Vita vya Kagera 1979: Kwanini Jeshi letu lilipitia mipaka ya Sudan badala ya kukatiza hapo kati kufika Kampala?

Vita vya Kagera 1979: Kwanini Jeshi letu lilipitia mipaka ya Sudan badala ya kukatiza hapo kati kufika Kampala?

Walipotea wapi; si ajabu unasikia hadithi tu; ni kweli tulipoteza wanajeshi karibu 2000 (sina namba kamili) ambayo ni kama batallion moja, na nimekuambia kuwa katika hatua za kwanza za vita Kuna karibu Batallion nzima iliyopotea kwa sababu ya uamuzi mbovu wa kamanda mmoja.

Vile vile vita ya Lukaya iliua waganda na walibya wengi sana lakini pia watanzania walikufa. Sasa unaposema mimi nina utaahira (lugha za matusi zinazozuiwa hapa JF) sema ukweli wako. Mimi nilikuwa karibu sana na taarifa za mapambano yale kuanzia mwezi Octoba mwaka 1979 kabla hata Rais hajatangaza vita yenyewe kwa vile nilikuwa kwenye Brigedi ya Magharibi ambayo ndiyo iliingia vitani kwanza.

Vita iliendelea kwa miezi saba katika mazingira magumu kama niliyosema hapo, hivyo ni kweli watu walikufa. Huwezi kupigana vita ya ardhini bila askari wako kufa. Jeshi la Uganda halikuasi bali lilielemewa nguvu na jeshi la Tanzania licha ya kuwa walikuwa wanasaidiwa na askari wengi sana kutoka Libya.

Unaposema kuwa watu wetu walielemewa sana ila baada ya hapo jeshi la Uganda likaasi ndipo tukapata unafuu- ni wazi hujui vita nini- ile siyo ngoma ya mdundiko ndugu yangu, ni kazi ya kurushiana risasi za moto, sema pia ni askari wangapi wa Uganda waliokufa kama hutapatwa na ugonjwa wa moyo iwapo unaliangalia jeshi la Tanzania wakati huo katika negative lens;

Jeshi la Uganda lilikuwa kubwa sana, Amini alikuwa anawekeza sana katika jeshi kuliko sehemu nyingine yoyote, ila sasa JWTZ ilikuwa inawafuta kama sisimizi ndipo wakafikia kukata tamaa ya kuendelea na vita ile.
Mkuu 2000
Ni Battalion mbili hizo.

Na makadirio huenda tulipoteza Battalion 3
 
Sasa nakuuliza same question nimemuuliza jamaa yako hapo juu hadi amekimbia:

Unaweza ukanipa straight fact (sio porojo) kwamba kwa nini immediately after Kagera War uchumi wa TZ ulishuka mpaka negative 3% (rejea mahindi ya Yanga kutoka Marekani na mchele wa Thailand)

Unaweza kutaja sababu moja plain (usipige story) kwamba kwa nini Nyerere baada ya kuona vita inamshinda, aliamuru Migambo Wote wa mitaani wapelekwe frontline vitani kupigana vita... Wanajeshi walikua hawatoshi?
Mkuu Kunguni kwanza kabisa Pole na stress za corona,

Tangu inchi ipate uhuru ni miaka takribani 17 pekee ilikuwa imepita, ndio tukakutana na janga la vita nchii ilikuwa haijakomaa na sidhani hata kama ilikuwa na akiba hata ya asilimia 40% ya kifedha.
Vita inahitaji fedha,

Na nchi yetu haikuwa na uchumi ya vyema ilikuwa ni nchi changa.

Na kwa wakati huo mwalimu Julius Kambarage Nyerere alikuwa akihitaji watu wajitolee na ndio maana kuna watu walikuwa wanatoa ng'ombe, fedha, kusafirisha watu walio jitolea kwenda vitani, magari, na vitu vingine vingi.

Russia pia na Cuba zina mchango kwetu wakati wa hii vita,
Hivyo ilikuwa ni kweli uchumi ulishuka sababu tulitumia chakula kingi wakati wa vita na kama ujuvyo uzalishaji ulipungua,

sasa wewe kichwa maji unakuja hapa jukwaani kama kumtuhumu mwl, Utadhani yeye ndie aliesababisha hiyo vita.
 
Kiuhalisia ile vita haikuwa na Ulazima

Watanzania walikufa wengi sana kuliko Waganda.
Watoto wa 2000 wanapojaribu kuzaliwa 1960

Mdogo wangu vita haikuwa ya ulazima wakati Nduli Iddi Amini Dada alivamia Mkoa wa Kagera kwa madai ya kwamba ile ni sehemu ya uganda lazima aichukue.

Kwa hiyo mwl. JKN angewaachia..!?
 
