#COVID19 Vita dhidi ya COVID-19 Angola imetuumbua, Balozi awajibike?

#COVID19 Vita dhidi ya COVID-19 Angola imetuumbua, Balozi awajibike?

Mbona ata wachezaji wa nchi zilizoendelea wenye kila ujuzi wa kujikinga na Covid walishakutwa na Corona siku za nyuma,au aufatilii michezo?
Iweje kwa Tanzania uone tatizo ilhali ni janga la Dunia nzima?
Ni kweli na kuna wachezaji wanaondolewa hadi wapone, na kuna baashi ya mechi zinaahirishwa; kwa hiyo siyo jipya, Hoja iliyopo mezani ni kuwa Tanzania tunasema hakuna corona je hao waliogunduliwa kuwa na corona Angola waliipata wapi?- au kwenye ndege waliyosafiria!
 
Inawazekana wewe au nyinyi ni wafuata redio,hili suala kama hulijui ulizia ,na si Angola tu hata Namibia,sio kila sehemu tulioshoroki katika harakati za ukombozi wa nchi zao wanatupenda kihiiiiiiivyoh,la hapana Angola ,namibia zisikie hivyohivyo ,Mtanzania kule anaonekana adui,nasema Mtanzania kama Mtanzania niondolee cheo cha mpigania ukombozi wa nchi za kusini,tuko pamoja au hujaelewa,iangalie South Afrika ya leo ,je Mtanzania bado anaonekana ndugu ? Sana sana tumebakiza Msumbiji.Halafu kuwa mwanachama isikufanye ujione unapendwa au unapendaza kwa nchi wanachama,vipi Malawi ? kwani so marafiki lakini ukichimba utaona tunavyokodoleana macho.
Hivi kweli Watanzania ni wajinga kiasi hiki hata kusahau kuwa Rais wao mpendwa alitembelea moja ya nchi hizo wanachama wa SADC akapokelewa vizuri na kuondoka bila mkasa pamoja na Dreamliner yake mpaka yakampata yaliyompata Harare, Zimbabwe akiwa njiani kurudi. Wajinga humu JF wanamlaumu Balozi haijulikani wangetaka afanye nini kwani hayuko kule kubadili taratibu za nchi ile za kupokea wageni wakati huu wa Covid-19 ambapo kila nchi inayojali raia wake, inajitahidi kwa kila njia kulinda watu wake wasiambukizwe pneumonia. Pamoja na nchi yetu kutokuwa na gonjwa la Covid-19 na wachezaji walifukizwa kabla ya kuondoka lakini wanne waligundulika wana Virus na walipewa option waingie karantini au warudi walikotoka na gonjwa lao. CAF iliingilia kati ikafutilia mbali Mchezo kuwalinda Waangola!
 
Kwa nini Balozi hakuziambia mamlaka za Angola kuwa majibu yao si sahihi maana hatuna Corona? Je, wanne hao hawatuletei Corona
Achana na fitna za soka la Africa
Mbona marubani hawakupimwa?
Mbona wafanyakazi wa kwenye ndege hawakuguswa?
Usirukie Mambo Kama huyajui
 
Nemsoma komment zote , hi yakwako ni Ya kibwege kuliko zote
Unadhani huwa nakoment ili nimfurahishe mtu! Pole sana.
Watu hukoment ili kutoa maoni yao na c kufurahisha kama unavyofikiria, maoni yanaweza yakawa yanajenga au yanabomoa , ukitoa maoni yanayobomoa lažima uonekane ni kituko
Sasa maoni niliyotoa yana bomoa nini? Uliisikiliza au kuiangalia simulizi ya namna timu ya Namungo ilichofanyiwa na hao Waangola?

Nimeandika kwa hisia zangu kama Mtanzania. Sikufurahia kuona Watanzania wenzangu wanatengwa na kubaguliwa kama wanyama pori na Waafrika wenzao, kisa kikiwa ni Corona.

