Hii vita ya kagera kama isingefanyika na mfumo wa kijamaa kama usingekuwepo na Watanzania tukajipanga vizuri TZ tusingekuwa hapa,tungekuwa tumepiga hatua sana
we jamaa umetuchukuliaje kwa hii comment?.Mkuu shida ni kwamba inapotokea mvutano wa pande mbili mara nyingi hua propaganda zinatawala kwa kila mtu kuvutia upande wake.
Ila ukiwa na msimamo wa kati na kati inakua ni rahisi kuelewa zaidi.
Mkuu mimi ni mtanzania na ni mzalendo.
Tatizo linapotokea hua nnasimama na nchi yangu kwa hali yoyote na hata hili la vita ya kagera ningekua frontline kumng'oa Iddi Amini kwa hali yoyote.
Ila linapokuja suala la propaganda hua nnajilazimisha kukaa katikati ili kufahamu mambo kwa undani wake zaidi.
Siku Hans pope anapigwa risasi, wanajeshi wa Uganda waliopo mpakani walipotelea Tanzania, sisi tumeaminishwa(propaganda) wanajeshi wale walikua wamelewa chakari kutokana pombe hawakujielewa wakavuka boder na kuingia Tanzania.
Na wale wanajeshi waliompiga risasi Hans Pope walikua wamevuka mpaka na vifaru viwili kuja kuwakomboa wenzao waliokua wamelewa chakari na kupotelea ndani ya mipaka yetu.
Kwa mazingira kama hayo ukiwa makini ukaacha kuendeshwa na propaganda utajua kulikua na nini behind the scene.
nyumbani kwetu kulikuwa na duka la ujamaa yaani kupata chumvi hadi balozi ajue
Nani kakuambia Kagera ilikuwa inataka kuchukuliwa....mkuu kuna ishu nyingi sana zimejificha nyuma ya ile vita....wala sio kuchukuliwa kwa kagera kama tunavyoaminishwaga.
hizi record umepata wapi kuwa jwtz walikimbia records zangu zote zinaonyesha hii ilikuwa battle fup ya siku 2 toka 10 march to 11 march na jwtz walishinda.Mkuu, hii ni scenario tofauti na yetu japo umesimulia ukweli, Jamaa yupo sahihi hatuja recover mpaka leo kwa vita ile kwa sababu deni hili mara ya mwisho nilifuatilia hatukulipa lote liishe hivo tulikuwa tunadaiwa na pia Uganda tulikuwa tunaidai pesa ndefu sana
fuatilia battle of Lukaya kwa wanajeshi wa JWTZ, hii ndio ilikuwa battle ngumu kuliko zote pale UG, JWTZ ilihelemewa na kupewa kichapo askari walikimbia,hivo hii vita ililicost mno taifa
Ebu wekeni mambo wazi jamani,mbona mnatupa kidogokidogo?.Hasira ya Waisrael dhidi ya Iddi Amini ilikua ni mwaka mmoja au miwili nyuma kabla ya vita ya kagera, baada ya kutekwa kwa ndege iliyokua na waisrael na kuwashikilia mateka katika uwanja wa Antebe.
Baada ya Waisrael kutuma makomando wao kuja kuwakomboa mateka kuna bibi mmoja wa kiyahudi hakukombolewa alikua mahututi alipelekwa hospital,
Hasira za Iddi Amini baada ya nchi yake kuvamiwa na wanajeshi wake kuuliwa na makomandoo wa Israel kwa hasira akaamua kumuua yule bibi.
Israel ikaingia nyongo na utawala wa Amin nchini uganda kwa mambo makuu matatu
1)Amini kuwasupport magaidi dhidi ya utekaji wa raia wa kiyahudi
2)Amini kutoa hifadhi kwa magaidi kuwashikilia mateka
3)Amini kumuua yule bibi wa kiyahudi
Hizo pesa kwa zama hizo zingeelekezwa kwenye huduma za kijamii, kilimo tungesogea sana mbele.