Wanajeshi wengi wa Amini walitokea Sudan wakati huo Sudan ni moja walikuwa wanubi pia kabila lake la kakwa lilikuwa karibu na Sudan mpakani inawezekana base yao ilikuwa huko

Kuhusu uchumi kushuka hivi unaelewa kwanini Marekani baada ya vita huwa anaingia mikataba ama ya kuchukua mafuta au vitu vingine kulipia gharama? Vita yoyote ina gharama na sisi baada ya vita Uganda alitakiwa kutulipa sijui malipo yalifikia wapi ila kuna kipindi museveni aliomba yasamehewe
 
Mkuu 2000
Ni Battalion mbili hizo.

Na makadirio huenda tulipoteza Battalion 3
Ni kweli inawezekana sana kwani sina mahesabu kamili haraka haraka kichwani, ila wakati ule batalian moja ilikuwa na kombania saba pamoja na hedikwota COY, na kila kombania ilikuwa na platuni tatu pamoja na ile ya hedikwota zote kwa pamoja zikiwa na kama askari kama 120 mpaka 130 hivi-sitaki kwenda kwa kina zaidi juu ya Organization ya wakati huo. Sasa ukipiga hseabu hiyo mara saba kwenye Battalion moja ni kama askari 910 ambao ukijumulisha na na HQ COY unapata kamaaskari kama 1260. Ila sasa Batallion za kivita wakati huo zilikuwa ni kubwa zaidi ya orgaization hiyo kwa sababu ya Mgambo, magereza, JKT na Polis waliunganishwa katika Batallions hizo.

Jamaa wa Wikipedia wanatoa namba za vifo kama ifuatavyo kwa hiyo hawakufika 2000 wala Batallion moja ya kawaida. Ila majeruhi walikuwa wengi zaidi.

1591578125998.png
 
Unaweza ukanipa straight fact (sio porojo) kwamba kwa nini immediately after Kagera War uchumi wa TZ ulishuka mpaka negative 3% (rejea mahindi ya Yanga kutoka Marekani na mchele wa Thailand)

Unaweza kutaja sababu moja plain (usipige story) kwamba kwa nini Nyerere baada ya kuona vita inamshinda, aliamuru Migambo Wote wa mitaani wapelekwe frontline vitani kupigana vita... Wanajeshi walikua hawatoshi?

Ahsante. 1979 ulikua una umri gani kaka?
Pumba kabisa wewe kwani kumbe unaongea mambo usiyoyajua bali ya kuhadithiwa tu. Hata hujui kuwa mahindi ya Yanga yalikuja kutoka wapi halafu unakuja hapa kupiga kelele.

Kwa vile mimi ni mwalimu nitakufundisha ifuatavyo. Mahindi ya Yanga yaliingia Tanzania mwaka 1975 kutokana na ukame uliokuwa umeikumba nchi mwaka 1973 na 1974 ikiwa ni muda mfupi sana baada ya opereshini vijiji ambayo ilivuruga kilimo cha asili na kuacha watu hawana chakula; na ulikuwa ni msaada ulioidhinishwa na Rais Jimmy Carter wa Marekani kupitia USAID.

Ule mchele wa Jasmine kutoka Thailand haukutolewa msaada kwa ajili ya vita, bali ulianza kuagizwa kuingia nchini wakati wa utawala wa rais Mwinyi na wafanya biashara binafsi baada ya Liberalization; hiyo ni pamoja na mafuta yakupikia ya OKI kutoka Singapore, ambayo ilikuwa ni kwa sababu za kibiashara kushindana sokoni tu. Kama unazungumza unga wa Yanga baada ya vita ni kuwa hukuwepo na wala hujui hali halisi ya wakati ule, kwani tuliokula unga ule mpaka mwaka 1977 hatusemi vile.

Vita iliaza mwaka 1978 wakati nchi haina unga wa yanga tena. Kwa upande wa pili; ni kweli kuwa uchumi wa nchi ulivurugika sana kwa sababu Tanzania ililazimika kununua silaha kali za kupambana na Amin kwa muda mfupi ambazo hazikuwa kwenye bajeti ya nchi; na ikatumia hela za kukopa zinazokaribia bajeti ya miaka miwili au mitatu hivi ya nchi ili kupata mitambo ya Balllistic misiles (BM40) mingi kuliko uwezo wake wakati ule kwa sababu amini alikuwa ameuza migodi yote ya Shaba kwa Urusi kusudi apatiwe vifaru vingi; na alikuwa na vifaru vingi sana ambavyo jeshi letu lilivivunjavuvunja kama chungu ambacho hakikupita kwenye tanuru. Kitu ambacho Tanzania tunashukuru tena kwnye vita ile ni kuwa baada ya vita kuanza, Urusi nayo ikaivamia Afghanstani kipindi hicho hicho na hivyo ikawa iko bize kupambana na Mujahedeen, ikaacha kupelea vifaru kwa Uganda tena.
 
