NAKWEDE,
Suala la kusitisha kabisa Misa zote za wiki na Jumapili, linapaswa kuangaliwa kwa umakini Mkubwa. Ni kweli, ukitumia Logic ya kawaida, katika kipindi hiki ambacho wataalam wa afya wanatuasa kuepuka mikusanyiko mikubwa, waweza sema, Misa kama sehemu ya Kusanyiko, nazo zatakiwa kusimamishwa. Lakin kumbuka, Wakati huu ambako watu Wana Wasiwasi/hofu/mashaka juu ya maisha yao, Ni Wakati ambao kama Kanisa lililo chanzo Cha Matumaini na Faraja kwa watu, linapaswa kukaa karibu zaidi na waamini na wote wenye uhitaji.
Na kwa kuwa huku kwetu, coverage ya Internet Ni ndogo, ndio kusema, Kanisa likianzisha program za Televised Masses, Ni waamini wachache watakaofikiwa na huduma hiyo. Wengi watabaki wapweke, bila tumaini mithili ya walivyokuwa Mitume wa Yesu mara baada ya Yesu kuuawa. Pia, wako waamini ambao Wakati huu wanahitaji huduma ya Kitubio kuliko Wakati mwingine, huduma ya Ushirika wa Bwana.
Hivyo, kama Kanisa likienda kichwa kichwa kuimpose baadhi ya Mambo, laweza kujikuta katika Wakati mgumu pindi maisha yatakavyorud kawaida, kwani Waamini wengi wanaweza kuachana na Kanisa kwa sababu Kanisa nalo liliwatelekeza Wakati walipokuwa wakilihitaji zaidi.