Vita ya Corona: Nahodha wetu katelekeza chombo Baharini, tutaponaje?

Vita ya Corona: Nahodha wetu katelekeza chombo Baharini, tutaponaje?

Gellangi

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2016
Posts
2,782
Reaction score
3,018
Hapa naandika kwa majonzi kwa kusikia jinsi Watanzania wenzetu wanavyougua Corona na wengine kupoteza maisha. Poleni nyote.

Kinachoumiza zaidi ni namna baadhi yetu tunavyoteteana hata kunapokuwa na uzembe kwenye hatua zinazochukuliwa kutulinda na Corona.

Kuna wanaosema Nahodha wetu ni shujaa, mwenye uthubutu na tupo salama ilhali abiria tunaona hatari iliyopo mbele yetu.

Nahodha wetu tunaambiwa yupo mapumzikoni. Je, tukisema kajitosa baharini na kutuachia chombo kielee kwenda kuzama tunakosea?

Corona bila lockdown itatumaliza, ilikuwa Arusha, Dar na Zanzibar hatukuona haja ya lockdown eti tutakufa njaa. Sasa tuna wagonjwa mikoani na hakuna kinachoonekana kufanyika, hatujaamua bado kulock maeneo yenye wagonjwa.

Tunafahamu kuwa hakuna dawa, chanjo, vifaa tiba, maabara za uchunguzi na vifaa vya kujikinga hasa kwa watoa huduma za afya.

Tuamini kuwa tupo salama? Tuamini kuwa Nahodha hajajitosa na kuacha chombo katikati ya mawimbi makali?
 
Gellangi,
Upuuzi mwingine bhana. Alafu kesho mtu kama wewe atakuja bishana na mtu kuwa oooh, urais ni taasisi.

Hivi waziri mkuu ambaye alikabidhiwa rasmi hii ishu tena laivu hatukuona? Akaunda timu yake ya kuongoza juu ya hii ishu. Au ishu ni jamaa aoneoane tu ktk tv.? Dah!
 
Upuuzi mwingine bhana. Alafu kesho mtu kama wewe atakuja bishana na mtu kuwa oooh, urais ni taasisi.
hivi waziri mkuu ambaye alikabidhiwa rasmi hii ishu tena laivu hatukuona? Akaunda timu yake ya kuongoza juu ya hii ishu. Au ishu ni jamaa aoneoane tu ktk tv.? Dah!
East Africa nchi gani inayoingoza kwa maambukizi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Upuuzi mwingine bhana. Alafu kesho mtu kama wewe atakuja bishana na mtu kuwa oooh, urais ni taasisi.
hivi waziri mkuu ambaye alikabidhiwa rasmi hii ishu tena laivu hatukuona? Akaunda timu yake ya kuongoza juu ya hii ishu. Au ishu ni jamaa aoneoane tu ktk tv.? Dah!

Nyie mifano yenu si mnatoa kwa Trump? Haya Trump kila siku yuko on air akitolea ufafanuzi janga kwa wamarekani.
 
Mimi simfananishi na nahodha wa chombo mimi namfananisha na dereva wa bajaji ambae ameona simba mbele yake ameachia usukani na kukimbilia siti ya nyuma huku yaani amekimbia majukumu yake
Ajabu ni kuwa bado kuna miongoni mwa abiria wanaamini na wanataka wenzao waamini kuwa Nahodha yupo sawa kujitosa kwa muda huu tunapomhitaji sana,na wanataka tuamini kwamba tupo salama maana Nahodha atarudi chomboni muda wowote atakaoona unafaa.

Tuendelee kumwita Nahodha wa chombo kwa sababu ni mkubwa sana hawezi kuwa dereva wa Bajaji.

Karibuni mchangie mada-Nahodha kajitosa Chombo chaenda mrama,tupo salama?
 
Unamtetea Nahodha wa Chombo chetu?Wewe pia ni abiria?Sijaelwa unataka kusemaje hasa?
 
Basi tuseme ni dereva wa Bajaji aliyepewa chombo dhoruba imemfanya akikimbie chombo na kwenda kujificha jikoni
Haonekani hats jikoni,yumkini kawaachia wengine wahangaike na mawimbi,kukitulia kidogo anachungulia na kutoa maagizo halafu anajitosa tena.
Simwelewi huyu Nahodha kwa nini alikubali kazi hiyo kama hana ujasiri wa kukabili mawimbi?
 
Haonekani hats jikoni,yumkini kawaachia wengine wahangaike na mawimbi,kukitulia kidogo anachungulia na kutoa maagizo halafu anajitosa tena.
Simwelewi huyu Nahodha kwa nini alikubali kazi hiyo kama hana ujasiri wa kukabili mawimbi?
Cha ajabu yeye kakimbia usukani halafu anawaambia abiria wasali siku tatu mfululizo ili chombo kisizame
 
Ndugu kwenye nchi hii yameshawahi kuundwa matimu mangapi na yameleta matokeo gani
Upuuzi mwingine bhana. Alafu kesho mtu kama wewe atakuja bishana na mtu kuwa oooh, urais ni taasisi.
hivi waziri mkuu ambaye alikabidhiwa rasmi hii ishu tena laivu hatukuona? Akaunda timu yake ya kuongoza juu ya hii ishu. Au ishu ni jamaa aoneoane tu ktk tv.? Dah!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haonekani hats jikoni,yumkini kawaachia wengine wahangaike na mawimbi,kukitulia kidogo anachungulia na kutoa maagizo halafu anajitosa tena.
Simwelewi huyu Nahodha kwa nini alikubali kazi hiyo kama hana ujasiri wa kukabili mawimbi?
Labda atakuwa nahodha hewa,aliwahi kusema nchi hii kila kitu ni hewa,so usishangae nae akawa hewa
 
Back
Top Bottom