Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Tabia yenu ya kukata sh.150 kwa ajili ya magazeti ambayo yanaleta habari za juzi hatutaki. Msituunganishe na huduma za kijinga. Habari mnazotuma mistari miwili afu mnakata 150. Nitakuja kuwashitaki mahakama ya kimataifa kama tanzania wanashindwa kuwadhibiti na wizi wenu
 
Ndugu mteja,

Una tatizo lolote unapotumia mtandao wetu? Una ushauri wowote ili tuiboreshe huduma yetu?

Tafadhali itumie mada (thread) hii ili tukusaidie kwa urahisi.

Unapokuwa na tatizo, ili tukusaidie kirahisi zingatia haya:

- Ni tatizo gani? (M-PESA, SMS, Calls, Internet, usajili, kukatika kwa mawasiliano n.k)
- Maeneo gani? (Tukifahamu location, inakuwa rahisi kukuelekeza wapi uende ili upate physical assitance toka kwa vendor wetu aliye karibu nawe)
- Tatizo limeanza lini na limejirudia au kuendelea kuwa kero kwako kwa muda gani?
- Kama ni ushauri, zingatia ya juu lakini tutafurahi tukijua kwanini unapendekeza unachopendekeza
- Kama ni pongezi, zingatia ya juu na tungependa pia upendekeze lipi tufanye kuzidi kuiboresha huduma kwako.

Karibu

Vodacom Tanzania

Tatizo lipo kwa nini kila nikinunua vocha ya jero, huwa mnanikata shs. 100?
 
Vodacom ni Wezi kila nikiweka vocha wananiibia na Jana nimewatest tena kwa kuweka vocha wameiba.Wezi hawa Vodacom
 
Mimi ombi langu ni kwamba nashauri muweke kifurushi cha wewk kwa wanafunzi wa vyuo kama kilivyo cha siku KIFURUSHI CHA WEEK KWA WANACHUO AU VYUONI
 
Khaa si muache kuchangia hamuoni tunajichoresha tu, mi niliamua kuwapotezea tangu march 2013 walipo anza uduwanzi
 
"Usipoteze MB zilizobaki muda wa kifurushi unapoisha. Nunua kifurushi cha Intaneti kama cha awali muda wowote kabla ya kuisha utumie vyote pamoja hadi kipya kitapoisha ""~ Vodacom TZ

Wateja wa vodacom kweli kazi mnayo
 
Kama niliibiwa simu na nika renew simcard, wakati nikisubiria akaunti yangu ya M pesa kuhuishwa ndani ya masaa 48 je ndani ya muda huo mtu anaweza akaniingizia fedha nikazikuta? Je kuna uwezekano wa kupungua kwa masaa hayo? Tumsifu Yesu Kristo.
 
voda kamtindo kakuchukua salio ikiwa mtu ajafanya mawasiliano yoyote mkaache, jana imekua mara ya pili nikiwapigia mnasema hamjapata summary ya matumizi yangu. ni hayo tu
 
voda kamtindo kakuchukua salio ikiwa mtu ajafanya mawasiliano yoyote mkaache, jana imekua mara ya pili nikiwapigia mnasema hamjapata summary ya matumizi yangu. ni hayo tu

Na mara zote wanasema hivyo. Hawa jamaa ningekuwa na nyenzo imara ningeanza kuangusha minara yao mmoja baada ya mwingine maana wanaiba kwa makusudi na still ukiwapigia wanajifanya kujua zaidi yako.
 
Juzi nimenunua 3000 kupitia sim banking ya crdb na nikapata txt ya benki kwamba transaction imefanyika. Lakini hadi leo voda hawajaingiza hiyo hela kwenye account yangu. Nyinyi ni wezi, majambazi. Mtu anapofikia mafanikio ya juu,, kuporomoka huwa kunamsubiri. Kazi ni kwenu
 
Ni kiasi gani mmefaidika na wizi wa salio mnaloiba kwa watanzania wanaponunua vocha na kuchelewa kuunga bando?
 
Sasa nimehamia airtel na Tigo....yaani nyie wezi kweli kila kukicha mnaongeza gharama ....nusu ya mshahara wangu niwafanyie nyie ...ebo kwendeni huko.....
Tutahama tu eehee hatuna namna nyingine . eti mnatupa mb8 ...mb8 za nini sasa...apps zikijiapdate hamna kitu....kwa herini
 
Back
Top Bottom