Vita vya Kagera 1979: Kwanini Jeshi letu lilipitia mipaka ya Sudan badala ya kukatiza hapo kati kufika Kampala?

Vita vya Kagera 1979: Kwanini Jeshi letu lilipitia mipaka ya Sudan badala ya kukatiza hapo kati kufika Kampala?

Hizi illusion za kidini huwa mnazitoa wapi ninyi wafia dini?.

Kwahiyo ule upuuzi wa majeshi ya uganda chini ya idi amini kuvamia Tz na kuua raia na kutaka kuchukua sehemu ya tz ilipaswa achekewe si ndio.

Kweli hakuna mtu mjinga kama mfia dini...no wonder mnajiripua kwa illusion.

#MaendeleoHayanaChama

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Historia iliyofichwa sana...
Amini aliamua kuivamia Tanzania baada ya Tanzania kuandaa wahasi dhidi ya utawala wa IDD Amin...Historia inafichwa kwa misingi hipi sijui?!
 
Historia iliyofichwa sana...
Amini aliamua kuivamia Tanzania baada ya Tanzania kuandaa wahasi dhidi ya utawala wa IDD Amin...Historia inafichwa kwa misingi hipi sijui?!
Na ndio maana dunia ilikaa kimyaa kumsikiliza tu.
 
Soma vizuri historia ya Vita ya Kagera.
Majeshi yetu katu hayakuingia Sudan, ila baada ya kuteka yalifika mpaka Arua, kijijini kwa Idi Amin.
Nilichelewa kuona hii post yako. Huu uzi kifupi mzee wangu Kichuguu alishautendea haki muda mrefu. Alimaliza kila kitu. Hamna haja ya kusoma historia wakati watu waliokuwepo kwenye vita wanatueleza kila kitu.
 
Soma vizuri historia ya Vita ya Kagera.
Majeshi yetu katu hayakuingia Sudan, ila baada ya kuteka yalifika mpaka Arua, kijijini kwa Idi Amin.
Nilichelewa kuona hii post yako. Huu uzi kifupi mzee wangu Kichuguu alishautendea haki muda mrefu. Alimaliza kila kitu. Hamna haja ya kusoma historia wakati watu waliokuwepo kwenye vita wanatueleza kila kitu.
 
Uswahiba wa Nyerere na Obotte ndio source ya vita hiyo.
Wazee fulani walienda mbali zaidi na kudai kuwa vita baridi ilichangia pakubwa.
Baada ya west kuona Mwalimu anaelekea Kwa Lenin, waka spin vita ili uchumi wa Tz uporomoke
 
Mimi hii hata sitachangia sababu sijui chochote nlisoma kwenye historia na kuimba akwenye mchakamchaka. 79 ndo mwaka wangu wa kuzaliwa
 
Hawakukatiza mkuu, ni kwamba majeshi ya Tanzania yalitembeza kichapo kwa Idd Amin, wakaingia hadi kaskazini na magharibi mwa nchi ya Uganda, wakafika kwenye mipaka ya Uganda na Zaire(DRC), mipaka ya Uganda na Sudan. Mji wa Arua uliopo kaskazini mwa Uganda ndio kipo kijiji cha Koboko, kijiji alichozaliwa Idd Amin Dada.

Waliingia huko wakiwa na mzuka wa mapambano. Amin akasalimu amri, akakimbia Uganda na kuacha majeshi ya Tanzania (Wakombozi) yakiikamata Uganda.
vita vya Kagera) na Uganda kama Vita vya Ukombozi vya 1979, [a] vilipiganwa kati ya Uganda na Tanzania kuanzia Oktoba 1978 hadi Juni 1979 na kupelekea kupinduliwa kwa Rais wa Uganda Idi Amin. vita hivyo vilitanguliwa na kuzorota kwa mahusiano kati ya Uganda na Tanzania kufuatia Amin mwaka 1971 kumpindua Rais Milton Obote aliyekuwa karibu na Rais wa Tanzania, Julius Nyerere. kwa miaka iliyofuata, utawala wa Amin uliyumbishwa na vurugu, matatizo ya kiuchumi, na kutoridhika katika Jeshi la Uganda.

Hali zinazozunguka kuzuka kwa vita haziko wazi, na akaunti tofauti za matukio zipo. Oktoba 1978, majeshi ya Uganda yalianza kuivamia Tanzania. Baadaye mwezi huo, Jeshi la Uganda lilianzisha uvamizi, kupora mali na kuua raia. Vyombo vya habari rasmi vya Uganda vilitangaza kunyakuliwa kwa Kagera Salient. Mnamo tarehe 2 Novemba, Nyerere alitangaza vita dhidi ya Uganda na kuhamasisha Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kuchukua tena nguvu. Nyerere pia aliwahamasisha waasi wa Uganda waliokuwa watiifu kwa Obote na Yoweri Museveni ili kuudhoofisha utawala wa Amin. baada ya Amin kushindwa kukana madai yake kwa Kagera na Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU) kushindwa kulaani uvamizi wa Uganda, TPDF iliikalia kwa mabavu miji ya Masaka na Mbarara kusini mwa Uganda.

wakati TPDF ikijiandaa kusafisha njia kuelekea Kampala, mji mkuu wa Uganda, Muammar Gaddafi, kiongozi wa Libya na mshirika wa Amin, alituma wanajeshi elfu kadhaa nchini Uganda kusaidia Jeshi la Uganda. Shirika la Ukombozi wa Palestina pia lilituma idadi ya wapiganaji wa msituni kumsaidia Amin. mwezi Machi vita kubwa zaidi ya vita hivyo vilitokea wakati Watanzania na waasi wa Uganda waliposhinda kikosi cha pamoja cha Uganda-Libya-Palestina huko Lukaya. Kupotea kwa Lukaya kulipelekea Jeshi la Uganda kuanza kuanguka. nyerere aliamini kuwa waasi wa Uganda walipaswa kupewa muda wa kupanga serikali yao ili kumrithi Amin. Alifadhili kongamano la waasi na watu waliohamishwa mjini Moshi baadaye mwezi huo, ambapo Uganda National Liberation Front (UNLF) ilianzishwa. libya ilimaliza uingiliaji kati wake mapema mwezi wa Aprili na wanajeshi wake waliikimbia nchi. Tarehe 10 Aprili kikosi cha pamoja cha TPDF-UNLF kilishambulia Kampala, na kuulinda siku iliyofuata. Amin alikimbilia uhamishoni huku serikali ya UNLF ikianzishwa. katika miezi iliyofuata, TPDF iliikalia Uganda, ikikabiliwa na upinzani uliotawanyika tu. Ililinda mpaka wa Uganda na Sudan mwezi Juni, na hivyo kumaliza vita.

Vita hivyo viliathiri vibaya uchumi wa Tanzania na kusababisha uharibifu wa muda mrefu kwa Kagera. pia ilikuwa na madhara makubwa ya kiuchumi nchini Uganda, na kuleta wimbi la uhalifu na vurugu za kisiasa huku serikali ya UNLF ikijitahidi kudumisha utulivu. mizozo ya kisiasa na kuendelea kwa mabaki ya Jeshi la Uganda katika maeneo ya mpakani hatimaye kulisababisha kuzuka kwa Vita vya Bush vya Uganda mwaka 1980
 
Back
Top Bottom