mkumbwa junior
JF-Expert Member
- Oct 22, 2014
- 835
- 1,608
Umenielewa sasa[emoji16][emoji16][emoji23]Sasa msingeambiwa kilichotokea usiku uliopita mngeendelea kuamini ni uchawi na mngesambaza habari kwamba mmeshuhudua uchawi na story ingeendelea hivyo hivyo. Hivi ndivyo story zoooote za ushirikina zilivyo ni story za hearsay zisizomake any sense au zenye majibu thabiti kabisa ila watu hawataki kufikirisha akili kupata hayo majibu wanaamini tu kama nyumbu.
Traffic huwa wahawakamati vijana bodaboda na probox wa ujiji,na huwa hawaendi ujiji wanaishiaga maweni tu.maana ujiji wabembe ni balaa,lakini kigoma wachawi ni watongwe wa ilagala na watu wa njia za maji) kama wanavyoita hao huku mwamgongo kalya mpaka ufipa.ila waha sio wachawi nao wanaogopa sana watongwe,wabembe na warundi.Kigoma Visa vya Uchawi na Ushirikina.
Kigoma ni moja ya Mikoa ambayo inasifika kwa Uchawi nchini Tanzania. Huu mkoa kiasili una watu wachapa kazi sana. Si wazembe ukilinganisha na mikoa mingine yenye ushirikina kama Tanga,Pwani au Zanzibar.
Kigoma maeneo ambayo yanasifika sana kwa Uchawi ni Mwandiga, Ujiji,Mwamgongo n.k
Hapo Mwamgongo ni hatari sana karibu na Mbuga ya Gombe. Kunasifika na moja ya visa vya uchawi ni kimoja ambacho kilitokea mwaka 2020 ni kifo cha Diwani mmoja ambaye inasemekana alichukua Mke wa mtu.
Huyu Diwani ambaye allhamdulilah alikuwa na vijicent ilitokea akawa anatembea na mke wa raia mmoja kijijini hapo.
Yule bwana Raia alipata taarifa. Akanyamaza. Diwani akafikia hatua akaona aoe kabisa mke wa jamaa. Na mke akadai talaka ili akaolewe na Diwani.
Jamaa alimfuata Diwani na kumwambia kwa upole tu kuwa "Mheshimiwa najua unatembea na mke wangu, tafadhali usimwoe maana mimi ntapata shida kulea watoto hawa 6 nlio nao na nina mke mwingine. Uwe na uhusiano naye lakini usimuoe"
Diwani alijibu kwa jeuri tu kuwa "mkeo ndiye anayenilazimisha mzuie yeye siyo mimi"
Jamaa akamenda mpaka kwa viongozi wengine wa kijijini pale akitaka wakamsihi Diwani asimwoe mkewe. Diwani akakaza.
Mpaka jamaa akaenda kwa Rafiki mkubwa wa Diwani kumwomba amsihi rafiki yake asimwoe mkewe yeye atapata shida na watoto. Diwani akamtolea nje jamaa.
Basi jamaa akanyamaza. Siku moja Diwani akakutana na Jamaa Mitaa flani kuna Soko. Diwani akaanza mshambulia jamaa kwa maneno kuwa "nasikia unataka niroga..
Huniwezi,mimi mpaka kufika kuwa Diwani nmetoka mbali sana..." Akaendelea mbele na kumwambia haya nakupa mate na nyayo hii chukua." Akatema mate. Jamaa alimwambia tu Diwani "huo uchawi wa kuchukua mate na nyayo ni mdogo sana,wa watu ambao ni underdog/amateur"
Akaondoka zake. Baada ya siku chache tu Diwani akaanza kuumwa sukari ikapanda mara akaanguka ndo basi tena. Akafa.
Akazikwa. Baada ya siku chache wanafamilia yake wakawa wanamwona Diwani anakuja anagonga pale kwao kuwa afunguliwe mlango anateswa sana.
Diwani alikuwa amevaa pensi chafu.anagonga dirishani akisema anachapwa sana viboko. Afunguliwe.
Mke na watoto wakawa nao wanajawa woga.
Hili tukio lilitokea Mkoani Kigoma mwisho wa Reli.
Na watu wa Kigoma tofauti na Mikoa ya Pwani. Pwani mchawi wako mnaweza mkawa mnacheka naye na kula naye huku anakuroga.
Kigoma ukikorofishana na mtu anakwambia kabisa bila kuuma uma maneno "nitakuroga" hata hatumii sauti ya vitisho. Anakuambia kwa upole tu akikuahidi kuwa kweli atakuroga mbele za watu wengine.na anaenda kukuroga kweli.
