Vita ya Starlink na Safaricom ni somo kwa kampuni za mawasiliano Tanzania

Vita ya Starlink na Safaricom ni somo kwa kampuni za mawasiliano Tanzania

Wewe ni mpotoshaji. God will punish you.
Screenshot_20240826-234700_Chrome.jpg


Screenshot_20240826-234423_Chrome.jpg


Ushahidi huo hapo, na link pia hiyo hapo.

 
Kiufupi Elon Ndio katia timu na amesha launch satellites kibao kwa ajili ya hili ,hawa waseng£ wanaooona raia ni kama misukule wao wa kuwakamua.tu wajisikiavyo litaisha na wataisoma namba tu ,ni suala la muda
Huyu mmarekani anamean business ,na atatengeneza pesa kweli kweli ,si masikhara , suala la internet coverage Africa kinahitajika sana

Na wazungu wanajua biashara vibaya mno, wanatumia ile kanuni ya "weka kiasi kidogo ili wateja wawe wengi then faida iwe kubwa", na ndo kanuni ambayo wachina wameiga japo ubora mdogo ila imewapa matokeo mazuri sana.

Hapo kina voda na tigo lazima walale na viatu mämæ

Itafika time kununua vifaa vya elon itakuwa laki na ushee tu. Time will tell
 
Maskini wengi wanadhani Starlink inawahusu. Hata ikiletwa leo watakaomudu gharama za Starlink ni wachache mno. Starlink hawana bundles za buku. Unalipia kwa mwezi sio chini ya laki. Na pia lazima ununue vifaa vyao ni zaidi ya Tsh 2m. Starlink iliingia Zambia mapema ila hadi leo raia wengi hawaitumii internet yao. Kwa Tanzania ni bei tu ya bundles zishuke ndo suluhisho. Starlink sio suluhisho
Una akili ila jina sasa.
 
Thed weld dwellers bana FANYENI kazi nyie acheni kuendekeza na kupenda anasa. Internet ni anasa tu kwenu kuchat chat na madem na umbea mtandaoni.

Hii nchi unaweza kusafiri zaidi ya kilomita 500 ukakutana na maripori manene yasiondelezwa yapoyapo tu kizembe. Nendendo huko mkayasafishe mjishughulishe.

Jerry komaa hapo hapo kama Nape.

Panueni wigo mpana.
Internet sio anasa kwa sasa ni lazima hata watumishi wa umma wanajaza majukumu yao kwenye mfumo
 
Internet sio anasa kwa sasa ni lazima hata watumishi wa umma wanajaza majukumu yao kwenye mfumo
Tatizo ni kwamba wachache wanaamini kuwa mtu kupata mtandao ni makosa ya jinai
 
Nataka niagize ivo vifaa apo kenya nifunge nyumban kwangu nina uhakik apa nilipo nitatumia bila shida na hakuna atakaeona akanichoma kwa wenyewe nchi😄
 
Nataka niagize ivo vifaa apo kenya nifunge nyumban kwangu nina uhakik apa nilipo nitatumia bila shida na hakuna atakaeona akanichoma kwa wenyewe nchi😄
Kesho nataka niingie border hpo nitafute kifaa changu! Nipige biashara! Naweka mtaani hapa!
 
Hii nchi unaweza kusafiri zaidi ya kilomita 500 ukakutana na maripori manene yasiondelezwa yapoyapo tu kizembe. Nendendo huko mkayasafishe mjishughulishe.
Acha kuwaponza watu wewe. Maeneo ya watu unaita mapori?
Hauwezi kuwa serious, yaani nikute tu pori nianze kulisafisha kisha nilitumie kibiashara!?
Maisha sio rahisi kiasi hiki.
 
Aliyekuwa waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye aliwahi kusema kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa na taasisi za kimataifa, Tanzania inashika nafasi ya sita kwa Bara la Afrika kwa kuwa na gharama za chini za bando “vifurushi” huku ikishika nafasi ya 50 Duniani kwa gharama ya chini ya data.