Bila shaka unafahamu umri wangu!
Hata kama sijui umri wako; ni wazi kuwa hukuwapo duniani hapa kabla ya mwaka 1986 wakati ambapo mchele wa Jasmin kutoka Thailand unaanza kuingia nchini. Kwa hiyo wakati vita inaaza mwaka 1978 ulikuwa bado unaishi sehemu fulani ya kufikirika tu, ndiyo maana unatoa maneno ya kufikirika tu.
 
Kiuhalisia ile vita haikuwa na Ulazima

Watanzania walikufa wengi sana kuliko Waganda.

Yaani jirani yako akija nyumbani kwako na kumbaka mke wako mbele yako utasema hakuna haja ya kumpigania mke wako? Nachukulia kama wewe ni mtoto wa kiume. Iwapo vita ile haikuwa na ulazima, basi hatuna haja ya kuwa na JWTZ tena
 
Hata kama sijui umri wako; ni wazi kuwa hukuwapo duniani hapa kabla ya mwaka 1986 wakati ambapo mchele wa Jasmin kutoka Thailand unaanza kuingia nchini. Kwa hiyo wakati vita inaaza mwaka 1979 ulikuwa bado unaishi sehemu fulani ya kufikirika tu, ndiyo maana unatoa maneno ya kufikirika tu.

Kumbe unakubaliana na maelezo yangu kuwa mchele wa Tailendi umeanza kuingia Bongo baada ya vita ya Uganda.

Halafu, weka jazba pembeni. Kuweka record ni kuwa IDD Amin alivamia mpakani mwa Uganda na TZ (akaingia maeneo ya Kagera)

Unakubali kuwa vita haikua na ulazima?

Kwamba ilikua inatosha kumwondoa adui mpakani arudi kwake, tubaki tukilinda mipaka yetu.

Kulikua na haja gani kwenda mpaka Kampala hadi Sudani huko na kuyaacha majeshi yakilinda usalama huku yakiendelea kutumia rasilimali za Tanzania?

Kwanini baada ya kumkimbiza Amini pale Kagera wasingerudi na kubaki kulinda mipaka tu na kuwaacha Waganda wapambane na uongozi wao?
 
Sasa mkuu wangemuacha Idd Amin kisa washamtoa Kagera si angejipanga akarudi tena?

Kumbe unakubaliana na maelezo yangu kuwa mchele wa Tailendi umeanza kuingia Bongo baada ya vita ya Uganda.

Halafu, weka jazba pembeni. Kuweka record ni kuwa IDD Amin alivamia mpakani mwa Uganda na TZ (akaingia maeneo ya Kagera)

Unakubali kuwa vita haikua na ulazima?

Kwamba ilikua inatosha kumwondoa adui mpakani arudi kwake, tubaki tukilinda mipaka yetu.

Kulikua na haja gani kwenda mpaka Kampala hadi Sudani huko na kuyaacha majeshi yakilinda usalama huku yakiendelea kutumia rasilimali za Tanzania?

Kwanini baada ya kumkimbiza Amini pale Kagera wasingerudi na kubaki kulinda mipaka tu na kuwaacha Waganda wapambane na uongozi wao?
 
Ni kweli inawezekana sana kwani sina mahesabu kamili haraka haraka kichwani, ila wakati ule batalian moja ilikuwa na kombania saba pamoja na hedikwota COY, na kila kombania ilikuwa na platuni tatu pamoja na ile ya hedikwota zote kwa pamoja zikiwa na kama askari kama 120 mpaka 130 hivi-sitaki kwenda kwa kina zaidi juu ya Organization ya wakati huo. Sasa ukipiga hseabu hiyo mara saba kwenye Battalion moja ni kama askari 910 ambao ukijumulisha na na HQ COY unapata kamaaskari kama 1260. Ila sasa Batallion za kivita wakati huo zilikuwa ni kubwa zaidi ya orgaization hiyo kwa sababu ya Mgambo, magereza, JKT na Polis waliunganishwa katika Batallions hizo.
Mzee wangu alishriki hii vita na alikuwa askari polisi
 
Kwa taarifa yako majeshi ya Uganda yalikuwa vizuri sana kabla ya uasi.
Vita ilipoanza tulipoteza wanajeshi wengi mno japo taarifa zilifichwa, binamu yangu amepigana na amesimulia mengi mno ambayo serikali haikuweka na haitaweka wazi.

