Vita vya Kagera 1979: Kwanini Jeshi letu lilipitia mipaka ya Sudan badala ya kukatiza hapo kati kufika Kampala?

Vita vya Kagera 1979: Kwanini Jeshi letu lilipitia mipaka ya Sudan badala ya kukatiza hapo kati kufika Kampala?

Sawaa lkn kuna kitabu kimoja kinasema Jeshi letu mpk 1978 kilikuwa na askari wasiozidii 20000 au 30000 lkn ndani ya miezi 6 hivi askari waliongezeka mpk 100000 au 150000....hapa tunajumuisha mgambo, askari polisi, uhamiaji, TISS na wengneo....

Kuhusu iyoo idadi (379) kuna makaburi Bunazi kyaka na Kaboya......


Nataman kujuaa waliokufa wengine walizikwa wapii au walitelekezwa uwanja wa vita, achana na wale waliogeuzwa chakula cha Mamba Kagera ambao tunaaambiwa walikuwa platoon 3 mpk 6 zilizomiminiwa Mizinga na Askari wa amini wakitaka kuvuka mpaka kuingia Uganda kwa mitumbwiii

Sent using Jamii Forums mobile app
Naona kama wewe unaquestion uwezo wa jeshi la Tanzania wakati huo, na unaelekea kuamini tu kuwa JWTZ walikuwa ni wanyonge. Leo hii sijui muundo wa JWTZ, lakini wakati wa Nyerere JWTZ ilikuwa ni pamoja na JTK, Polisi, Magereza, na Mgambo kama majeshi ya akiba. Kulikuwa na sera ya kuwa jukumu ulinzi wa taifa letu ni raia wote na kila askari katika eneo lolote alikuwa ni mlinzi wa taifa. Hicho kitabu ulichosoma inawezekana kilikuwa kinaripoti namba za wale active soldiers wa TPDF na kusahau kuwa TPDF ilikuwa na reserve soldiesr wengi sana; baada ya vita kuanza wale reserve soldiers wote walikuwa activated na jeshi kuonekana kubwa sana. Katika yote ya Nyerere nadhani sifa yake kubwa ni ile ya kujenga mioyo ya uzalendo kwa wananchi.
 
Hii ni mentality ya kutokujiamini tu, kudhani kuwa sisi ni inferior kwa kila kitu. Vile vile ni kutokuelewa historia halisi

Elewa kuwa jeshi la Uganda wakati huo lilikuwa chini ya Amini, siyo kuwa Jeshi lilikuwa limegawanyika. Chanzo kikubwa cha kuelekea Amin kumpindua Obote ni kwa vile alikuwa anasuka jeshi kuwa lake na kuwa ana-sideline wasiokuwa wafuasi wake kwa kutumia hela za serikali, na Obote alipomtaka aeleze matumizi ya hela za jeshi ndipo akaamua kumpindua. Ni kikundi kidogo kilichokuwa kimebaki upande wa Obote ambacho ndicho kilikimbilia Tanzania kikiongozwa na akina Oyite Ojok na Tito Okello ambacho kiliitegemea sana Tanzania kwa miaka yote minane ya utawala wa Amini; kilikuwa hakifiki hata batallion moja. Baada ya kuangushwa kwa Amini na jeshi lote la Uganda kuvunjwa na TPDF, ndipo UPDF ilipoanzishwa na kufundishwa na TPDF, unaweza kuona hata jina lenyewe. Mvutano wa madaraka uliotokea ndani ya Uganda baada ya Amini kuwa amsheaangushwa na jeshi letu kuwa limesharudi nyumbani ndio uliosababisha Museveni aanzishe jeshi lake la msituni NRA ikiwa ni mwaka 1983. Museveni mwenyewe alipandikizwa kutokea Tanzania; wengine ni kama Dani Wadada Nabudere ambaye alikuwa anafundisha UDSM kabla ya vita.

