Viungo vya binadamu (idadi kubwa) vyaokotwa Bunju-Machimbo

Viungo vya binadamu (idadi kubwa) vyaokotwa Bunju-Machimbo

Jamani tusalini sana. Mmesikia kilichotokea jioni hii huko Bunju. Bodaboda wamefanikiwa kuikatama Susuz Carry iliyokuwa na miili ya watu zaidi ya 20 idadi kubwa ikiwa ni wanawake. Wamegawanywa vipande vinne na miili yote haina ngozi. Kwa mujibu wa reporter wetu aliyopo kituo cha Usalama Bunju anasema inasadikika miili hiyo imetoka maeneo ya Inter chick ila dereva ni wa Bunju hivyo wanasubiri uongozi Wa Juu Wa Polisi ufike eneo la tukio. Eeh Mungu tunusuru Watoto wako
nilipata taarifa kama zako ila TBC na ITV maelezo yao kwa mujibu wa taarifa za hapa hawajaeleza hayo ya Toyota sasa sielewi kama ni kweli ama la
 
duuuu hapa naona kama kuna malue lue maana kunawatu. washafanya uchunguzi wao nakuja na majibu kuwa hayo nimabaki kutoka vyuo VYA udaktari je ?? nikweli au ndio mnataka kudivert ukweli halisi
 
Viungo vya Binadamu vyaokotwa BUNJU MACHIMBO. Hali inatisha sana.
 

Attachments

  • 1405974928628.jpg
    1405974928628.jpg
    61.4 KB · Views: 494
  • 1405974950326.jpg
    1405974950326.jpg
    85.1 KB · Views: 486
Habari ya kusikisha usiku wa habari TBC one. Viungo vya BINADAMU vinavyokadiriwa zaidi ya 85 vyaonekana Bunju. Dereva wa gari la taka ashikiliwa.
 
Sawa tunakubali madaktari lazima wajifunze lakini baada ya mafunzo ndo wakazitupe maiti jalalani kwanini wasizichome hawa IMTU lazima washitakiwe kwa udhalilishaji wa binadamu
 
Hii ni bunju genocide...bwana mrisho naona kma kawaida yake atasympasize na genociders...!!
Cc kagame.
Intarahamwe.
 
mi mtu inawaza hela tu bila kujari utu yaani mtu anapewa gari akawamwage binadam wenzie dampo? Hivi kweli ni hapa Tanzania?

Mwenyewe nashangaa mkuu hata kama ni mafunzo kwa nini wasifukie huko jamani ama kweli tunapoelekea hiyo tabia mbaya wachukuliwe hatua kali watakaobainika kuhusika
 
Aisee madaktari wanakazi, kurukaruka na viungo vya binadamu kama hivyo hyo si so.?
 
Kwa wapenda amani wote hii habari inasikitisha sana. Police wachunguze na majibu yotolewe haraka kuwatoa wananchi wasiwasi. Mungu Ibariki TZ.
 
Mwenyewe nashangaa mkuu hata kama ni mafunzo kwa nini wasifukie huko jamani ama kweli tunapoelekea hiyo tabia mbaya wachukuliwe hatua kali watakaobainika kuhusika
Mkuu ukiona hivo ujue walifukia vyakutosha uko kwao nafasi zimejaa ndo wakatafuta altenative...lazima kuna kitu kibaya kinaendelea la sivyo huyo driva asingekamatwa..mungu tu ameamua kuwaumbua.
 
"Polisi wa kituo cha BUNJU A NA WAZO WANAPIGA RISASI HEWANI MUDA HUU ILI KUTAWANYISHA WATU WALIO VAMIA KITUO CHA POLISI BUNJU A ILI WAMUUE DEREVA ALIYEKAMATWA AKIENDESHA GARI AINA YA HILUX ILIYOJAA VIUNGO VYA BINADAMU AMBAVYO NI VIBICHI BADO VIKIWA VINAVUJA DAMU KWA TAARIFA NIKUWA DEREVA ALIFANIKIWA KUMWAGA TRIP YA KWANZA ENEO LA SHULE YA CONSOLATA YA MASISTA ALIPORUDI KUMWAGA TRIPU YA PILI NDIO WANANCHI WAKAITA POLISI. NI AJABU SANA JAMANI."
 
wananchi wenye hasira wanataka kumuua dereva polisi wanazuia, mwisho wa siku dereva anakuwa hana hatia anaachiwa huru kwani pengine ni kazi ya wakubwa fulani.

tena dereva akiuawa na wananchi itakuwa ngumu kupata habari wapi katoa mzigo huo japo najua wananchi tutafichwa ukweli tu, tume itaundwa na itachunguza hadi kiama.
 
Nimeona picha za viungo husika. Kuna gloves na nyembe za upasuaji ambazo zimehifadhiwa pamoja na hivyo viungo. Japo sijui mazingira ya tukio, lakini ni muhimu pia kujua baadhi ya vyuo vya magonjwa ya tiba ya binadamu huwa vina dispose wapi mabaki ya cadavers wanazotumia?
 
Nimeona picha za viungo husika. Kuna gloves na nyembe za upasuaji ambazo zimehifadhiwa pamoja na hivyo viungo. Japo sijui mazingira ya tukio, lakini ni muhimu pia kujua baadhi ya vyuo vya magonjwa ya tiba ya binadamu huwa vina dispose wapi mabaki ya cadavers wanazotumia...
 
Back
Top Bottom