Vituko kutoka kwenye Makanisa ya Kilokole -Tupia chako

Vituko kutoka kwenye Makanisa ya Kilokole -Tupia chako

Katika juhudi zangu za kutafuta kanisa mkoa fulani, niliwahi ingia kanisa moja dogo tu ila wamefunga maspika hayo hatari.

Kulikuwa na muhubiri mmoja anaongea kiingereza na mwingine anatafsiri kwa kiswahili. Sasa kwenye mahubiri mtafsiri hajamaliza kutafsiri muhubiri kashaongea jingine full kelele halafu waumini wanashangilia balaa.
Muda wa maombi sasa ,Mhubiri anaomba kwa kutumia mike hizo kelele sasa si unajua maombi ya walokole, ikawa mara yangu ya kwanza na ya mwisho kukanyaga pale.
Ungetoka kabla ibada kuisha. Au ni dhambi!?
 
wanachonifurahisha waislam sio warahisi kivile kuingizwa mkenge.Ona Babu wa Loliondo alivyotingisha mataifa mbali mbali sasa amekuwa tajiri anasema kipindi hiki anataka kuja na kali kuliko ya kwanza
 
Dini ya kikristo imeyeyuka sana na imeshuka thamani michango mingi.

Saivi hakuna uhuru ukisali agrican wewe mroma unapigwa madongo, ukiwa mlokole ukihama kanisa unapigwa madongo, ukisali roma wewe ni kkt utapigwa madongo saa zingine unaonekana ni kondoo uliepotea hakika kwa sasa ubinafsi mkubwa wa kuona kila mmoja ana thamani tumekua wakujipenda wakati sisi wote kilio chetu ni kupitia mwana wa adam aliekufa msalabani,sisi ni watoto wa abraham, isaka na yakobo ila ukisema umeungana nao wanakupokea na kusema karibu ila ukiwa umeenda kujisalia vijembe vingi kuliko neno lenyewe.

Ubaguzi kama huna jumuiya kanisani utaisoma namba utasemwa sana, kuna watu tunataka kusali na kuondoka ila mwishoni makanisa mengine mnapigwa madongo jamani kwa biblia inalazmsha hayo kuna maeneo huwezi kuta kanisa lako.

Michango imekua mingi wakati hali hairuhusu kila kukicha ni kujenga makanisa likikamilika ujenzi mwingine sijui unatokea wapi Hakuna Amani Ya Kusali tena.

Kwa kweli hizi zama ni za mwisho tunasali kufuata ratiba lakini tumekosa uhusiano na Mungu kupitia kristo tunasali kutimiza wajibu ila ndani hakuna kitu kabisa.


All in all makanisa ya kilokole madhabahu zao wanaweka mazindiko mazito sana haiwezekani tulazimshwe kuzizunguka na kuomba wakati unaweza omba ukiwa hata umekaa kwenye siti yako.

Kuna kanisa moja hapa kati kati ya tz dodoma watu walipangwa kufanya ibada asubuhi kumbe kuna ng,ombe kachinjwa toka saa kumi usiku kufika saa kumi na mbili kisha iva wakaambiwa kuleni lakini mifupa kusanyeni sehemu moja, ilivyofika saa kumi na mbili wakiwa wamemaliza kula walianza ibada alitua tai mkubwa mida ya saa kumi na mbili na madakika wakaambiwa wamzunguke waombe wakiwa wamefumba macho.

Walivyomaliza watu walibaki mdomo wazi wakuhama walihama wakuendelea waliendelea.


Nimepita makanisa Mengi kwa sababu sio kila eneo utakuata kani lako mfano KKKT, AGRICAN na T.A.G lakini ROMAN CATHOlIC wamejipanga mpka vijiji ambavyo huwezi tegemea lakini wapo.
Eti wewe ni mtoto wa yakobo..

Ukute Ni lisukuma la Geita au Linyamwezi la Tabora linajiita litoto la Yakobo au isaka. Ujinga umewajaa vichwani.
 
