Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) inapanga kuchangisha $1bn (£759m) katika muda wa wiki moja kusaidia uzalishaji wa kilimo barani Afrika na kulinda bara la Afrika kutokana na uhaba wa chakula unaotokana na uvamizi unaoendelea wa Urusi nchini Ukraine.
Nchi nyingi za Kiafrika zinategemea mataifa hayo mawili yanayopigana kwa usambazaji wao wa nafaka.
Somalia, Benin, Misri na Sudan zinaongoza kwenye orodha ya nchi ambazo zinategemea pakubwa Urusi na Ukraine, huku zaidi ya 70% ya ngano yao ikitoka katika mataifa hayo mawili.
“AfDB inaona ongezeko hili la bei ya ngano, mahindi na maharagwe ya soya kama uwezekano wa kuzidisha uhaba wa chakula na kuongeza mfumuko wa bei,” Rais wa AfDB Akinwumi Adesina alisema.
Mkopeshaji huyo wa kimataifa anasema ataitisha mkutano wa mawaziri wa fedha na kilimo barani Afrika ili kutekeleza mpango huo.
Kupitia mfuko huo, AfDB inalenga kuongeza uzalishaji wa mpunga wa ngano, mahindi na soya kwa kutumia teknolojia zinazostahimili hali ya hewa, zikiwemo aina za mazao zinazostahimili joto na ukame.
Aina ya ngano inayostahimili joto tayari imejaribiwa nchini Sudan na Ethiopia.
Kulingana na Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Biashara na Maendeleo (UNCTAD), angalau mataifa 25 ya Afŕika yanaagiza zaidi ya thuluthi moja ya ngano yao kutoka Russia na Ukrainia.
Kwa hakika, kwa 15 kati yao, sehemu hiyo ni zaidi ya nusu ya matumizi yao ya kila mwaka ya ngano ambayo yanatoka katika mataifa hayo mawili yanayopigana.
BBC Swahili
Nchi nyingi za Kiafrika zinategemea mataifa hayo mawili yanayopigana kwa usambazaji wao wa nafaka.
Somalia, Benin, Misri na Sudan zinaongoza kwenye orodha ya nchi ambazo zinategemea pakubwa Urusi na Ukraine, huku zaidi ya 70% ya ngano yao ikitoka katika mataifa hayo mawili.
“AfDB inaona ongezeko hili la bei ya ngano, mahindi na maharagwe ya soya kama uwezekano wa kuzidisha uhaba wa chakula na kuongeza mfumuko wa bei,” Rais wa AfDB Akinwumi Adesina alisema.
Mkopeshaji huyo wa kimataifa anasema ataitisha mkutano wa mawaziri wa fedha na kilimo barani Afrika ili kutekeleza mpango huo.
Kupitia mfuko huo, AfDB inalenga kuongeza uzalishaji wa mpunga wa ngano, mahindi na soya kwa kutumia teknolojia zinazostahimili hali ya hewa, zikiwemo aina za mazao zinazostahimili joto na ukame.
Aina ya ngano inayostahimili joto tayari imejaribiwa nchini Sudan na Ethiopia.
Kulingana na Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Biashara na Maendeleo (UNCTAD), angalau mataifa 25 ya Afŕika yanaagiza zaidi ya thuluthi moja ya ngano yao kutoka Russia na Ukrainia.
Kwa hakika, kwa 15 kati yao, sehemu hiyo ni zaidi ya nusu ya matumizi yao ya kila mwaka ya ngano ambayo yanatoka katika mataifa hayo mawili yanayopigana.
BBC Swahili