Nape alitoa ufafanuzi huo wakati aliposhiriki kipindi cha Power Breakfast on Saturday cha Clouds TV na redio, Agosti 20, 2022 jijini Dar es Salaam ambapo alisema na kudai kuwa bei ya data kwa wastani wa 1GB ni Dola 1.71 sawa na shilingi 3990. Maneno ya Nape yalikuwa “Tanzania kuwa miongoni mwa Mataifa yenye gharama za chini za mawasiliano haimaanishi kuwa itapunguza malalamiko kwa kuwa uchumi wetu haufanani na wananchi wengi wana kipato cha chini”.

View attachment 3079455

Nape alidai kuwa Serikali kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeendelea kufanya tathmini ya gharama za uwekezaji, utunzaji na usafirishaji wa data kila baada ya miaka minne na tathmini nyingine inafanyika mwaka huu ili kupata uhalisia wa gharama za bando kama zitapanda au kushuka.

Aidha, Nape aliweka wazi kuwa Serikali imeruhusu ushindani kwa kuweka mazingira wezeshi ya kuwa na kampuni nyingi zinazotoa huduma za mawasiliano ambapo huduma ya vifurushi ni huduma ya ziada inayotolewa na makampuni hayo na kuleta unafuu wa gharama za mawasiliano.

View attachment 3079456

Kama ni mfuatiliaji wa mtandao na habari za ulimwengu basi ni wazi umepata kuona viongozi wa Safaricom Kenya wakikutana na kitu kizito sana kutoka kwa Elon Musk, dharau zao sasa zimekuwa majuto kwao kwa kile ambacho Starlink wamekuja kuwapatia nafuu ya gharama za mtandao ndani ya Kenya. Kwa taarifa za wazi kutoka mtandao wa X unadai kuwa mtu anaweza kufurahia mtandao kwa gaharama ya 40657.50 sawa na dola 15 za kimarekani.

Safaricom kwa sasa hawana ujanja tena kwa kile ambacho kinaendelea ndani ya Kenya, ni Safaricom ambao walikuwa wanafanya kazi kwa mazoea na kiburi kikubwa, huduma mbovu kupita maelezo na kuzima mtandao kwa maagizo ya serikali. Starlink anakuja katika Wakati ambao wakenya wengi wamechoshwa kupita maelezo. Kwa sasa sijui utamwambia nini Mkenya aendelee kutumia huduma za mtandao kutoka Safaricom Wakati ameona kuna nafuu kubwa sana ya kutumia Starlink.

View attachment 3079457

Mageuzi haya yasiishie tu ndani ya Kenya bali Starlink fanya hima na Tanzania mje ili mitandao yetu hii ipate kujifunza na kukaa kwa adabu! Mara kadhaa gharama za bando zimekuwa zikipanda tu bila mpangilio wowote wa msingi huku TCRA akiwa kimya kama haoni kinachoendelea. Starlink akija Tanzania atatuonesha wapi panavuja na wapi kuna tatizo kabsa ndani ya hizi kampuni za mawasiliano.

Je unadhani Starlink akija Tanzania, utaendelea kununua bando la wiki kila siku au utahamia Starlink bila hata kuaga mtandao wako?​
Ziendelee kalala kuna siku zitakuta kumekucha
 
Acha kuwaponza watu wewe. Maeneo ya watu unaita mapori?
Hauwezi kuwa serious, yaani nikute tu pori nianze kulisafisha kisha nilitumie kibiashara!?
Maisha sio rahisi kiasi hiki.
Kabsa Mkuu
 
Screenshot_20240925_163307_Reddit.jpg

Kutoka mtandaoni huko 😃 mambo yanaanza kuwa moto moto.
 
Starlink kuja Tanzania ni ngumu sana kwa sababu viongozi wengi, wana HISA katika makampuni ya mawasiliano, short and clear.
Rais wetu auvunje mzizi wa fitina ili Watanzania tufaidike na revolution speed and super telecom services!
Ni kweli kabsa! Wanaona ni threat kwa pesa na uwekezaji wao
 
Hakuna poti lisilomilikiwa.Ukitska ujue mmiliki jidanganye kujipeleka kama hujafurushwa kama mvamizi.
Ni kweli mtu anaona Pori ila kiuhalisia ni makazi ya watu
 
Aliyekuwa waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye aliwahi kusema kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa na taasisi za kimataifa, Tanzania inashika nafasi ya sita kwa Bara la Afrika kwa kuwa na gharama za chini za bando “vifurushi” huku ikishika nafasi ya 50 Duniani kwa gharama ya chini ya data.

