Vituko kutoka kwenye Makanisa ya Kilokole -Tupia chako

Vituko kutoka kwenye Makanisa ya Kilokole -Tupia chako

Jumapili iliyopita tarehe 27.06.2021 alikuwa Temeke Kata 15, yalitolewa Maji ya Bluu na PILAU DAWA na wikendi hii sijui itakuwa wapi,,,,, na Shekhe yupo salama mpaka leo.....
Huyo shehe anauza maji ya blue au hebu fafanunua ueleweke,, na hayo maji alikuwa anayauza msikitini?
 
Sabato ni siku gani?
Soma luka 23:50.........,then utaelewa ni siku gani.
Kama dunia nzima tunaadhimisha Ijumaa kuu kama siku ya kufa bwana wetu yesu kristo, na jumapili kama siku ya kufufuka bwana wetu yesu Kristo, basi utajua sabato ni siku gani.

Pia ushaidi mwingine ni huu hapa wa baadhi ya dictionary.
Screenshot_20210626-114009_UC%20Browser.jpg
 
Baba mmoja mkewe alikuwa anasali kanisa moja la kilokole ,ulokole ukamuingia kweli kweli yule mama,jumatatu hadi jumapili yeye ni kanisani akikosa kanisani anaenda nyumbani kwa mchungaji asubuhi anadamka anapika chakula cha kushinda nacho mpaka jioni muda ataokuwa kanisani,baba mwenye nyumba ile tabia ikamchomsha jumapili akaamka akaenda kanisani akawakuta wako kwenye maombi mchungaji yuko mbele,akamchukua mke wake mpaka mbele akawa anawagonganisha vichwa na mchungaji anawaambia eti "oaneni sasa"[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Sio mbali nyumba ninayoish mimi ,mke wa mtoto wa mama mwenye nyumba akiamka asubui tu kuoga na kuvaa nguo kanisan hata chai anywi basi naangalia kisha naona ufala tu

Sent from my Infinix X623 using JamiiForums mobile app
 
Kanisani, ma pastor namba wani ni sadaka, waumini wanamuomba mwenyezi mungu mpaka wana nena, wakitoka ni kutongozana na kupigana miti balaa
 
Tena umkute mwanamke anasali makanisa ya kilokole yanayochipuka kila siku,wabishi kweli sijui wanalishwaga sumu gani huko kanisani?halafu kila kitu kwao ni shetani, mfano huyo mama alikuwa anaambiwa na mume wake aende kanisani siku tatu katika wiki siku nne afanye mambo mengine yeye ndo kwanza anafunga na kusali anaona mumewe kaingiliwa na shetani !!!
Tatizo ni Moja tu, awana elimu ,tena hata hiyo biblia awaijui kwaiyo mengi wanakaririshwa na wachungaj wao,yan chochote ukimwambia akuelew ,sema ni hao waume zao ,mimi unaondoka mchana kweupe na mabeg yako uende huko kwa pasta

Sent from my Infinix X623 using JamiiForums mobile app
 
Ndugu usijumuishe kiasi hiko, nenda kwa Mwamposa J4 au J2 uone ni Waislamu kiasi gani wanaokwenda pale kununua Maji na Mafuta. Binafsi nimeshawaona wengi tu
Waislam jina awaja isoma dini ya kiislam vyema , ukiusoma uislam na kuulewa uwez yumbishwa na wapuuz kama wale , kuna siku eti Moja anaonyesha tende ,eti nimekunya hivi vitu baada ya kunywa maji ya baraka ,maji hata wew unaweza ombea ya kwako Mwenyew na yakawa tiba ,kwan yey anamuomba Mungu yup!?