Wakuu, ni dhahiri kuwa kuna makanisa yanaibuka sasa kama uyoga. Sioni shida kuibuka kwa makanisa kila kukicha, kwasababu hata baa mpya zinaibuka kila siku.

Pamoja na yote, haya makanisa kuna baadhi yana vituko sana, yaani Mtumishi anaweza kuwa Mtume, Nabii au Mchungaji lakini mambo wanayofanya ni vituko na ajabu! Cha kushangaza bado waumini wapo.

Nianze mimi.
1. Hichi kituko kinaendelea kutokea kanisa moja Arusha, mtumishi kaacha familia Dar, kaenda kutumika Arusha kapachika muumini mimba, mke Kaenda Arusha, kulalamikia kanisa kuwa amefunga ndoa na huyo mtumishi, kituko Kanisa linamtetea Mtumishi kuwa wao hawakujua kama ameoa. Hivyo ataendelea kutoa huduma kanisani, can you imagine!!

2. Jamaa yangu huyu kaanzisha kanisa lake, kapata waumini wakutosha! Kaoa mke November, February mwaka unaofuata mke anaondoka na kila kitu, kwa madai mume wake ni mzinzi, shutuma zinafika kanisani, waumini wanaungana na mchungaji wao kukemea 😂😂😂. hii ni Kilimanjaro.

3. Christina Shusho anaanzisha kanisa baada ya kutalakiana na Mume wake na ana waumini wakutosha. Ya kujifunza ni mengi hapa.

Tuendeleze vituko vingine....
Kanisa la mtaani kwangu kila siku wanaanza kupiga mayowe tangu saa 9 usiku. Juzi napita kichochoroni namkuta kiongozi wa kanisa anaongea na kabinti usiku neno la mwisho nililosikia alimwambia " si tutaenda wote mbinguni" dah
 
In short ukiwa kama ni Mkristo, unapaswa utambue hakuna kanisa ambalo halina mwanzilishi (mwanadamu mmoja au kikundi cha wanadamu) na hiyo ipo hivyo kwa kanisa kongwe au la sasa...

Hivyo kama kuna udhaifu wowote, hayo ni matokeo ya uwepo wa wanadamu kama viongozi au waumini...

Sisi wanadamu tumekuwa wepesi sana wa kuona watu wengine wasio na msimamo sawa na sisi kama wanakosea, aliye mlokole ataona asiye mlokole kapotea na kinyume chake pia...

Kama kuna mwanadamu wa imani yoyote aliye kamili kwa kila idara, basi na anyooshe kidole...

Na kama wewe ni Mkristo kweli (kwa kufuata maandiko), inasemwa huko kwamba mwenzako akipotoka wewe muombee arejee kwenye mstari na sio kuanza kumsimanga (usihangaike kutoa kibanzi kwa mwingine, ingali una boriti)


Lk 6:41-45 SUV
Basi, mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe huiangalii? Au, utawezaje kumwambia ndugu yako, Ndugu yangu, niache nikitoe kibanzi kilicho ndani ya jicho lako, nawe huiangalii boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe, itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe, ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi kilichomo katika jicho la ndugu yako. Kwa maana hakuna mti mzuri uzaao matunda mabaya, wala mti mbaya uzaao matunda mazuri; kwa kuwa kila mti hutambulikana kwa matunda yake; maana, katika miiba hawachumi tini, wala katika michongoma hawachumi zabibu. Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake.

Sent using Jamii Forums mobile app
: Mwanzo2:2
Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya.

: Mwanzo2:3
Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya.

: Kutoka20:8
Ikumbuke siku ya Sabato uitakase.

M: Kutoka20:9
Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote;

: Kutoka20:10
lakini siku ya saba ni Sabato ya Bwana, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.

: Kutoka20:11
Maana, kwa siku sita Bwana alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo Bwana akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.

: Isaya66:22
Kama vile mbingu mpya na nchi mpya, nitakazofanya, zitakavyokaa mbele zangu, asema Bwana, ndivyo uzao wenu na jina lenu litakavyokaa.