Sasa kutoa hisia na mawazo yangu, naona imegeuka kuwa kero kwenu. Nadhani tunatakiwa tuchukuliane wakati fulani tunapo jadili masuala ya Kitaifa. Ingekua ni ishu za kisiasa, simba na Yanga, ningekuelewa. Ila kwa hili, am very sorry. Nadhani niko sahihi kuliko unavyodhani.
 
Kipimo kinaendelea kufanya kazi. Watu wanapimwa maana ni kati ya requirements za kusafiri nje ya nchi. Tatizo ni kuwa majibu yanaelekea kama vile ni ya kupangwa ili kuonyesha kuwa hakuna huo ugomjwa Bongo!
MENGI yanaweza kuzungumzwa kuhusiana na kadhia hiyo, na wazungumzaji hawaachi kujipambanua na itikadi yake ya kisiasa. Lakini serikali ilishaweka utaratibu wa kupimwa Corona kwa wasafiri wote wanaokwenda nje ya nchi, na wanaobainika kukutwa na maambukizo hukataliwa kusafiri.

Nadhani ili kuukata mzizi wa fitna, tungevuta subira, angalau kwa wiki mbili, muda ambao unatosha kuwafuatilia wachezaji na viongozi wanaodaiwa kukutwa na maambukizo ya virusi vya kama watakuwa na corona, ili tuwe na uhakika wa yale tunayoyajadili, kwani endapo washukiwa hao wataonekana ni timamu kiafya hata baada ya muda huo, tutajua kwamba ni kweli walifanyiwa njama na figisu kwa malengo wanayoyajua wenyewe.

Hata hivyo Mamlaka ya Afya na serikaliilishatahadharisha kuwa kila mtu ana wajibu wa kujilinda, kuchukua tahadhari na kufuata kanuni zote za afya ili kujikinga na janga hili, huku tukimtanguliza MwenyeziMungu!

Lakini kuna baadhi ya watu, ama kwa kufuata mkumbo, kutumika kwa maslahi ya nje, kutojiamini, kushibishwa fikra potofu ama kwa sababu zote hizo, wanadhani uhai wa mtu ni mali ya serikali ama Chama fulani!

Haijakatazwa mtu binafsi, familia na ama ukoo kujifungia ndani ('lock down'), kwa muda wowote anavyoona inafaa kwake au kwao!, bila kuathirika.
Lakini kudhani kuwa suluhisho la changamoto zinazoikabili jamii haiwezi kupatikana kutokana na fikra, ubunifu na kwa kuzingatia mazingira yetu, ni dalili kuwa bado tunakubali kutawaliwa kifikra na tungali utumwani, tena utumwa mbaya kabisa na wakujitakia.

Matukio ya watu kufariki dunia yalikuwepo na yataendelea kuwepo, hata baada ya kupita kwa janga hili la sasa, kwani Imeandikwa 'Kila nafsi lazima itaonja umauti'.
 
Sijafurahishwa kabisa na unyanyasaji walio fanyiwa hao wachezaji na viongozi wa Namungo Fc. Ni vyema mamlaka zetu nazo zikajipanga ili kuja kulipa kisasi kwa kuwafanyia fitna za kutosha hao kenge iwapo watakuja Nchini mwetu kucheza mechi ya aina yoyote ile. Yaani waliwageuza Watanzania wenzetu kama mbwa vile!! Nimekasirika sana!!😟

Ila siungi mkono pia ishu ya serikali kupotezea uwepo wa huu ugonjwa. Ni bora hata kile kituo chao cha kupimia sampuli za huo ugonjwa kinge endelea kutumika hasa kwa wale Watanzania wote wanao safiri nje ya nchi ili kuondokana na aina hii ya manyanyaso kwa Watanzania.
Ukiwa na covid lazima unyanyapaliwe,kule sio Bong ni nchi ya watu wanajali afya za watu wao wewe endelea kupiga nyungu corona hakuna
 
Unadhani huwa nakoment ili nimfurahishe mtu! Pole sana.