Sent from my Infinix X623 using JamiiForums mobile app
 
Sasa huku mbeya , kuna familia imeanzisha kanisa lao wenyewe yan wamejenga kanisa kubwaaaa hatari ingawa wameezeka nusu afu idadi nadhani hawafiki hata kumi na tano lkn wamefunga maspika makubwa yan humo ndani no kelele tu sasa najiuliza c waongee tu bil mic maana wamekaa mabenchi mawili tu
Nipo mbeya tuonane basi
 
 
Soma luka 23:50.........,then utaelewa ni siku gani.
Kama dunia nzima tunaadhimisha Ijumaa kuu kama siku ya kufa bwana wetu yesu kristo, na jumapili kama siku ya kufufuka bwana wetu yesu Kristo, basi utajua sabato ni siku gani.

Pia ushaidi mwingine ni huu hapa wa baadhi ya dictionary.View attachment 1834955
Sabato iliyokuwa inaadhimishwa Siku ya Saba na Wayahudi katika Torati iliishia pale Msalabani!
Waebrania 4:4-8
Ile ilikuwa kivuli cha Yesu ambaye ndiye Sabato halisi,
Wakolosai2:16-18
Sabato maana yake ni Pumziko lililofanyika siku ya Saba,siku ambayo Wayahudi waliambiwa
Kupumzika kutoka kwenye Shughuli za mikono,Kutoka20:8-10
Lakini hiyo siku ilikuwa haiwapi Pumziko la Kweli!
Katika Agano Jipya Sabato inayozungumzwa ni ya Kupumzika katika Utumwa wa Dhambi,na hii ndiyo Sabato Halisi! Na Yesu Kristo ndiye Sabato ya Kweli,Ndiye aliyekuja kutuweka Huru mbali na Utumwa wa Dhambi!(Yohana8:31-34),Ndiyo maana aliwaambia Wayahudi kuwa,Njooni Msumbukao na Mizigo nipate KUWAPUMZISHA,(Mathayo11:28-29)
Kwa sababu hiyo Sasa,kwa Kufa na Kufufuka ameiondoa Siku ya Saba,na kuitaja Siku nyingine iitwayo LEO! Maadamu Yesu Kristo ni wa Jana,na LEO hata Milele,tumwendee atupumzishe na Dhambi,Waebrania13:8
Akishatupumzisha ndiyo tunaingia Raha ile Ya Sabato MBINGUNI,Waebrania 4:9
Watu wa Mungu watakaiongia Raha ya Sabato,Ni wale tu waliomwamini Kristo kisha wakatubu Dhambi na Kuokolewa,Marko16:16-18,Matendo2:38
Kwa hiyo mpendwa toka kwenye Kongwa la Torati,Njoo kwa Yesu Kristo akuokoe ili uingie Raha ile ya Sabato Halisi.
 
Wakuu, ni dhahiri kuwa kuna makanisa yanaibuka sasa kama uyoga. Sioni shida kuibuka kwa makanisa kila kukicha, kwasababu hata baa mpya zinaibuka kila siku.

Pamoja na yote, haya makanisa kuna baadhi yana vituko sana, yaani Mtumishi anaweza kuwa Mtume, Nabii au Mchungaji lakini mambo wanayofanya ni vituko na ajabu! Cha kushangaza bado waumini wapo.

Nianze mimi.
1. Hichi kituko kinaendelea kutokea kanisa moja Arusha, mtumishi kaacha familia Dar, kaenda kutumika Arusha kapachika muumini mimba, mke Kaenda Arusha, kulalamikia kanisa kuwa amefunga ndoa na huyo mtumishi, kituko Kanisa linamtetea Mtumishi kuwa wao hawakujua kama ameoa. Hivyo ataendelea kutoa huduma kanisani, can you imagine!!

2. Jamaa yangu huyu kaanzisha kanisa lake, kapata waumini wakutosha! Kaoa mke November, February mwaka unaofuata mke anaondoka na kila kitu, kwa madai mume wake ni mzinzi, shutuma zinafika kanisani, waumini wanaungana na mchungaji wao kukemea [emoji23][emoji23][emoji23]. hii ni Kilimanjaro.

