Vituko kutoka kwenye Makanisa ya Kilokole -Tupia chako

Vituko kutoka kwenye Makanisa ya Kilokole -Tupia chako

Siku asimame shekhe msikitini aseme kaoteshwa na mungu kwa hiyo kuna maji ya upako anauza kikombe Jero, huyo shekhe kama akitoka salama humo msikitini sijui,,,, lkn upande huu pili sijui kwanini mnaongopewa kizembe, yani masanja nae mchungaji achilia mbali yule wa kuitwa nabii frola😄
Mbona shehe yahaya majini anauza vichupa vya maji ya baraka kutoka uarabuni.

Siku hiyo ndio niligundua kuna mashehe hama mitume na manabii. Vimaji vinanguvu maana alipofungua kamoja tu uwanja mzima wanawake wakalipuka mapepo.
 
Baba mmoja mkewe alikuwa anasali kanisa moja la kilokole ,ulokole ukamuingia kweli kweli yule mama,jumatatu hadi jumapili yeye ni kanisani akikosa kanisani anaenda nyumbani kwa mchungaji asubuhi anadamka anapika chakula cha kushinda nacho mpaka jioni muda ataokuwa kanisani,baba mwenye nyumba ile tabia ikamchomsha jumapili akaamka akaenda kanisani akawakuta wako kwenye maombi mchungaji yuko mbele,akamchukua mke wake mpaka mbele akawa anawagonganisha vichwa na mchungaji anawaambia eti "oaneni sasa"[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
kimeumana
 
Nmegundua, wote waliochangia hili bandiko hawajasikiliza wala kuangakia Video iliyowekqa. Leo ndo nmeamini bando limepanda bei.

Kuna watu wakilisikiliza hiyo Video, watafuta Post zao. Wakurupukaji wanaitwa.

Hata mleta mada hajaaangalia Video yote. Ajabu
 
Siku asimame shekhe msikitini aseme kaoteshwa na mungu kwa hiyo kuna maji ya upako anauza kikombe Jero, huyo shekhe kama akitoka salama humo msikitini sijui,,,, lkn upande huu pili sijui kwanini mnaongopewa kizembe, yani masanja nae mchungaji achilia mbali yule wa kuitwa nabii frola😄
Acha kujisahaulisha...
Mbona mnauza miti shamba huko misikitini?
 
Wakuu, ni dhahiri kuwa kuna makanisa yanaibuka sasa kama uyoga. Sioni shida kuibuka kwa makanisa kila kukicha, kwasababu hata baa mpya zinaibuka kila siku.

Pamoja na yote, haya makanisa kuna baadhi yana vituko sana, yaani Mtumishi anaweza kuwa Mtume, Nabii au Mchungaji lakini mambo wanayofanya ni vituko na ajabu! Cha kushangaza bado waumini wapo.

Nianze mimi.
1. Hichi kituko kinaendelea kutokea kanisa moja Arusha, mtumishi kaacha familia Dar, kaenda kutumika Arusha kapachika muumini mimba, mke Kaenda Arusha, kulalamikia kanisa kuwa amefunga ndoa na huyo mtumishi, kituko Kanisa linamtetea Mtumishi kuwa wao hawakujua kama ameoa. Hivyo ataendelea kutoa huduma kanisani, can you imagine!!

2. Jamaa yangu huyu kaanzisha kanisa lake, kapata waumini wakutosha! Kaoa mke November, February mwaka unaofuata mke anaondoka na kila kitu, kwa madai mume wake ni mzinzi, shutuma zinafika kanisani, waumini wanaungana na mchungaji wao kukemea [emoji23][emoji23][emoji23]. hii ni Kilimanjaro.

3. Christina Shusho anaanzisha kanisa baada ya kutalakiana na Mume wake na ana waumini wakutosha. Ya kujifunza ni mengi hapa.

Tuendeleze vituko vingine....
[emoji23][emoji23][emoji23] zote kali.. Kinachoniacha hoi ni nabii mzinzi akilamatwa ugoni waumini wanamlinda na kumuombea eti ni vita!
 
Nmegundua, wote waliochangia hili bandiko hawajasikiliza wala kuangakia Video iliyowekqa. Leo ndo nmeamini bando limepanda bei.

Kuna watu wakilisikiliza hiyo Video, watafuta Post zao. Wakurupukaji wanaitwa.

Hata mleta mada hajaaangalia Video yote. Ajabu
Toa utapeli wako hapa.
 
In short ukiwa kama ni Mkristo, unapaswa utambue hakuna kanisa ambalo halina mwanzilishi (mwanadamu mmoja au kikundi cha wanadamu) na hiyo ipo hivyo kwa kanisa kongwe au la sasa...

Hivyo kama kuna udhaifu wowote, hayo ni matokeo ya uwepo wa wanadamu kama viongozi au waumini...

Sisi wanadamu tumekuwa wepesi sana wa kuona watu wengine wasio na msimamo sawa na sisi kama wanakosea, aliye mlokole ataona asiye mlokole kapotea na kinyume chake pia...

Kama kuna mwanadamu wa imani yoyote aliye kamili kwa kila idara, basi na anyooshe kidole...

Na kama wewe ni Mkristo kweli (kwa kufuata maandiko), inasemwa huko kwamba mwenzako akipotoka wewe muombee arejee kwenye mstari na sio kuanza kumsimanga (usihangaike kutoa kibanzi kwa mwingine, ingali una boriti)


Lk 6:41-45 SUV
Basi, mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe huiangalii? Au, utawezaje kumwambia ndugu yako, Ndugu yangu, niache nikitoe kibanzi kilicho ndani ya jicho lako, nawe huiangalii boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe, itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe, ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi kilichomo katika jicho la ndugu yako. Kwa maana hakuna mti mzuri uzaao matunda mabaya, wala mti mbaya uzaao matunda mazuri; kwa kuwa kila mti hutambulikana kwa matunda yake; maana, katika miiba hawachumi tini, wala katika michongoma hawachumi zabibu. Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maeneo ya mijini makanisa hayo yako mengi sana kuliko vijijini na sehemu ambazo watu hawana hela,

Je hii haitoshi kuonesha kuwa jamaa wako kutafuta pesa zaidi kuliko uinjilisti?
 
Dar ndio Ma mogul yamejazana huku.
1. Gwaji
2. Buldoza(Mwamposa)
3. Mzee wa Upako-mlevi mlevi huyu sikumbuki vizuri jina lake.


Sasa hivi wameanza kwenda Dodoma kama strategic region.

Wameona pamekuwa makao makuu pana fursa kidogo na watumishi wa Umma na wageni kwa hiyo sadaka zitapatikana kwa wingi kuliko zamani.

Yani wao wanalenga Penye kupata hela tu mengineyo ni ziada.

Wakati imeandikwa kuutafuta ufalme wa Mungu kwanza na haki yake yote na mengio kuzidishwa lakini wao wanaanza kutafuta mazidisho kwanza Yani mengineyo ufalme badae.

Utaua na kuridhika wafaa sana kuliko fedha na mali.
 
Back
Top Bottom