mzee puto kapagawa mwezi na nusu sasa ameshindwa kumaliza mchezo, na majeshi yake yamekula mkong'oto yamerudi nyuma, sasa imebidi ajipange tena maana alifikiri vita ingekuwa rahisi kwake amebweeka mara ohh naweka makombora ya nyuklia kwenye high alert wanaume wanamtazama tu wala hawatishiki, mara ohh wanajeshi wa ukraine wajisalimishe wenyewe, wanaume wakakaza, mara ohh atakayemsaidia ukraine nitadeal nae, ukraine kasaidiwa na anaendelea kusaidiwa, sasa chawa wa russia wakasema ohh zelensky ashakimbia nchi, Boris jana alikuwa naye kyiev anagonga mvinyo huku wakilicheka babu puto kwa zerauu, na Italy ashasema soon anareopen ubalozi wake, huku finland na sweden inatarajiwa soon watajoin nato. Kwa kifupi putin kwa sasa anachezeshwa kama mwanasesere kufanya regime change aweke kibaraka wake ameshindwa, kwenye uchumi amefeli, rafikiye mchina amamtazama kwa mbaaaaali maana anajua kwa sasa russia ananuka nuksi na shombo laana so hataki kujiungamnisha naye kwa 100% maana anajua urusi kiuchumi si size yake yeye kwa sasa anataka ampiku US. Huku rafikiye Imran Khan wa pakistan naye kafurushwa yaan ni sheeeda. Sasa hapo anapambana na ukraine anatokwa na jasho la nywele halafu eti ndo awe na uwezo wa kuikabili nato thubutuuuu ingawa warusi wa mchambawima na matombo watabisha maana wana mahaba sana na babu puto na watakwambia babu puto ana akili nyingi sanaaaaa.