Vita vya Kagera 1979: Kwanini Jeshi letu lilipitia mipaka ya Sudan badala ya kukatiza hapo kati kufika Kampala?

Mkuu 2000
Ni Battalion mbili hizo.

Na makadirio huenda tulipoteza Battalion 3
Mkuu hizii ni battalion 4, bro wangu alikuwepo uwa nashangaa Nyerere kipindi anawapokea wanajeshi waliorudi alisema "tumepoteza vijana wetu 379" na Mkapa kwenye mbook wake karudia kosa hili kwa makusudi. Tulipoteza askari zaidi ya 5000, na raia zaidi ya 2500 miezi mitatu ya kwanza ya vita baada ya kutekwa kwa eneo la Kakunyu, Kabwobya na Minziro wanajeshi wetu walivofka Mutukula walilipa kisasi cha staili ile ya kyaka (ya raia na wanajeshi waliokufa) yaan "Masacre" au "mfekane" kwa hiyo Mutukula kuna raia zaidi ya 3000 waliuliwa (na Watanzania wakiwemo) yaan dah hii vitaa kuna mengi tunafichwa huyu jamaa ameamua kuwa muwazii lakini nae hajasema ukwelii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkapa alifatiliaa hili deni katika utawala wake tukalipwa kidogo baadae ikabidi wasamehewee

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Ni kweli, kuna watu wengi walikufa ila hawawezi kufikia askari 5000 kwa sababu jeshi letu lilikuwa na brigedi tano tu kabla hazijaongezwa wakati vita ikiendelea, kwa hiyo askari 5000 ingekuwa ni karibu robo tatu ya brigedi nzima.

Kumbuka ni vita ambayo tulivamiwa kwa hiyo kuna raia wetu wengi waliokufa baada ya uvamizi kabla vita haijaaza.

Namba za Nyerere zinaweza kuwasahihi zaidi kwa vile zinahusu askari wa jeshi ambao walikuwa na namba za kijeshi na zinaweza kuwa hazihusishi askari wa akiba kama mgambo na JKT.
 
Mkapa alifatiliaa hili deni katika utawala wake tukalipwa kidogo baadae ikabidi wasamehewee

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwanini wasamehewe huu ndio ujinga wetu kwani tulipoteza rasilimali watu na pesa zetu na hii vita ni miongoni mwa vitu vilivyoturudisha nyuma kitaifa mfano kiwanda cha sukari kiliharibiwa leo hii tunanunua sukari Uganda
 
Tunachukua umeme utokao Uganda unatumika Kagera kwa fidia ya vita
 
Isitoshe wanajeshi wengi wa Iddi Amini hawakuwa waganda akiwepo Malyamungu. Wengi walitoka Sudan na Zaire sasa wakati wa kichapo wengi wakawa wanakimbilia kule kuji-regroup ikabidi tupande nao
 
Kwani babako alishawahi kukuambia jinsi alivyokuwa anacopy majibu darasani, alivyokuwa kilaza wa hesabu? Ni mfano tu, kwanini tuyaandike na kuyaanika mabaya yetu? Kwa manufaa gani? Muulize mmarekani anapotezaga wanajeshi wangapi katika vita zake
 

Mzee wetu wewe ni shujaa...na tunashukuru kuja kutupa historia nzuri ya Taifa letu, Vijana wengi hatujui wapi tulipotoka. Shukrani mzee achana na hawa Mbu tasa wanaokejeli na kupinga pasipo maana
 
Sawaa lkn kuna kitabu kimoja kinasema Jeshi letu mpk 1978 kilikuwa na askari wasiozidii 20000 au 30000 lkn ndani ya miezi 6 hivi askari waliongezeka mpk 100000 au 150000....hapa tunajumuisha mgambo, askari polisi, uhamiaji, TISS na wengneo....

Kuhusu iyoo idadi (379) kuna makaburi Bunazi kyaka na Kaboya......


Nataman kujuaa waliokufa wengine walizikwa wapii au walitelekezwa uwanja wa vita, achana na wale waliogeuzwa chakula cha Mamba Kagera ambao tunaaambiwa walikuwa platoon 3 mpk 6 zilizomiminiwa Mizinga na Askari wa amini wakitaka kuvuka mpaka kuingia Uganda kwa mitumbwiii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mmmmmhhhhh, ukatoliki unakujaje tena kwenye hiyo vita?

Ni kwa sababu alipofukuzwa Amin akawa kiongozi ni Yusuf Lule mwislamu lakini Nyerere kuona huyu siye anayemtaka akaleta mizengwe ya kumrudisha Mkatoliki mwenzake Obote ambaye waganda walikuwa hawamtaki.

Gazeti la Reporter la Kenya la tarehe 20/6/1963 lilitangaza katika ukurasa wake wa mbele: "KUIBADILI AFRIKA YA MASHARIKI KUWA KATIKA DINI YA ROMANI CATHOLIC". Ndani ya gazeti hilo ukurasa wa 18 liliwataja waliopewa dhamana ya kufanikisha jambo hilo kuwa ni: Uganda - Kiwanuka, Kenya - Mboya na Tanganyika Mheshimiwa Nyerere.
 
Mkuu hapa sasa nimekuelewa baada ya Uganda kuingia madarakani aliua mapadri wengi na akiwemo huyu Kiwanukaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Mzee wetu, nasikia kuwa kwenye hiyo miaka kabla ya Vita uchumi wetu wa Tanzania ulikuwa juu kuliko hata Kenya, ila baada ya vita ndo uchumi wetu ukapitwa na kenya hadi leo, je kuna ukweli hapo mkuu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…