Vodacom Tanzania yadaiwa kutowalipa mawakala wake wa huduma ya kifedha(M-Pesa) kamisheni zao

Watanzania sisi tumejaliwa kulalamika... Mbona vodacom ndio mtandao unaoongoza kwa commission nzuri Kuliko wengine?... Bado kuna ofa kibao kila siku unapata 2500...1900 n. K.. Vodacom huwa wanalipa saa sita usiku siku ya mwisho wa mwezi... Sasa wamechelewa kidogo tu unalia... Mbona tigo wanachelewesha hulii... Airtel ndio kabisaa hawalipi kabisa siku nyingine mbona hulii... Wapongeze vodacom kwa kuwa na huduma bora bana.. Wewe kama kweli ni wakala umeelewa
 
Matusi tena chief? Mi pia nabiashara hizi zaidi ya moja huna la kunidanganya. Wadanganye wasojua.
Na ndo maana upo hapa kulalamika..kumbe nabishana na mtu mwenye uelewa mdogo sana! Unajua maana ya neno mjinga!?? Ujinga ni ignorance..ujinga ni kutojua na wewe kweli hujui lkn hata kujifunza hutaki! Hii ni comment yangu ya mwisho,sitaku-quat tena. Me nilikurahisishia km upo dar,njoo ofisini na ntakupa elf 10 km nauli uje uone watu tunavyofanyakazi. Hiyo nyumba unaiona kwenye avatar yangu imetoka kwenye biashara hiyo. Hiyo ni nyumba ya vyumba 3 na imekamilika kila kitu na nimepangisha kwa laki 4 na nusu nyumba nzima..wewe kaa kulalamika!!
 
Mkuu na usirudi tena ikiwezekana ufie huko huko kabisa. Kila mtu akiweka anachomiliki kwenye avatar saver haitatosha Muhaya wewe. Unatishia kutokujibu ? Acha nyodo Dada. Hiyo elfu wanunulie vitabu wadogo zako
 
Mkuu tufahamishe mtu akiweka laki mbili wakala anapata commission sh ngapi? Na je kutoa laki mbili wakala anapata commission ya kiasi gani pia?
 
Miaka ya Nyuma hii biashara ilikuwa nzur lakin hawa jamaa wa mitandao waka punguza Commision

Tena kama Voda ndio waseng** zaidi.. Mtu unalipwa na cent yaa .85 ni ufala basi
 
Acha kuingiza watu mkenge kwa maslahi yako. Hiyo ni biashara ya kitumwa kabisa. Unaweza niambia kazi ya wakala mkuu kwa wakala mdogo ni ipi ? Na kwa mini kamisheni yake nikubwa kuliko ya wakala mdogo ambae ndie anatafuta wateja na kurisk pesa zake?
Natamani nitume kamisheni zangu Mzione
 
Hii biashara kwanza inabidi uwe wakala wa mitandao yote na pia benki kubwa zote......lakini pia uichanganye na biashara nyingine kama duka au steshenari
 
Utakuwa chuma ulete wewe siyo bure!
 
Biashara ya kibumbavu Sana. Voda ukipata kamisheni ya 200,000 wanakukata kodi ya 19,819.9. Unabaki Na 180,180.1
 
Utakuwa chuma ulete wewe siyo bure!


Hivi unapataje kamisheni ya mil 3 kwa mzunguko wa laki 6 tu?

Hata kama kuna wateja wengi unagawanyaje laki 6 kwa wateja hao wote?

Je wakitoa utaenda kwanza kutoa cash bank ndo uwape?

Labda ukiwa na mtaji wa milion 15 unaweza kupata kamisheni ya mil 3 tena ukichanganya kamisheni za line zote

Lakin laki 6 utengeneze mil 3 udanganyifu wa kiwango cha lami.....
 
Uongo per se huu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…