Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Kuna wizi mkubwa kwa fedha za salio za wateja unaoendelea sasa hivi katika mtandao wa Vodacom.
Kwa vile hili si jungu bali ukweli nimisha report wizi huo katika kitengo cha malalamiko TCRA kwa hatua zaidi.

Nimeweka salio la Tsha 10,000 mchana wa leo kwa Mpesa ref Y23SY687 na baada ya muda mfupi nikakuta salio langu la maongezi ni sifuri.

Nikanunua vocha na kutumiwa tshs 10,000 na hela yote imekatwa tena.

Wateja wa Vodacom jihadharini, kuna mwizi kaingia mtandaoni Vodacom

UPDATE
=====
VODACOM wamefanya ustaarabu wa kunipigia baada ya kuona detail ya transaction hapo juu, na kuiona kwenye mtandao wa Jamiiforums.
Kimsingi wameapologise kwa mtafaruku uliotokea lakini wamenieleza nifike ofisini kwao kuona aian ya simu ninyotumia isije ikawa data apps ziko wazi.
Na kweli baada ya maongezi ya kuchunguza, mobile data setting ilikuwa ON, na mimeizima sasa.

Hata hivyo ni vema nitaenda kupata maelezo ya kuyeyuka kwa salio langu , karibu 20,000, kwa siku moja.
Wanabodi mtajulishwa inawezekana kuna wenye tatizo kama langu.

Bado ni wezi tu! Mimi nimejiunga na chekatime, hela wamekata na huduma sijapata! Na eti wakasema nitajulishwa kwa sms hakuna cha sms wala nini na hela yangu inaniuma sana!
 
Ni wazi vodacom ni wezi wa siku nyingi huiba salio na kusingizia kuwa umetumia simu vibaya mara umemuachia mtu au ameisahau mtu akachota salio mara ulijiunga na kitu gani sijui ndicho kinatumia pesa yako kwa kifupi vodacom haifai . Mimi nimeshaachana nayo napeta tu na TIGO na AIRTELL
 
Unajiunga ktk promosheni zao, wanakuambia piga namba fulani kisha aidha ujiunge na cheka time au internate masaa 24, unaambiwa subiri ujumbe mfupi utajibiwa. Unasubiri weee! Hakuna kitu, ukiangalia salio limekatwa! Na hakuna huduma hiyo wala nini! Ni kwa nini hamtuhurumii wateja wenu?

Habari,tutumie namba ya simu PM tafadhali.
 
Vodacom wamekithiri ktk wizi...

1. Nilijiunga na kifushi cha Cheka, 7000 kwa wiki... Kesho yake kuangalia kifurushi kimekwisha.... Wakati sikutumia sana.

2. Ktk bango lao la kutoa na kutuma pesa kwa Mpesa wameandika kuwa, kutuma fedha kwa wateja wasiosajiliwa kutoka 400,000 mpaka 499,999 wanatoza 7000... Wiki iliyopita nilituma 490,000 wakanikata 7800.. Ikiwa ni ziada ya 800.

3. Kutuma pesa kwa wateja wasiosajiliwa, kutoka 20,000 mpaka 49,999 wanatoza 1,600... Nilituma 20,000 wakanitoza 1,800... Ikiwa ni ziada ya 200.

.

Habari,tutumie namba ya simu PM kwa mawasiliano zaidi.
 
Hawa voda ni MATAPELI walinidanganya kwa sms nijiunge dk 60 kwa Sh 200 nilipojiunga nilipipiga simu ya kwanza na ya pili hazikua na majibu, mara ya tatu nilijibiwa kuwa sina salio .

Nikaamua kuishiana nao kimya kimya sasa nipo kwenye mitandao wanayojua kusoma hali ya soko.
 
Hahahahahah me sina ham nao kubadili line naona zengwe basi wanantia mawazo ila ikifika january ntachukua maamuz magumu insha'allah!
Voda si wezi bali wanyang'anyi
 
Nilikuwa natumia voda kwa net. cha kushangaza nanunua bando na pesa inakatwa afu service sipati. hao customer care kuwapata ni mziki mnene nikaamua kujiweka mbali nao.

mmmh mkuu umezungumzia mambo ya net nikakumbuka, hawa jamaa wamekuwa wezi kuliko hata tanesco, nimefikisha sii chini ya mara 4 nanunua bando 100mb, lkn hata dakika 2 haimalizi net inakata ukiangalia salio hola, SASA sijui ndo fedha za kampeni zinasakwa? na kwa vile ule mpango wao wa kulipia kila mwezi umeingia zwengwe ndo kabisaaaa tuaibiwa kwa nguvu.
 