Sasa maoni niliyotoa yana bomoa nini? Uliisikiliza au kuiangalia simulizi ya namna timu ya Namungo ilichofanyiwa na hao Waangola?

Nimeandika kwa hisia zangu kama Mtanzania. Sikufurahia kuona Watanzania wenzangu wanatengwa na kubaguliwa kama wanyama pori na Waafrika wenzao, kisa kikiwa ni Corona.

Sasa kutoa hisia na mawazo yangu, naona imegeuka kuwa kero kwenu. Nadhani tunatakiwa tuchukuliane wakati fulani tunapo jadili masuala ya Kitaifa. Ingekua ni ishu za kisiasa, simba na Yanga, ningekuelewa. Ila kwa hili, am very sorry. Nadhani niko sahihi kuliko unavyodhani.
Usibwabwaje hapa,wewe unaweza changanyikana na mgonjwa wa corona huku unaona anavyokohoa au hata kama hakohoi umeambiwa anao unaweza changamana nae?

Pili ukiambiwa na demu kwamba nina ngoma ila tutumie condom utalala nae? achilia mbali kuwa peku
 
Ndugu zangu tunazidi kuumbuka kuhusu janga la Corona.

Hadi niandikapo uzi huu, msimamo wa Serikali ya Rais Magufuli (si ya wananchi wa Tanzania) ni kwamba hakuna Covid-19 isipokuwa "changamoto ya upumuaji" hivyo basi ni dhambi ya mauti kutamka kuwa kuna "korona" Tanzania hata kama tunapukutika kama nzige wa jangwani waliopuliziwa dawa.

Vijana wetu wa Namungo FC waliondoka hapa nchini (kusiko na korono) kwenda kucheza nchini Angola (Champions Legue). Wamepimwa na kukutwa na ugonjwa huo ambapo ni wachezaji watatu na kiongozi mmoja wamekutwa na Corona. Mchezo wao umefutwa maana timu pinzani hawako tayari kurisk maisha yao. Wamehifadhiwa "jela".

Angola imeitangazia dunia kuwa Tanzania kuna Covid-19 mbele ya Balozi wetu nchini humo. Sasa wanne hao wanarejea nyumbani. Je, ndio wagonjwa wa kwanza hivyo tuwatenge na kuchunguza waliokutana nao kama yule mama wa Arusha mwaka Jana? Au watakapokanyaga ardhi tu ya Tanzania ugonjwa utakauka?

Kwa nini Balozi hakuziambia mamlaka za Angola kuwa majibu yao si sahihi maana hatuna Corona? Je, wanne hao hawatuletei Corona? Nawaza tu nikielekea kumzika Brigadier Mbena!
We pumbavu kweli ww hujui hizo ni hujuma za soka
 
Ni kweli na kuna wachezaji wanaondolewa hadi wapone, na kuna baashi ya mechi zinaahirishwa; kwa hiyo siyo jipya, Hoja iliyopo mezani ni kuwa Tanzania tunasema hakuna corona je hao waliogunduliwa kuwa na corona Angola waliipata wapi?- au kwenye ndege waliyosafiria!
Waliipata Kenya.
 
