku nimekuwa nikijutia kitendo nilichokifanya na nina imani hata huyo niliyemfanyia atakuwa amenisamehe.
Ilikuwa Kigoma, mpaka siku ya tukio nilikuwa nimeshakaa siku 21 nalala msikitini, mpango wangu ulikuwa kuvuka kuingia nchi jirani, lakini kutokana na mambo yalivyokuwa tofauti najikuta nagika kigoma nina shilingi hamsini tu, muda ulikuwa ni ule wa salat magharib, sipendi kuelezea sana ila nilikomaa mui huo ka hizo siku 21 mapanga na kupangua, cna ndugu zaidi ya Utanzania wangu, hiyo siku nakumbuka...nitaendelea
Ilikuwa ni jumanne ktk pitapita zangu nikaona tangazo la mganga wa kienyeji kubwa kwamba ndio kiboko huyo mama na anuani zake pale, nikafuata maelekezo mpaka ujiji nikaulizauliza nikaelekezwa nikafika, wakati mimi naingia kulikuwa kuna jamaa na wakezake wawili walikuwa ndani kwa huyo maman a muda huo ndio walikuwaw akiondoka, nikasubiri mpaka wametokomea ndipo nami nikabisha hodi na nikakaribishwa ndani, nikamsalimu yule bi mkubwa kisha nikatulia tuli sikusema shida yangu, yule bibi akaseti mitambo yake pale kisha akaanza yeye kunichana mimi matatizo yangu na tangu siku naamua kutokomea huko, yaani hakuacha kitu ikumbukwe mimi sikwenda huko kuinjoy maisha hapana, nilikuwa na targets zangu ambazo hatanikiamua kuzianika hapa mnaweza kunielewa tofauti ila kifupi ni ktk kupambana nitoboe ninakotaka kwenda..bibi akaongeaaaa sana na mwisho nikaona naniwekea usiku nikamuuliza kama tayari matatizo yangu yote ushayajua unanisaidiaje? Akasema yeye atanisaidia kwa elfu arobaini, Dah, nikasema huyu bibi mwehu nini? Ina maana kashindwa kujua kama hapa sina hata kumi? Nikamwambia fanya dawa ila moyoni nilishavurugwa kwa tabia ile ya kutaka pesa wakati mfukoni sina mia nyekundu, Yule mama alinyanyuka akaingia ndani kuongeza dawa huku nyuma mimi nikabeba simu yake Nokia ya tochi na kwenye ungo kulikuwa na shilingi elfu hamsini ambazo nahisi wale niliopishana nao ndio walizitoa, nikabeba kisha nikamuandikia ujumbe ktk kipande cha gazeni "nikifanikiwa nitarudi, ahsante kwa msaada wako" nikaondoka, nikavaa lemba langu (Kama wapalestina) nilikuwa na kijiti nikakiweka mdomoni kisha nikanuia ninavyojua huku natokomea kule chini ziwani....ni story ndefu ila mwisho wa siku yule bibi alikuja ziwani akinitafuta na akaja kuniuliza kijana hujamuona kijana flani anarangi hivi na nywele zake ndefu kazibana kwa nyuma? Ananiuliza mimi na mtu anayemuulizia ni Mimi...nikamwambia sijamuona mama huku natafuna kile kjiti na napiga dua zote mnazo zijua na msizo zijua ili yule aondoke niendelee na safari, karata ilikuwa upande wangu ile ibilisi nikaiepuka ila sasa mbele ya safari boti ( mtumbwi wenye engine mbili) ulizama jirani na hifadhi ya gombe....naomba niishie hapa kwa sababu nazojua mwenyewe
Sema mchizi hata ajateseka, kamwagiwa vimaji na kugaragara, kuna watu wanarud hawana meno, miguu imevunjikaMwana jana kabananishwa uhamiaji alipojifanya yeye ni afisa takukuru..Alichokipata hatakaa akisahau..lakini kabla ya hapo sijui kapiga wangapi
Sent using Jamii Forums mobile app
Chai !!! Mtu kaiba million 400 afu eti aninulie bia haiwezekan labda km hao mafund ni wendaazimu mm bila million 4 hapo cmwachii namchoma kwa mzee wa arusha tena namweka bond pesa io ioJamaa Auza Ghorofa Lisilolake Kkoo kwa Milioni 400Tsh.
Ilikuwaje?
Jamaa ni kutoka Manzese Sokoni, mti pesa.
Jamaa alikuwa kila siku jamani nauza ghorofa langu kariakoo...nauza ghorofa langu kkoo...ikawa kama wimbo.