Voda ni wezi sana mimi waliniibia nikawapigia wakaniambia wamegundua kuna tatizo ni wapigie baada ya masaa matatu ,nilivyowapigia wakaniambia siruhusiwi kupiga huduma kwa wateja mpaka January 15 nilichofanya nikanunua line ya airtel nikacopy majina cjui hata nilikoitupa line ya Voda. I hate this Voda for sure.
 
mh.....hapa bado sijaelewa huu uwizi. kama ndivyo kwa kweli inabidi wapelekwe mahakamani
 
ni kweli hata mimi imenitokea mara kadhaa na juhudi za kuongea na customer care hazikuzaa matunda sasa nimeachana nao.

kama mimi mkuu. Imenitokea mara mbili lakini castomer care kimeo.
 
Vodacom wamekithiri ktk wizi...

1. Nilijiunga na kifushi cha Cheka, 7000 kwa wiki... Kesho yake kuangalia kifurushi kimekwisha.... Wakati sikutumia sana.

2. Ktk bango lao la kutoa na kutuma pesa kwa Mpesa wameandika kuwa, kutuma fedha kwa wateja wasiosajiliwa kutoka 400,000 mpaka 499,999 wanatoza 7000... Wiki iliyopita nilituma 490,000 wakanikata 7800.. Ikiwa ni ziada ya 800.

3. Kutuma pesa kwa wateja wasiosajiliwa, kutoka 20,000 mpaka 49,999 wanatoza 1,600... Nilituma 20,000 wakanitoza 1,800... Ikiwa ni ziada ya 200.

.

Pole sana, kama ungekuwa na line ya baba lao ungeongeza shs 3000 tu halafu ungepiga simu mwezi mzima kwa 10,000 internet ya kumwaga na sms zisizohesbika

Hawa akina dogo (voda na tigo) wezi wanataka kula bila jasho, wasamehe bure bado wanakua they have to eat excessively so that they grow big
 
Hili jambo lilinitoke hata mimi majuzi tuu, kila nikitaka kujiunga kifurusha ina kataa lakini salio lina katwa hadi likaisha. nili kerwa sana siku hiyo lakini niliwapigia tuka yamaliza na customer care.

Vodacom ni wasikivu sana.
 
Habari,tutumie namba ya simu PM kwa mawasiliano zaidi.
Mkuu naona kama kawaida yenu mnaomba namba, kama fb vile! Hapa ni JF ni muhimu utoe ufafanuzi wa kutosha mnaana haya matatizo ni kwa watumiaji karibia wote, sasa wewe unaposema pm namba unawasaidiaje wale wasioingia JF!!
 
Mkuu naona kama kawaida yenu mnaomba namba, kama fb vile! Hapa ni JF ni muhimu utoe ufafanuzi wa kutosha mnaana haya matatizo ni kwa watumiaji karibia wote, sasa wewe unaposema pm namba unawasaidiaje wale wasioingia JF!!

umemkimbiza customer care wa watu....teh teh teh..
 
Mtandao wao mbaya sana saiv,mimi nilikua najiunga na Cheka za 500 cha kushangaza,data zinakaa muda mfupi wananiletea ujumbe eti zimeisha bila hata kuzitumia.

Niliwapigia nikapewa majibu hovyo hovyo kabsa,nilipowapigia tena eti nikaambiwa huduma ya bure nimefungiwa mpaka january!

Nilichokifanya nikopy majina kwenye simu na kuivunja iyo line,staki tena Voda nimesharudi nyumban Airtel coz nilihamiaga voda mwaka 2010 bada ya kukuta wanafunzi wengi chuon wanavoda na tiGO bt saiv nimeshamaliza chuo na Airtel ndo mpango mzima.
Voda ni wezi tu!
 
Hiyo iko wazi kbs kuwa vodacom wana matatizo makubwa sana hata ya usikivu wakati unaongea. Hili la wizi limekithili kwani unawekewa wimbo na kukatwa bila ya wewe kuomba wimbo husika. Huu sio mtandao kabisa jamani.
 
Back
Top Bottom