3. Christina Shusho anaanzisha kanisa baada ya kutalakiana na Mume wake na ana waumini wakutosha. Ya kujifunza ni mengi hapa.

Tuendeleze vituko vingine....
Shusho kapewa talaka?
 
: Mwanzo2:2
Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya.

: Mwanzo2:3
Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya.

: Kutoka20:8
Ikumbuke siku ya Sabato uitakase.

M: Kutoka20:9
Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote;

: Kutoka20:10
lakini siku ya saba ni Sabato ya Bwana, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.

: Kutoka20:11
Maana, kwa siku sita Bwana alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo Bwana akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.

: Isaya66:22
Kama vile mbingu mpya na nchi mpya, nitakazofanya, zitakavyokaa mbele zangu, asema Bwana, ndivyo uzao wenu na jina lenu litakavyokaa.

: Isaya66:23
Na itakuwa, mwezi mpya hata mwezi mpya, na sabato hata sabato, wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema Bwana.

Luka 23:50-56
Luka23:54
Na siku ile ilikuwa siku ya Maandalio, na sabato ikaanza kuingia.

Luka23:55
Na wale wanawake waliokuja naye toka Galilaya walifuata, wakaliona kaburi, na jinsi mwili wake ulivyowekwa.

Luka23:56
Wakarudi, wakafanya tayari manukato na marhamu. Na siku ya sabato walistarehe kama ilivyoamriwa.
Ni wapi Biblia inapotaja kuwa siku ya Saba Ni jumamosi?
 
Sabato iliyokuwa inaadhimishwa Siku ya Saba na Wayahudi katika Torati iliishia pale Msalabani!
Waebrania 4:4-8
Ile ilikuwa kivuli cha Yesu ambaye ndiye Sabato halisi,
Wakolosai2:16-18
Sabato maana yake ni Pumziko lililofanyika siku ya Saba,siku ambayo Wayahudi waliambiwa
Kupumzika kutoka kwenye Shughuli za mikono,Kutoka20:8-10
Lakini hiyo siku ilikuwa haiwapi Pumziko la Kweli!
Katika Agano Jipya Sabato inayozungumzwa ni ya Kupumzika katika Utumwa wa Dhambi,na hii ndiyo Sabato Halisi! Na Yesu Kristo ndiye Sabato ya Kweli,Ndiye aliyekuja kutuweka Huru mbali na Utumwa wa Dhambi!(Yohana8:31-34),Ndiyo maana aliwaambia Wayahudi kuwa,Njooni Msumbukao na Mizigo nipate KUWAPUMZISHA,(Mathayo11:28-29)
Kwa sababu hiyo Sasa,kwa Kufa na Kufufuka ameiondoa Siku ya Saba,na kuitaja Siku nyingine iitwayo LEO! Maadamu Yesu Kristo ni wa Jana,na LEO hata Milele,tumwendee atupumzishe na Dhambi,Waebrania13:8
Akishatupumzisha ndiyo tunaingia Raha ile Ya Sabato MBINGUNI,Waebrania 4:9
Watu wa Mungu watakaiongia Raha ya Sabato,Ni wale tu waliomwamini Kristo kisha wakatubu Dhambi na Kuokolewa,Marko16:16-18,Matendo2:38
Kwa hiyo mpendwa toka kwenye Kongwa la Torati,Njoo kwa Yesu Kristo akuokoe ili uingie Raha ile ya Sabato Halisi.
Hapa wafuasi wa Ellen G. White sijui kama watakuelewa! Umedadavua vizuri sana mkuu!
 
[emoji23][emoji23][emoji23] zote kali.. Kinachoniacha hoi ni nabii mzinzi akilamatwa ugoni waumini wanamlinda na kumuombea eti ni vita!
Ukiyajua haya unapata wepesi wa fikra. Nadhani Kuna haja ya kuendelea kuabudu Kwa mujibu wa Imani zetu. Hizi za kuja zimeprove failure.
 
Back
Top Bottom