Nape alitoa ufafanuzi huo wakati aliposhiriki kipindi cha Power Breakfast on Saturday cha Clouds TV na redio, Agosti 20, 2022 jijini Dar es Salaam ambapo alisema na kudai kuwa bei ya data kwa wastani wa 1GB ni Dola 1.71 sawa na shilingi 3990. Maneno ya Nape yalikuwa “Tanzania kuwa miongoni mwa Mataifa yenye gharama za chini za mawasiliano haimaanishi kuwa itapunguza malalamiko kwa kuwa uchumi wetu haufanani na wananchi wengi wana kipato cha chini”.

View attachment 3079455

Nape alidai kuwa Serikali kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeendelea kufanya tathmini ya gharama za uwekezaji, utunzaji na usafirishaji wa data kila baada ya miaka minne na tathmini nyingine inafanyika mwaka huu ili kupata uhalisia wa gharama za bando kama zitapanda au kushuka.

Aidha, Nape aliweka wazi kuwa Serikali imeruhusu ushindani kwa kuweka mazingira wezeshi ya kuwa na kampuni nyingi zinazotoa huduma za mawasiliano ambapo huduma ya vifurushi ni huduma ya ziada inayotolewa na makampuni hayo na kuleta unafuu wa gharama za mawasiliano.

View attachment 3079456

Kama ni mfuatiliaji wa mtandao na habari za ulimwengu basi ni wazi umepata kuona viongozi wa Safaricom Kenya wakikutana na kitu kizito sana kutoka kwa Elon Musk, dharau zao sasa zimekuwa majuto kwao kwa kile ambacho Starlink wamekuja kuwapatia nafuu ya gharama za mtandao ndani ya Kenya. Kwa taarifa za wazi kutoka mtandao wa X unadai kuwa mtu anaweza kufurahia mtandao kwa gaharama ya 40657.50 sawa na dola 15 za kimarekani.

Safaricom kwa sasa hawana ujanja tena kwa kile ambacho kinaendelea ndani ya Kenya, ni Safaricom ambao walikuwa wanafanya kazi kwa mazoea na kiburi kikubwa, huduma mbovu kupita maelezo na kuzima mtandao kwa maagizo ya serikali. Starlink anakuja katika Wakati ambao wakenya wengi wamechoshwa kupita maelezo. Kwa sasa sijui utamwambia nini Mkenya aendelee kutumia huduma za mtandao kutoka Safaricom Wakati ameona kuna nafuu kubwa sana ya kutumia Starlink.

View attachment 3079457

Mageuzi haya yasiishie tu ndani ya Kenya bali Starlink fanya hima na Tanzania mje ili mitandao yetu hii ipate kujifunza na kukaa kwa adabu! Mara kadhaa gharama za bando zimekuwa zikipanda tu bila mpangilio wowote wa msingi huku TCRA akiwa kimya kama haoni kinachoendelea. Starlink akija Tanzania atatuonesha wapi panavuja na wapi kuna tatizo kabsa ndani ya hizi kampuni za mawasiliano.

Je unadhani Starlink akija Tanzania, utaendelea kununua bando la wiki kila siku au utahamia Starlink bila hata kuaga mtandao wako?​

Haya mambo ya kuwapa OYA OYA nafasi kubwa za maamuzi, ambao hawana uwezo wala weledi, yanaigharimu sana Africa.
At least mtu awe anajitingisha basi. Kuna mijitu akili zimetulia hapo chini, utafikiri boga linalokua. Jinsi siku zinavyoenda na ujinga na uzezeta unavyoongeza.
Kuwa kada sio lazima kuwa kiongozi mzuri kwenye ofisi za umma. Tujirekebishe. Wakati ukuta
 
Back
Top Bottom