: Isaya66:23
Na itakuwa, mwezi mpya hata mwezi mpya, na sabato hata sabato, wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema Bwana.

Luka 23:50-56
Luka23:54
Na siku ile ilikuwa siku ya Maandalio, na sabato ikaanza kuingia.

Luka23:55
Na wale wanawake waliokuja naye toka Galilaya walifuata, wakaliona kaburi, na jinsi mwili wake ulivyowekwa.

Luka23:56
Wakarudi, wakafanya tayari manukato na marhamu. Na siku ya sabato walistarehe kama ilivyoamriwa.
 
Na mwingine yuko hapo Kimara anajiita Musa huyo ni noma balaa
Kuhani Mussa.😂😂.

Nasikia ili kwenda kumuona unajaza form, 100k.. then unasema shida yako kama ni kutabiriwa unatabiriwa!😁.. Daaah, watu wanapgwa balaa na akiwaamini hao jamaa, hata umwambie vipi hakuelewi yaan..
 
Masanja kawa Mchungaji
yule Pilipili nae yuko njiani kuwa Mchungaji

waumini wakuu wa haya makanisa ni wanawake
kwenye Maisha bhanaaa ombea ukubalike na wanawake utavuna mnooo
 
Religious interpreneur , wajasilia dini kazini ndani ya ngozi ya kondoo huku ni mbwa mwitu wakali .
 
"JINA LA BWANA LIBARIKIWE" Hii kauli niliisikia kwenye kanisa moja. Nikajiuliza kwa kuwa Bwana ndiye Mkuu sana ni nani tena mwingine aliye mkuu awezaye kulibariki jina lake?
 
Jaribu wewe siku moja nenda msikitini waambie mm nimeoteshwa nimeshukiwa na upako natoa maji ya baraka tena bure sio kwamba unauza kisha ulete mrejesho. Tatizo unashindwa kutofautisha dini na siasa,, mimi na wewe tunaweza kuwa dini tofauti lkn kwenye chama tupo pamoja, naweza nikakupigia kura wewe lkn yule wa dini yangu nisimpigie kwa sababu labda tunagombania mwanamke mmoja. Ila linapokuja suala la magumashi ndani ya msikiti lazima bakora zitembee. Msikitini hamna magumashi. We unayaonaje maisha ya muft mkuu wa waislam Tanzania nzima na maisha ya gwajizo foshizo[emoji1] ambaye ye ni mtu mmoja tu kaanzisha kanisa lake ukitaka kujua huko kwenu kuna magumashi na upigaji wa kufa mtu.
Maji ya baraka msikitini?.
 
Acha uongo,,, aliyekuwa anatangaza hayo maji ni aliyekuwa mchungaji anaitwa kessy,, alikuwa akiwaonyesha watu jinsi gani mnavyopigwa. Huyo shekhe yahya tangu lini umesikia anauza maji acha fiksi bana, kwanza waislam hawadanganyiki kizembe na hilo unalitambua usijitoe ufaham, yani uote afu uwatangazie watu ww mtume 😄
Ndugu usijumuishe kiasi hiko, nenda kwa Mwamposa J4 au J2 uone ni Waislamu kiasi gani wanaokwenda pale kununua Maji na Mafuta. Binafsi nimeshawaona wengi tu
 
kuna kanisa Mchungaji Mkuu ni Mwanamke Msagaji na waumini wote wanajua na asilimia tisini ya wanawake wanao enda kusali mahali hapo ni wanawake wanao fanya mapenzi na wanawake wenzao
 
Ndugu usijumuishe kiasi hiko, nenda kwa Mwamposa J4 au J2 uone ni Waislamu kiasi gani wanaokwenda pale kununua Maji na Mafuta. Binafsi nimeshawaona wengi tu
Kumbe wanaenda kununua kwa mwamposa mm nikajua labda wananunua msikitini,, sio waislam hao, zuga tu ili wakuvutie kama wewe apo
 
Back
Top Bottom