Hiki ni moja ya kisa cha mambo ya Uchawi Kigoma.nitaleta Visa vingine vya Uchawi na Ushirikina Kigoma.
Kisa Cha Pili
Kuna jamaa mmoja alikuwa ana tatizo dogo tu na jirani yake shambani. Akawa anasema migomba flani ni ya kwake. yule mzee akamwambia hapana hili shina la Mgomba lipo shambani kwangu. Jamaa mbabe akasema ni lake na atakata.
Kweli ule mgomba mmoja ukazaa. Siku hiyo jamaa akaenda shambani akachonga chonga majani ili akate ndizi. Kunyanyua panga. Mkono ulipigwa ganzi haukushuka. Ukabaki juu na panga.
Akapiga kelele sana maana mkono ukawa kama unanyongwa hivi. Watu wakamchukua kumpeleka kwake. Mkono ulipooza.
Bro inaonekana ulikuwa mwamzi kwenye hili pambanoKuna yule alikuwa Mkuu wa Mkoa toka Sumbawanga ambaye amefariki miezi michache iliyopita,alipimana ubavu kichawi na wazee wa Ujiji ngoma ikawa droo wakaanza kuheshimiana
Huwezi kupewa kidono kama huna kinkuti.hizi dawa huenda sambamba lakini ni za wakongomani(wabembe)Wana uchawi wao unaitwa "Kidono"
Ni zindiko kali sana hilo, hata ukatwe mapanga, au risasi haiingii
Yaan mganga anachukua mwanawe, anamfanyia ilo zindiko
Kisha nakuambia wee umkatekate ..utakata weee lkn wapi
Sasa ndio ukiridhika anakufanyia wew
Ewaa kumbe kuna Kikunti?? Hiii imekaaje?Huwezi kupewa kidono kama huna kinkuti.hizi dawa huenda sambamba lakini ni za wakongomani(wabembe)
Hii you became more powerful unawezapiga kundi la watu.sasa ili uwe salama na hilo kundi ndio unachanjwa kidono ili utakaowazidi wasikuzuru kwa mapanga mshale au bunduki.hizi dawa huenda pamoja.Ewaa kumbe kuna Kikunti?? Hiii imekaaje?
Duuhh sawasawa, kuna jamaa liniambia kuna dawa moja,majambaz yakija kwenu. Yanaona Bahari tu au ziwa.Hii you became more powerful unawezapiga kundi la watu.sasa ili uwe salama na hilo kundi ndio unachanjwa kidono ili utakaowazidi wasikuzuru kwa mapanga mshale au bunduki.hizi dawa huenda pamoja.
Sister, usi underestimate nguvu ya "Pussy" aiseeMtu anaoaje mke wa watoto 6 huko si kuvunja familia aisee, useless diwani adhabu aliyopata alistahili
Itakuwa unapotosha kwa makusudu mazima au kwa kukosea ila Kama unaamini uchawi upo Basi unaweza kuwa na wasaa wa kuchunguza mikoa iliyo kwenye top ten ya wachawi inakaliwa na wenyeji wengi wa dini ipi hii itakusaidia na itatusaidia kwenye kuondoa upandikizi ulioukusudiaJamii yoyote iliyojaa waislam Hayo Mambo Ni kawaida
Hilo ni la kweli na kabla sijaivunja miiko yake ilishawahi kutokea wababe wakashindwa kunichana kwa kisu......majarbio ya hilo zindiko wanakufanyia wewe mwenyewe kwa kupigwa mapanga mwiliniWana uchawi wao unaitwa "Kidono"
Ni zindiko kali sana hilo, hata ukatwe mapanga, au risasi haiingii
Yaan mganga anachukua mwanawe, anamfanyia ilo zindiko
Kisha nakuambia wee umkatekate ..utakata weee lkn wapi
Sasa ndio ukiridhika anakufanyia wew
ππππTraffic huwa wahawakamati vijana bodaboda na probox wa ujiji,na huwa hawaendi ujiji wanaishiaga maweni tu.maana ujiji wabembe ni balaa,lakini kigoma wachawi ni watongwe wa ilagala na watu wa njia za maji) kama wanavyoita hao huku mwamgongo kalya mpaka ufipa.ila waha sio wachawi nao wanaogopa sana watongwe,wabembe na warundi.
Babati msumari wa batiππUkitoka kigoma katusimulie na visa vya uchawi Ugweno kwenye milima ya Upareni. Baada ya Upareni neda kwa Wairaq wao wanasema njoo Babati upigwe msumari wa bati.