Vladimir Putin amewataka wanajeshi wa Ukraine wajisalimishe wenyewe


hapo kwa gengis khan umenikumbusha ile tamthilia kali ya kituruki vile etuglu anavyopambana na wamongoli ambao kiongozi wao mkuu ni khan wa makhan gengis khan.

mimi huwa naifatilia kule youtube, ila nasikia huwa inaonyeshwa na tv fulani hapa bongo.
 
Russia hayuko vizuri kiuchumi ukilinganisha na wenzake wa Western countries, hata kipato Cha mrusi mmoja mmoja ni kidogo
Punguza upumbavu kidogo kichwani kwako. Russia ni wa 11 Duniani unawezaje kusema hawana uchumi?

Nchi za Europe zilizompita Russia ni nne tu, na hapo hizo data zimetolewa na WB ambao ni anti-Russia.
 
Unatoa hayo ukiwa wapi buzza kwa kwa mpalange . ko wewe na puttin yupi mwelewa zaidi kuhusu faida ya vita hiyo
 
Basi wewe ndiye mtu wa ajabu kwa mwezi huu wote, ukraine ni point muhimu ya kiulinzi kwa urusi , sawa na zanzibar kwa tanzania
Kwa hiyo tuivamie Zanzibar, tuivunje SMZ na kuigeuza mkoa.

Putin amesaini mikataba ya usalama kuhusu Ukraine. Ukraine imebomoa silaha zake zote za nuklia katika mikataba hiyo. Ukraine bado haijakubaliwa kuwa mwanachama wa EU wala NATO. Ukraine haijawahi kutishia maslahi ya Urusi hata mara moja. Diplomatic channels are all open.

Kinyume chake Putin amekiuka mikataba yote na kuvamia na kukalia majimbo ya Ukraine: Crimea na Donbas (Donetsk na Luhansk). Sasa anataka kuichukua Ukraine yote! Kwa jeuri ya mtu mmoja tu!

Putin haitambui Ukraine kama nchi huru (sovereign territory). Anadai ilikuwa sehemu ya ufalme wa Russia (Imperial Russia 1721-1917). Anataka kuirejesha Urusi.

Ni madai ya kipuuzi yasiyokubalika kisheria kimataifa. Ndio maana anatumia mbinu za Hitler za kusema uongo kuanzisha vita ya kipumbavu. Ameamua kujidhuru. Hayuko sawa kichwani. Time wil reveal soon.
 
Unajidanganya anajua analolifanya pro Amerika wewe, marekani kavamia mataifa mangapi?? Mbona haujasema uchumi wake umeyumba.unajua uchumi kuyumba wewe
 
Uko sawa kabisa mkuu sunction tu ndo kitu wanaweza fanya..
Sio kuingia kwenye vita ya uyo jamaa..
Madhara ni makubwa sana kuliko watakachoenda kupigania.
 
Bei ya mafuta ishapanda duniani, tutegemee mwezi ujao yawe Tshs 2800
 
una uhakika kwamba uamuzi huo hauna manufaa kwa nchi yake? Mzungu sio mjinga kiasi iko
Soma habari za Hitler, Himmler, Mussolini, Ceausescu na hivi leo Trump (aliyewaita sthl) na Bolsonaro ujue wapo wazungu wa kila aina.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…