Hivyo unaposema kwani tulizunguka, unafikiri hao jamaa walikuwa dhaifu kiasi hicho?
Vita ina mbinu nyingi, moja wapo ni kumzunguka adui wakati yeye anapambana na wale waliom face...ghafla snashangaa anashambuliwa eneo ambslo hskutegemea.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwataarifa yako mkuu, bado Uganda iko njema kivifaa vya vita
 
Ina semekana kuwa bila mgawanyiko wa majeshi ya Uganda basi jamaa wangetuchapa ile mbaya...tuwashukuru sana akina mseveni
Hii ni mentality ya kutokujiamini tu, kudhani kuwa sisi ni inferior kwa kila kitu. Vile vile ni kutokuelewa historia halisi

Elewa kuwa jeshi la Uganda wakati huo lilikuwa chini ya Amini, siyo kuwa Jeshi lilikuwa limegawanyika. Chanzo kikubwa cha kuelekea Amin kumpindua Obote ni kwa vile alikuwa anasuka jeshi kuwa lake na kuwa ana-sideline wasiokuwa wafuasi wake kwa kutumia hela za serikali, na Obote alipomtaka aeleze matumizi ya hela za jeshi ndipo akaamua kumpindua. Ni kikundi kidogo kilichokuwa kimebaki upande wa Obote ambacho ndicho kilikimbilia Tanzania kikiongozwa na akina Oyite Ojok na Tito Okello ambacho kiliitegemea sana Tanzania kwa miaka yote minane ya utawala wa Amini; kilikuwa hakifiki hata batallion moja. Baada ya kuangushwa kwa Amini na jeshi lote la Uganda kuvunjwa na TPDF, ndipo UPDF ilipoanzishwa na kufundishwa na TPDF, unaweza kuona hata jina lenyewe. Mvutano wa madaraka uliotokea ndani ya Uganda baada ya Amini kuwa amsheaangushwa na jeshi letu kuwa limesharudi nyumbani ndio uliosababisha Museveni aanzishe jeshi lake la msituni NRA ikiwa ni mwaka 1983. Museveni mwenyewe alipandikizwa kutokea Tanzania; wengine ni kama Dani Wadada Nabudere ambaye alikuwa anafundisha UDSM kabla ya vita.

Hata kama unaidharau Tanzania, kubali kuwa TPDF ilikuwa jeshi imara sana wakati huo. Kumbuka lilikuwa limeshapitia mapigano mabalimbali kusini mwa Afrika kwa hivyo lilikuwa na experience kubwa sana kuliko jeshi lolote Afrika ya Mashariki.
 
Nilikuwa katika mazingira ya jeshi la akiba wakati huo, na siyo kweli kuwa Jeshi la Uganda lilikuwa liko vizuri sana kuliko la Tanzania. Wale askari wetu waliokufa wengi kwa kipindi kimoja ni wale waliotumwa na Brigadia Yousufu Himid ambaye wakati huo ndiye aliyekuwa Brigade Commander wa Brigedi ya Magharibi kabla ya kuondolewa (kwa kosa hilo) na nafasi yake kukaimiwa na Kanali Kotta - baba yake na Faraja Kotta.

Brigedia huyo aliituma battalion kadhaa zivuke mto kwa mitumbwi kuingia hilo enelo llililokuwa limetekwa baada ya daraja kuvunjwa. Kwa vile upande ule uliokuwa umetekwa ni high tactical ground ndiyo maana askari wa Tanzania waligundulika na kuuwawa kwa vile walikuwa wanajiandaa kuvuka na bunduki tu, bila ya kuwa na silaha kubwa. Askari wetu wa kwanza kuingia Uganda kukomboa ile sehemu iliyokuwa imetekwa na kusaidia ujenzi wa daraja la muda walipitia Rwanda.

Ni vivyo hivyo pia kwa kupitia Rwanda ilikuwa ni rahisi wao kuingia ndani zaidi ya uganda kwa upande wa Magharibi, hivyo hata mashambulizi makubwa ya kuingia Kampala yalitokea huko Magharibi, na ni kweli askari wetu wengine walishafika mbali karibu na Sudan kabla ya kuja kushambulia Uganda. Kikosi Kikikubwa cha Idi Amini ni kile kilichokuwa kinaitwa Simba Batallion kilichokuwa na makazi yake pale Masaka ambacho baadaye kilikuja kusaidiwa na askari wa Libya wakati wa yale mapambano ya Lukaya.

Kikosi kile cha Simba Batallion kilizingirwa pia na majeshi ya Tanzania kutokea Magharibi kikiongoizwa na Brigadier Imran Kombe na Major General Marwa, ndipo Amini alipotuma wale askari wa Libya waje kusaidia na kufanya mapambano ya Lukaya kuwa makali sana lakini mwishowe Simba Batallion na askari wa Libya wakasalimu Amri na kuiacha Baracks ya Masaka mikononi mwa Imran Kombe. Ukishaondoa hiyo Simba batallion na Askari wa Libya, sehemu kubwa ya jeshi la Amin lilikuwa ni "maharage ya Mbeya tu"
Mambo haya mazuri sana Unaweza kukubali tukufanyie Mahojiano Tuandike kitabu??
 
Back
Top Bottom