Viwango vilivyopendekezwa na Serikali, Bima ya Afya kwa Wote

Viwango vilivyopendekezwa na Serikali, Bima ya Afya kwa Wote

kalacha mateo

Senior Member
Joined
Sep 27, 2021
Posts
119
Reaction score
240
Hivi karibuni, Rais Samia Suluhu alisema serikali itapeleka mswaada wa Bima ya Afya bungeni ili uweze kujadiliwa. Wakati mchakato huo unaendelea Serikali kupitia Wizara ya Afya imependekeza viwango vya kulipia kwenye Bima.

Prof. Makubi amesema uchangiaji unaopendekezwa ni Sh. 340,000 kwa kaya ya watu 6 na Sh. 84,000 kwa mtu mmoja asiye na familia kwa mwaka.Kiwango hiki ukilinganisha na gharama za matibabu ni ndogo na serikali bado itafidia gharama nyingine.

"Sheria hii ya Bima ya Afya kwa wote inaenda kuwakomboa wananchi, inaenda kuhakikisha kila mwananchi, Mtanzania anakuwa na Bima ya afya, kwa sasa hivi takribani 15% tu ya wananchi wanabima za afya mbalimbali, inawaacha 85% ya Watanzania kutokuwa na uhakika wa kutibiwa".

Prof. Makubi amebainisha kuwa kwa wananchi watakaotambuliwa kutokuwa na uwezo wataendelea kupatiwa huduma kwa utaratibu utakaowekwa na Serikali kwa kila mtu kuwa na kadi yake ya Bima ya Afya.
 
Hata mimi nawaza hivyo, kama tu ya watoto imewatoa jasho hii ndio itakuwa balaa kabisa.
Ni lazima italemewa halafu waanze zile style ya kuna shida ya network
Hii nafikiri watawin, waziri alisema, mtoto au mtu mzima ukiona anakatiwa bima basi ujue ni mgonjwa kuepuka gharama zaidi wanamkatia bima at the end mfuko unalemewa, lakini hii ya kila mtu itabalance maana wengi unaisha mwaka hajaingia hospital au homa ndogo ananunua dawa dukano ful stop.

Nafikir kwa mfumo huo pesa zitatosha na kubaki nyingi tu.!
 
Hii nafikir watawin, waziri alisema, mtoto au mtu mzima ukiona anakatiwa bima basi ujue ni mgonjwa kuepuka gharama zaidi wanamkatia bima at the end mfuko unalemewa, lkn hii ya kila mtu itabalance maana wengi unaisha mwaka hajaingia hospital au homa ndogo ananunua dawa dukan ful stop.
Nafikir kwa mfumo huo pesa zitatosha nakubaki nyingi tu.!
Unanunua kwa sababu unajua ukienda hospital wni gharama ila ukiwa na bima ni rahisi kwenda tena hospital za private kama Rabininsia, Kitengure n.k.
Kuna matatizo ya kiafya ukiwa huna bima utayatibu kwa home remedies ila ukiwa na bima utajikuta tu unakwenda hospital.
 
Inasikitisha sana viongozi wanaposhindwa kujua hali za wananchi wao. Tunayo maelfu ya kaya zisizoweza kumudu milo miwili kwa siku, unawaambia walipe hiyo pesa wataitoa wapi?

Na kwanini swala la bima ya afya liwe lazima?

Wanasiasa wetu wakiondoka duniani wanachokutana nacho kitakuwa kitisho kikubwa.
 
Inasikitisha sana viongozi wanaposhindwa kujua hali za wananchi wao. Tunayo maelfu ya kaya zisizoweza kumudu milo miwili kwa siku, unawaambia walipe hiyo pesa wataitoa wapi?

Na kwanini swala la bima ya afya liwe lazima?

Wanasiasa wetu wakiondoka duniani wanachokutana nacho kitakuwa kitisho kikubwa.
Hivi hawa asilimia kama 28 wanaoishi chini ya dola 1.5 kwa siku wataweza kulipia. Fikiria wauza karanga wakina mama wadogo wadogo waponda kokoto wauza bagia nk.

Pili mtu atakuwa huru kwenda hospitali anayoitaka iwe binafsi au ya umma au watu watapigwa pini waende hospitali za umma tu tena ngazi ya chini kama vituo vya afya na zahanati. Ikiwa hivyo maana yake watu bado wataenda hospitali bora za binafsi kwa kujilipia licha ya kuwa watakuwa wamechangia kiasi hicho cha pesa bima.
 
Hivi hawa asilimia kama 28 wanaoishi chini ya dola 1.5 kwa siku wataweza kulipia. Fikiria wauza karanga wakina mama wadogo wadogo waponda kokoto wauza bagia nk.
Mtu hata unashindwa kujua hawa binadamu wana vitu gani vichwani mwao.

Na kila siku yanaingia makanisani na misikitini.
 
Unaenda hospitalini, unapimwa malaria, unagundulika unayo dawa hakuna "Nenda duka la madawa, dawa zimeisha bado serikali haijaleta" .......MWEWE huyooo anaruka......
 
Unanunua kwa sababu unajua ukienda hospital wni gharama ila ukiwa na bima ni rahisi kwenda tena hospital za private kama Rabininsia, Kitengure n.k.
Kuna matatizo ya kiafya ukiwa huna bima utayatibu kwa home remedies ila ukiwa na bima utajikuta tu unakwenda hospital.
Inategemea, labda nikitoka nje tu ya nyumba ndo naiona aghakan hii hapa ndo nikiumwa naenda, lkn asilimia kubwa hoptl kubwa na zinazotumia bima huwa mbali na makazi kwa hiyo kichwa kinauma nipande bus wakati naona duka la dawa hili naliona naweza kupata flagile tumbo likatulia.
Bima kwa wote maana yake kumbuk mpaka wa vijijin pia
 
Back
Top Bottom