Hata kama unaidharau Tanzania, kubali kuwa TPDF ilikuwa jeshi imara sana wakati huo. Kumbuka lilikuwa limeshapitia mapigano mabalimbali kusini mwa Afrika kwa hivyo lilikuwa na experience kubwa sana kuliko jeshi lolote Afrika ya Mashariki.
Mkuu Kichuguu vijana wa siku hizi hawataki kujifunza historia ya nchi yao
 
Mkuu hapa sasa nimekuelewa baada ya Uganda kuingia madarakani aliua mapadri wengi na akiwemo huyu Kiwanukaa

Sent using Jamii Forums mobile app


Idd Amin hakuwa mdini , ila Kanisa Katoliki lilikuwa likijiingiza kwenye siasa kama linavyofanya kwenye nchi nyingi duniani ikiwemo Tanzania. Labda kwa kuona malengo yao hayatotimia kwa urahisi
 
Ila wahaya ni wakuwaonea huruma sana, Ukimwi ulipoingia uliwafyeka sana wao na Vita ya Kagera iliwamaliza sana.... haiyumkini leo hii hili ndio lingekuwa kabila kubwa na lenye nguvu nchini hasa kwa idadi ya watu.... pia Mji wa Bukoba ungekuwa Jiji pengine.... Mungu awape nguvu wahaya na makabila yote wazawa wa Bukoba
 
Mmmmmhhhhh, ukatoliki unakujaje tena kwenye hiyo vita?


Ukumbuke Kabla Idd Amin hata hakuwa na fikra za kuivamia TZ isipokuwa kwa vile wapinzani wa Amin walikuwa wakifanya vitendo vya kigaidi ndani ya Uganda kutokea Tanzania . Mwisho Amin akaona ni bora avamie aichukuwe Kagera iwe ni kama buffer zone yake kuzuia vitendo hivi vya kigaidi.
 
Ni kweli, kuna watu wengi walikufa ila hawawezi kufikia askari 5000 kwa sababu jeshi letu lilikuwa na brigedi tano tu kwa hiyo askari 5000 ingekuwa ni karibu robo tatu ya brigedi nzima. Kumbuka ni vita ambayo tulivamiwa kwa hiyo kuna raia wetu wengi waliokufa baada ya uvamizi kabla vita haijaaza. Namba za Nyerere zinaweza kuwasahihi zaidi kwa vile zinahusu askari wa jeshi ambao walikuwa na namba za kijeshi na zinaweza kuwa hazihusishi askari wa akiba kama mgambo na JKT.
Yapo mengi yanapotoshwa kuhusiana na hii vita. Angalau wewe unatupa mwanga halisi na taswira kamili juu ya kilichotokea. Endelea kutushushia madini kama hutojari mzee wetu achana na huyu poyoyo anayekupinga bila kuweka hadidu za rejea
 
Walipotea wapi; si ajabu unasikia hadithi tu; ni kweli tulipoteza wanajeshi karibu 2000 ambayo ni kama batallion moja, na nimekuambia kuwa katika hatua za kwanza za vita Kuna karibu Batallion nzima iliyoptea kwa sababu ya uamuzi mbovu wa kamanda mmoja.

Vile vile vita ya Lukaya iliua waganda na walibya wengi sana lakini pia watanzania walikufa. Mimi nilikuwa karibu sana na taarifa za mapambano yale kuanzia mwezi Octoba mwaka 1979 kabla hata Rais hajatangaza vita yenyewe kwa vile nilikuwa kwenye Brigedi ya Magharibi ambayo ndiyo iliingia vitani kwanza. Vita iliendelea kwa miezi saba katika mazingira magumu kama niliyosema hapo, hivyo ni kweli watu walikufa. Huwezi kupigana vita ya ardhini bila askari wako kufa.

