Vita dhidi ya Corona: Mikusanyiko ya watu isiyo lazima isitishwe, misongamano idhibitiwe ili kuepusha madhara makubwa zaidi

Moja kwa moja kwenye mada, obvious siioni mantiki ya kufunga shule tu na kuacha vyuo, maana vyuoni pia kuna mkusanyiko mkubwa sana wa watu.. Na kama mambo za mabweni yapo kama kawaida..
Vyuo kama vya ualimu, kilimo, afya na kozi mbalimbali wanachuo wamelundikana vyuoni.

Ombi langu kwa serikali ni kwamba fungeni mpaka vyuo kwa huu mda wa mwezi mmoja hapo nitaona mantiki ya hili suala.
Ila kwa ujumla tu, tuendelee kumwomba ALLAH atuepushe na hili janga.
INSHAALLAH
 
I think the first step is to take precautions of or kids below 18.

Nyie wazee mna akili zenu bananeni huko wee kwenye mapantoni na madaladala ila mkirudi majumbani moja kwa moja kuoga na sabuni yenye sanitation.

Kwanza mmezeeka hata mkifa Taifa halina hasara sana...ha ha ha
 
Kwani kuhusu usafiri wa umma unatakaje? Serikali imnunulie kila mwananchi usafiri wake au?
 
Umeshau vivuko vya Ferry kigamboni!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
CCM imesitisha shughuli zote za chama ambazo zinahusisha mikusanyiko ya watu wengi.

Mh Polepole amewaomba viongozi wote wa dini kumuomba mwenyezi Mungu atuepushie balaa hilo.

Source ITV habari

My take; Chadema waige mfano wa CCM kwa kuweka siasa pembeni kwa sasa.

Maendeleo hayana vyama!
 
Vyuoni wapo watu wazima wanaojua hata matumizi ya kondomu wanajua namna ya kuishi kwa tahadhari.
Mkuu, huu ugonjwa hauna mtu mzima wala mtu mdogo.. Kwani muathirika was Corona unaweza kumjua kwa macho..?
Maana kuna watu wameambukizwa hyo corona na hawajijui..
That is serious issue, so serikali iliangalie hili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…