Corona IPO Duniani kote
Nashangaa mnapoteza muda kuijadili
Na hadi leo hakuna mchezaji hata mmoja duniani aliyekufa kwa Corona
 
Sijafurahishwa kabisa na unyanyasaji walio fanyiwa hao wachezaji na viongozi wa Namungo Fc. Ni vyema mamlaka zetu nazo zikajipanga ili kuja kulipa kisasi kwa kuwafanyia fitna za kutosha hao kenge iwapo watakuja Nchini mwetu kucheza mechi ya aina yoyote ile. Yaani waliwageuza Watanzania wenzetu kama mbwa vile!! Nimekasirika sana!!😟

Ila siungi mkono pia ishu ya serikali kupotezea uwepo wa huu ugonjwa. Ni bora hata kile kituo chao cha kupimia sampuli za huo ugonjwa kinge endelea kutumika hasa kwa wale Watanzania wote wanao safiri nje ya nchi ili kuondokana na aina hii ya manyanyaso kwa Watanzania.
Suruhisho si kulipa kisasi, suruhisho ni kufuata maagizo ya WHO kuhusu ugonjwa huu - kuna hatari michezo yetu yote ikafutwa tukabakia kama kisiwa.
 
KWA KITENDO HICHO PEKEE, TIMU YA NAMUNGO INAKWENDA KUPEWA USHINDI WA MCHEZO ULIOFUTWA.

WANAKWENDA HATUA YA MAKUNDI!
 
Ndugu zangu tunazidi kuumbuka kuhusu janga la Corona.

Hadi niandikapo uzi huu, msimamo wa Serikali ya Rais Magufuli (si ya wananchi wa Tanzania) ni kwamba hakuna Covid-19 isipokuwa "changamoto ya upumuaji" hivyo basi ni dhambi ya mauti kutamka kuwa kuna "korona" Tanzania hata kama tunapukutika kama nzige wa jangwani waliopuliziwa dawa.

Vijana wetu wa Namungo FC waliondoka hapa nchini (kusiko na korono) kwenda kucheza nchini Angola (Champions Legue). Wamepimwa na kukutwa na ugonjwa huo ambapo ni wachezaji watatu na kiongozi mmoja wamekutwa na Corona. Mchezo wao umefutwa maana timu pinzani hawako tayari kurisk maisha yao. Wamehifadhiwa "jela".

Angola imeitangazia dunia kuwa Tanzania kuna Covid-19 mbele ya Balozi wetu nchini humo. Sasa wanne hao wanarejea nyumbani. Je, ndio wagonjwa wa kwanza hivyo tuwatenge na kuchunguza waliokutana nao kama yule mama wa Arusha mwaka Jana? Au watakapokanyaga ardhi tu ya Tanzania ugonjwa utakauka?

Kwa nini Balozi hakuziambia mamlaka za Angola kuwa majibu yao si sahihi maana hatuna Corona? Je, wanne hao hawatuletei Corona? Nawaza tu nikielekea kumzika Brigadier Mbena!
Angola waliogopa kufungiwa nyumbani kwao wakatafuta kisababu cha kuwavunja moyo Namungo baada ya kuona Simba walivyoua huko Congo! Walianza kwa kuwaweka karanatini mara baada ya kutua kwenye ndege; halafu baada ya usumbufu wote huo, ndipo wakajifanya kupima na wala hakuna ushahidi unaoonyesha kuwa ripoti yao ni sahihi kwani tests hizo hazikufanywa na independent entity!
 
Ila kipimo kile ni kitengo cha serikali kutupiga
 
Namungo hachezi champions league, Timu nzima imerudi Tanzania na sio wale waliokutwa na Corona, Mchezo umefutwa lakini haina maana hawatakutana, Hakuna relationship yyte kati ya Balozi na Ugonjwa wa Corona ndani ya Namungo

Ile timu inaonyesha ni Jinsi gani baadhi ya Waafrika walivyo Malimbukeni. Tatizo lao hawakufuata utaratibu uliowekwa. Wamewa-treat Watu wa Namungo kama wanyama.
Nilikuwa South Africa, nchi inayoongoza kwa wagonjwa na vifo, lakini sikuwa nasikia vifo mara kwa mara kama hapa.

Kwa kuangalia taarifa za matukio ya vifo, kuna uwezekano mkubwa kwa sasa Tanzania kuwa imeathirika zaidi ya Afrika Kusini.
 
Back
Top Bottom