Jeshi la Uganda halikuasi bali lilielemewa nguvu na jeshi la Tanzania licha ya kuwa walikuwa wanasaidiwa na askari wengi sana kutoka Libya. Unaposema kuwa watu wetu walielemewa sana ila baada ya hapo jeshi la Uganda likaasi ndipo tukapata unafuu- ni wazi hujui vita nini- ile siyo ngoma ya mdundiko ndugu yangu, ni kazi ya kurushiana risasi za moto-, sema pia ni askari wangapi wa Uganda waliokufa kama hutapatwa na ugonjwa wa moyo iwapo unaliangalia jeshi la Tanzania wakati huo katika negative lens; Jeshi la Uganda lilikuwa kubwa sana, Amini alikuwa anawekeza sana katika jeshi kuliko sehemu nyingine yoyote, ila sasa JWTZ ilikuwa inawafuta kama sisimizi ndipo wakafikia kukata tamaa ya kuendelea na vita ile.
Ukitaka kujua unajadili na nani itisha ile hidden profile yake. Au muulize umri wake utapoteza muda na wanafunzi wanaosubiri tangazo la Covid 19 kuisha.
 
Unaweza ukanipa straight fact (sio porojo) kwamba kwa nini immediately after Kagera War uchumi wa TZ ulishuka mpaka negative 3% (rejea mahindi ya Yanga kutoka Marekani na mchele wa Thailand)

Unaweza kutaja sababu moja plain (usipige story) kwamba kwa nini Nyerere baada ya kuona vita inamshinda, aliamuru Migambo Wote wa mitaani wapelekwe frontline vitani kupigana vita... Wanajeshi walikua hawatoshi?

Ahsante. 1979 ulikua una umri gani kaka?
Ndugu mimi ni layman kwenye maswala ya kijeshi, lakini kwa mtazamo wa kawaida unajua hatuna kiwanda cha silaha na zote zinatoka nje, unadhani zilikua zinanunuliwa nini, unadhani tons ngapi za risasi zilikua zinatumika kwa siku, mabomu mangapi kwa siku, dawa kiasi gani kwa siku kutibu majeruhi, mafuta kiasi gani kubeba maaskari na vifaa, kwa kufirikia just even as a layman unaweza kuona kiasi gani cha fedha kilikua kinaenda kwa siku na nchi ilikua na just 18years umepata Uhuru.

Lazima uchumi utetereke, kama Marekani inatetereka, how about Tanzania? Vita si biashara the loss is always greater hata ukishinda. Ndio maana Sun Tzu akasema the greatest military strategist is the one who can win the war (diplomatically) before the fi bullet is fired. Kuhusu kupelekwa mgambo, nadhani hii ni obvious huwezi kuchukua all your professional and experienced soldiers ukawapeleka frontline. Anything can happen kule, kuna commanding errors na mambo mengine yanaweza kutokea. So lazima wawepo wa ku-train new recruits na pia wa kwenda nao front ili wazoee Vita. Si mpaka uwe mwanajeshi au ufanye kazi wizara hiyo kujua haya. Just a common sense
 
Waliosoma na kuhadithiwa vita ya Kagera wanaonekana wanajua sana kuliko waliopigana vita yenyewe soon natia neno
Ni kweli kwa sababu sisi tulio_iishi hiyo vita tupo kimya.

nakumbuka miaka hiyo wakati vita imepamba moto.

Mimi nilitokaga BELENGE sita sahau.

kipindi hicho VIAZI vilikuwa bado havijaanza kuitwa CHIPS
 
Watu 2000 walikuwa % ngapi ya watanzania? Je leo hawa 2000 wangekuwa wamezalisha watu wangapi? Population yetu leo ingekuwa inasoma watu 65 milion
 
Hapo nimekuelewa.
Hii ni mentality ya kutokujiamini tu, kudhani kuwa sisi ni inferior kwa kila kitu. Vile vile ni kutokuelewa historia halisi

Elewa kuwa jeshi la Uganda wakati huo lilikuwa chini ya Amini, siyo kuwa Jeshi lilikuwa limegawanyika. Chanzo kikubwa cha kuelekea Amin kumpindua Obote ni kwa vile alikuwa anasuka jeshi kuwa lake na kuwa ana-sideline wasiokuwa wafuasi wake kwa kutumia hela za serikali, na Obote alipomtaka aeleze matumizi ya hela za jeshi ndipo akaamua kumpindua.

