Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Mimi wananifanyia uhoneythi lakini nakomaa nao tu hivyo hivyo huku najipa moyo labda watajirekebisha kesho senzy kweli hawa vichwabuta
 
hata tiGO nao wana mambo hayohayo mimi nilinunua muda wa maongezi wa tsh10,000 kwenye tiGO pesa hawakunipa lakin salio wamenikata,,Customer care wanakuambia tatizo linapelekwa idara husika subir masaa24 litatafutiwa ufumbuzi,,hadi leo hii kimya. WEZI sana hawa Voda na Tigo sijui hawa Airtel maana sijawahi tumia.
 

hapi nyu iya kaka f80
 
Habari ndugu mteja,tafadhali tutumie namba ya simu PM kwa msaada zaidi,pole.
Mnaudhi sana tu nyie, kwanza limtandao lenu net inakata hovyo hovyo na hakuna maelezo ya kujitosheleza.

Halafu kuna na ile bundle ya unlimited ya mwezi ile ndo full upuuzi.
 
Ninatumia modem ya voda haija nisumbua hata kidogo.
 
Ninatumia modem ya voda haija nisumbua hata kidogo.

na wewe ndio haohao tu ila different ID. mimi wameanza nami mwaka mpya kwa kukwangua kavocha kangu ka 500. imebidi ninunue tena muda wa maongezi mara mbili ili kujiunga. PERIOD
 
Kumbe Voda Wako humu, sasa mbona malalamiko mengi sana but wamekaa kimya tu?????
 
Pole sana. Mi imekuwa ikinitokea mara nyingi sana. Nanunua muda wa maongezi kutoka M-Pesa.

Na unapata ujumbe wa kuthibitisha kuwa umenunua kiasi kadhaa. Cha ajabu, ukiangalia salio unakuta hakuna kitu.
 
Mijizi sana midude hii ukiweka vocha ktk cimu au modemu hata bila kuitumia ikikaa nusu SAA tu kosa ukiangalia salio ni sifuri najuta na nataangaza kuuhama
 
Tangia wameiba elfu kumi yangu mpesa, sijatumia voda tena na kiline chao metupia mbali huko
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…