Vita ya vifaru kule Vulhedar/Bakhmut ishara ya ushujaa wa Urusi

Vita ya vifaru kule Vulhedar/Bakhmut ishara ya ushujaa wa Urusi

Katika vita hua Kuna hatua Fulani inafikiwa,
Mfano.
Ili kufika mahala Fulani ama kufikia malengo Fulani,
Ni ama mkubali kupoteza idadi kubwa ya askari na silaha na kisha kufikia malengo,

Ama kuepuka kupoteza idadi kubwa ya askari na vifaa lkn na hamtafikia malengo.

Bila kufikia malengo usumbufu mkubwa utatokea siku za mbele.
 
Kwa upande wangu tukiacha ushabiki pembeni, naona kama mwisho wa vita Kati ya Russia na Ukraine inakwenda kuishia pabaya zaidi.
Ukraine bado hajarusha silahaa ndani ya Russia kwasababu bado anajilinda...sababu anajua yeye.

Russia bado anatumia Askari wa kukodi kwa wingi pamoja na wafungwa akijua kuwa vita bado mbichi sana...sijui siku akiwaingiza askari wake kamili.

Nchi zinazomuunga Ukraine bado wanapeleka msaada interns of Money na Silaa siku...je siku wakiamua kuingiza askari wao pamoja na silahaa zao?

Nchi zinazomuunga Russia bado wanatoa msaada wa silahaa...je siku wakiamua kuingiza msaada wa askari na wataalam wao?

Sioni vita hii ikiacha Dunia sehemu salama pa kuishi tena.
Mmoja ataumia sana either Russia au Ukraine ndo vita itaisha, kwasasa Ukraine bado hajaumia sana kwasababu Russia anaumiza miundombinu kama majengo nk.
Russia hajaumia mpaka sasa kwasababu ajaanza kushambuliwa nyumbani kwake na yeye aanze kujilinda.

Tuombe vita iishe ili Dunia iwe sehemu salama pa kuishi.
Ukraine ndo kaumia na ataendelea kuumia....nchi yote imechomwa...hakuna hasara ya maana Russia kapata zaidi ya wanajeshi kuuawawa....Ukraine anaisha
 
Tumekusikia msemaji wa Wagner group na Urusi, muhimu unashindwa kuutambua nguvu na ujasiri wa Ukraine hapo tu ndo unapokosea msemaji.

Ukraine ni mbabe wa Russia, enzi za kuogopwa mrusi na majirani zake zimepitwa na wakati, mwaka umekata Putin ameshindwa kutwa Kyiv, alijaribu kupeleka pua yake Kyiv alichokipata hatamani kurudia tena.

Urusi anaendelea kupata hasara kila kukicha, jaribu kuwa mkweli ndg msemaji USA is another level, angekuwa ni USA mda huu tungekuwa tunazungumzia kusafisha safisha tu na kutoa msaada kwa raia wa huko baada ya mkong'oto mkali.

Urusi wamefeli bwashee, tuweke ushabiki maandazi pembeni, eb twende kiuhalisia, sioni kama mrusi atafanikiwa kilichobaki ni kujaribu kufuta aibu tu
Hivi unapumulia machine ukiwa wapi au ni kaka mkuu wa Milembe University? Aliyekwambia ktk hii vita urusi inaitaka Kiev ni nani? Yaani huyo US na UKubwa wake nae kajikusanya kwenye kikundi kinaitwa NATO ili kujilinda dhidi ya Russia halafu wewe njomba NCHUMARI unabisha? Ngoja Russia aendelee kuyafumua hayo mabwabwa
 
Back
Top Bottom