Ni kikundi kidogo kilichokuwa kimebaki upande wa Obote ambacho ndicho kilikimbilia Tanzania kikiongozwa na akina Oyite Ojok na Tito Okello ambacho kiliitegemea sana Tanzania kwa miaka yote minane ya utawala wa Amini; kilikuwa hakifiki hata batallion moja. Baada ya kuangushwa kwa Amini na jeshi lote la Uganda kuvunjwa na TPDF, ndipo UPDF ilipoanzishwa na kufundishwa na TPDF, unaweza kuona hata jina lenyewe.

Mvutano wa madaraka uliotokea ndani ya Uganda baada ya Amini kuwa amsheaangushwa na jeshi letu kuwa limesharudi nyumbani ndio uliosababisha Museveni aanzishe jeshi lake la msituni NRA ikiwa ni mwaka 1983. Museveni mwenyewe alipandikizwa kutokea Tanzania; wengine ni kama Dani Wadada Nabudere ambaye alikuwa anafundisha UDSM kabla ya vita.

Hata kama unaidharau Tanzania, kubali kuwa TPDF ilikuwa jeshi imara sana wakati huo. Kumbuka lilikuwa limeshapitia mapigano mabalimbali kusini mwa Afrika kwa hivyo lilikuwa na experience kubwa sana kuliko jeshi lolote Afrika ya Mashariki.
 
Tactician mkubwa wa JWTZ alikuwa ni Kanali Kitete (Siyo Lupogo) kabla hajawa Brigadier. Jamaa yule anajua kupanga vita siyo mchezo, sijui kama bado JWTZ leo hii ina tacticians kama yeye. Jamaa alichambua kuwa Amini alikuwa ameweka ulinzi mkubwa sana directly kwenye mpaka wa Tanzania (backed by heavily Mechanized Simba Batallion), ila hakuwa na ulinzi kule Magharibi kwa nsababu alikuwa na uhusiano mzuri sana na Mobutu wakati huo (mpaka leo Kampala kuna mtaa una jina la Mobutu liliowekwa na Amini). Kamanda akachambua ramani na kuweka mkakati uliomfuta Amin kwenye ramani kwa kutokea Magharibi ya Uganda.



Kwenye video hii hapa chini huwa napenda sana kile kipande kuanzia 1:04 hadi 1:34 kinachoonyesha makamanda wetu shujaa.

 
Ni kwa sababu alipofukuzwa Amin akawa kiongozi ni Yusuf Lule mwislamu lakini Nyerere kuona huyu siye anayemtaka akaleta mizengwe ya kumrudisha Mkatoliki mwenzake Obote ambaye waganda walikuwa hawamtaki.

Gazeti la Reporter la Kenya la tarehe 20/6/1963 lilitangaza katika ukurasa wake wa mbele: "KUIBADILI AFRIKA YA MASHARIKI KUWA KATIKA DINI YA ROMANI CATHOLIC". Ndani ya gazeti hilo ukurasa wa 18 liliwataja waliopewa dhamana ya kufanikisha jambo hilo kuwa ni: Uganda - Kiwanuka, Kenya - Mboya na Tanganyika Mheshimiwa Nyerere.
Uongo huo;

Kwanza elewa kuwa Professor Lule aliwekwa pale na Nyerere akiamini kuwa atawaunganisha waganda. Failure kubwa ya Professor Lure (hakuwa na PhD) ni pale aliposhindwa kujiweka katika maisha ya waganda na kushindwa kutuliza matakwa ya upkeeping cost ya cabinet yake. Hapo ndipo alipotofautiana na Nyerere mpaka mwisho
 
Si maoni yangu tu hata wewe unayo haki ya kunisahihisha kama si kweli
Kuna sababu za wazi na nyingine ni za siri. Mimi sina ushahidi wa hili ya Nyerere kuingiza nchi kwenye vita kisa ukatoliki wake. Ndio maana nimeita "maoni" maana sijui kama una ushahidi wowote wa hayo unayoyasema
 
Back
Top Bottom