Kumbe jamaa kajipanga kweli kuuza "ghorofa lake" kkoo...
Sasa kumbe kuna ghorofa moja kalilenga pale kkoo chini kuna garage. Ikawa anaenda pale garage na kusalimia na wakati mwingine anatoa offer kwa vijana wa garage...ya mihogo na soda...hali ikaendelea kwa miezi kama sita mpaka mafundi na saidia fund wote wakamzoea pale chini.
Mara akawa siku nyingine anapanda ghorofa, anapandisha ngazi mpaka juu sasa flow za chini hujui anaenda kwa nani kule juu na huwezi kumuuliza wakati ashakuwa alwatan pale...mara siku kaja na watu akapanda nao mpaka juu kbsaa flow ya tatu. Kumbe wale aliyekuja nao mmoja ni tajiri kalengwa toka Arusha aje apigwe Dar.
Kingi aliyoingizwa jamaa ni kuwa jamaa anataka kuuza ana kesi na anauzia kwa mwanasheria wake. Basi tajiri akaliona ghorofa...akalikagua mpaka akalidhika kisha wakaenda kwa mwanasheria wake ofisini. Malipo yakafanyika ofisini huku tajiri anapigwa na kiyoyozi hahaa...
Akatoka na document sake akaenda zake hotelini. Kesho asubui anaenda ghorofani kwake kuwapa notisi wapangaje wake wapya hahaaaa...hapo ndo jamaa akaishiwa nguvu. Akaambiwa mbona wenyewe wapo flow ya kwanza...jamaa akatoa document zake za mauziano...hola...akawai ofisini kwa mwanasheria hola...wala hawajulikani popote ila frame ilikodishwa miezi kama mitatu nyuma kwa misheni moja tu ya kuuza ghorofa kkoo...yule tajiri akawauliza mafundi garage kuwa mbona tulikuja naye hapa na mkapiga naye story sana. Wakamwambia huwa anakuja marakwamara na kutupa offer hapa hivyo tunamuitaga bosi.
Jamaa akapigwa kwa style hiyo.
Sasa alivyofanikisha hilo akarudi pale kijiweni akawaambia si niliwaambia nuaza ghorofa langu kkoo? Sasa nshauza anayekunywa anywe ebwana zilinyweka bia hapo si mchezo...asubui jamaa hakuonekana mpka leo.
Nb
Utapeli huu umetokea miaka kadhaa nyuma.
Mambo yasiwe mengi, mengi yasiwe mambo
Na waliomhenyesha nao kibarua kimepigwa stop.Mwana jana kabananishwa uhamiaji alipojifanya yeye ni afisa takukuru..Alichokipata hatakaa akisahau..lakini kabla ya hapo sijui kapiga wangapi
Sent using Jamii Forums mobile app
Ulikosea Sana binti,kwani mbona kuna maskini unawapa bure? Ulichonifanyia siyo kizuri ,subiri nitakupiga pigo kuu utafurahi na roho yakoNGOJA NIWAPE MKASA MMOJA
kuna boss wangu juzi nimemtapeli kazi aliyoniandikia pamoja na 50000 ya lodge.
Alikuwa ananitongoza nikakubali nikamwambia aniandalie document flani ambazo nilitakiwa nikaguliwe kazini kwa kuwa alijua atapata mzigo akaniandalia hizo document.
Siku ya kuzifata akaniambia yupo pale Madengo bar ya Dodoma wengi wanaifahamu. Basi nikaenda pale nikaagiza savvana kama mbili na Kitimoto rost nikazifukia nikala nikashiba.
Nikamwambia document zikwapi akasemaa hizi hapa kwenye bahasha nikazichukua nikaweka kwenye mkoba nikatulia.
Akasema tutafute lodge tukalale mm nikamwambia kwa sababu wewe ni mheshimiwa watu wakikuona itakuwa shida unatengeneza skendo nipe hela mm nikachukue chumba pale Simba hotel alafu nakupigia simu unakuja.
Akawa amenipa elfu 50000 ya chumba mm nikachukua pikpik ndruuuuki mpaka Geto kwangu.
Nilivyofik ninatumia sms usinitafute mm nipo nyumbani.
Hapa nilipo nawaza siku nikipata shida ya kikazi yeye ndiye boss wa hicho kitengo atanisaidia?
Maana alimpigia simu mpaka kiongozi wa ofisi yetu kumwambia jinsi mfanyakazi wake nilivyomtapeli.
Sahihi kabisa..ila jamaa hana pumzi kabisaaaSema mchizi hata ajateseka, kamwagiwa vimaji na kugaragara, kuna watu wanarud hawana meno, miguu imevunjika