Viungo vya mwili kufa ganzi: Elewa Chanzo, Tiba na mambo muhimu ya kuzingatia

Viungo vya mwili kufa ganzi: Elewa Chanzo, Tiba na mambo muhimu ya kuzingatia

Hapati homa,ila miguu na vidole ndio vinauma,sometimes kiuno pia tangu ajifungue,hospitali alienda wakamwambia asubirie ndani ya miezi mitatu toka alipo jifungua kama tatizo linaendelea basi aende tena hispitali.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nenda hospitali kubwa zaidi ikiwezekana aende emergency.
 
Habari wadau,kama kichwa kinavyojieleza hapo juu. Nasumbuliwa na ganzi sana miguuni( kuanzia magotini hadi chini) mikononi( kuanzia kwenye viwiko hadi kiganjani) mpaka kutembea shida tafadhari msaada wadau nimetingwa sana.

Nenda Hospitali kapime Bp, Kisukari, Figo, Mafuta kwenye damu, Moyo etc kwani hii inaweza kuwa ni dalili za kwanza kabla ya shambulio la Moyo " Heart attack" achana na hao wapiga ramli na wauza dawa mitandaoni
 
Nenda Hospitali kapime Bp, Kisukari, Figo, Mafuta kwenye damu, Moyo etc kwani hii inaweza kuwa ni dalili za kwanza kabla ya shambulio la Moyo " Heart attack" achana na hao wapiga ramli na wauza dawa mitandaoni
Ahsante sana kwa ushauri.
 
deo paul555, GANZI, ni tatizo linaloashiria kukosekana kwa fahamu katika sehemu hizo. Hisia ndiyo inakosekana kwa sababu hakuna damu na neva zinakosa mawasiliano ya moja kwa moja na ubongo.

Ni jambo la kawaida linalowapata watu wengi sana katika miaka ya hivi karibuni, lakini pasipo kujua nini chanzo chake wala tiba.

Vyanzo vya ganzi mwilini

Vifuatavyo vinatajwa kuwa vyanzo vya ganzi mwilini mwa binadamu:

1. Shinikizo la muda mrefu.
2. Kuwa karibu na vitu vyenye baridi sana kwa kipindi kirefu.
3. Mabadiliko ya muda mfupi kwenye neva/mishipa.
4. Ajali kwenye neva.
5. Kunywa pombe kupita kiasi.
6. Uvutaji sigara na bangi.
7. Uchovu usioisha.
8. Kutokujishughulisha na mazoezi ya viungo kila mara.
9. Ukosefu wa vitamini B12 na Magnesiamu mwilini,
10. Ugonjwa wa kisukari n.k

Kwa kawaida, ganzi inayotokea kwa dakika kadhaa na kupotea huwa haina shida yoyote.

Inaelezwa, ni vyema kuonana na daktari mapema ili kupata vipimo, iwapo ina kawaida ya kutokea kila mara na inadumu muda mrefu. Inaweza kuwa ishara ya ugonjwa fulani unaohitaji matibabu ya haraka.
 
deo paul555, Habari? Mke wangu alikua na tatizo hili la ganzi miaka iliyopita. Alisumbuka sana maana hata usiku alikuwa hawezi jifunika shuka miguuni na mikononi. Nilijaribu kumpeleka hosptal but wapi japo walimpa dawa kibao miongoni mwa hizo ni neural support but ikashindikana.

Katika soma soma yangu humu JF nikaomba ushauri nikaambiwa nijaribu kubadili life style ya lishe! Hapo nikafuata ushauri aisee utafikiri JF ndiyo walijua wamemroga ile ganzi ikaanza kuisha na kupotea mpaka sasa.

Ndugu yangu achana na waganga hao watakumalizia vihela vyako buree, kwa ushauri wangu kwako kutokana na niliyopitia nenda hospital. Lakini muhimu badili life style ya vyakula vyako. Jitahid kula mboga za majani, samaki ugali usiokobolewa na vingne vya kujenga mwili wako. Acha na bia chipsi!
 
Wakati ukiendelea kupata tiba, achana na vyakula vyenye Gluten hasa ngano na ubwabwa, punguza matumizi ya sukari.
 
Nimekuwa nahisi ganzi kichwani na kupepesuka haiumi na wala hainipotezei nguvu ya kufanya kazi Ila inashuka mpaka usoni upande wa kuume. Kuna siku nikiamka asubuhi nakuta mikono nayo imekufa ganzi.

Nisaidieni dawa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
HI,
Samahani wakuu.

Mimi kwa sasa niko na shida moja kwenye vidole vya mikono usawa wa kucha ni kama vina ganzi hasa nikivibinya vinaonyesha hali fulani ya kuwa na ganzi.

But sijajua nini tatiza mpaka sasa. Kwa sasa mwezi unakaribia kuisha.

Ila nikitaka kwenda hospital naona uvivu au nakosa muda.
 
Back
Top Bottom