Vodacom, tiGO wapandisha tena bei za vifurushi vya Internet. Nape unafanya kazi gani?

Tanzania hatuna viongozi, nchi inaenda tu kama kipofu
 
Hii mizinguonimeanza jana kwenye tigo kwa 500 tsh ulikuwa unapata 280mb ila sasa unapata 245Mb.
Hawawez kushusha bila kupata authority kutoka kwa mamlaka ,wanadai uendeshaji una gharama kubwa.
 
MTATUBUU😅😅😅
 
Unaipataje hiyo
 
Sijawahi kuamini utendaji wake. Alikuja na mbwembwe kuhusu channels za ndani kuonyeshwa. Hakuna Cha maana kilichofanyika. Dstv wanakata hadi TBC!

Ubaya nyuma yake yupo Rostam Aziz.....na nape hana la kumfanya.
 
Hata hao ni wezi tu, nilikuwa natumia cha 15k kwa mwezi ambapo wlijuwa wananipa GB 8 na dk.800 mitandao yote! Mpaka nimeachana na Tigo post paid kwa bei hiyo hiyo walikuwa wananipa Gb 7
Una uhakika ilitakiwa kuwa 8GB?!

Wana namna mzuri sana ya kuiba... kwa mfano, wanaweza kusema 8GB na kweli baada ya kupewa ikasoma 8GB lakini ujazo wake halisi usiwe 8GB. Lakini sidhani kama wanaweza kuwa stupid waseme 8GB halafu wakupe 7GB jambo ambalo yeyote ataona kwamba HUU NI WIZI!

Anyway, I don't know lakini nikiangalia vipeperushi ambavyo nilipewa wakati najiunga, naona kifurushi cha 15K wanatoa 7.5GB na dakika 875.
 
Unaipataje hiyo
xx
Nipe utaratibu kidogo boss..
Mkuu hii ni lazima niende kwenye ofisi za tigo ?
Unaipataje hiyo
Mie nilijaza fomu yao online kisha wakanipigia. Muhimu unatakiwa kuwa na Kitambulisho cha NIDA, and of course, kwavile ni Business Pack, watakuuliza suala la leseni.

Yeyote anayetaka namba ya simu ya Mkuu wa Idara, let me know.

NOTE: Binafsi nilijiunga miezi kadhaa iliyopita ingawaje kwa sasa najaribu kutafuta alternative kwa sababu speed yake sio rafiki sana kwangu!

Hata hivyo, sio kwamba ni slow sana bali kuna mambo kwa upande wangu yanahitaji speed ya sifa na ndo maana nahangaika kupata Fibre!

Sasa kwavile nili-join zamani kidogo, huenda hizo packages zikawa zimebadilika though hadi last month, bill ambayo nililetewa ni the same, na sasa nasubiri mwezi huu kuona kama ipo vile vile manake hii speed ya kubadili data packs imekuwa sio ya kawaida
 
Waziri mwenye zamana ni mtu wa porojo wote hao wanakula meza moja na makampuni hakuna mtetezi jipangeni
 
Hayo ni maelekezo yake, wanapandisha kwa stage,lengo ni gb 1 elfu iwe elf 2 mpaka elfu 3
 
Kwa kuwa hawajaguswa wakubwa na familia zao ndiyo maana husikii maumivu ya mishale na kelele za watu wakipiga kelele ..." 🔊 mwingine huo kwepa!", Yaani Magufuri angesimangwa hapa mpaka headache.

But kwa sababu ni huku chini ndiyo mnachapwa sawasawa never listen any thing up there.

Tulieni sindano iwaingie mtajua nurse anafaa au akawe doctor wa mifugo.
 
Kabla ya kulalamika unaijua bei elekezi kwa kila Mb 1?
 
Balaa balaani, wao wanapewa za bure za mtandao wao uleee wala hawa feel kama kuna ugumu wa maisha katika nchi hiyo, POleni sana
 
Bila wateja kuja jufanya maamuzi.magumu hakuna kitakacho badilika na walisha jua mtalalamika siku 2 then mtanyamaza, watapandisha kila mwezi, na hakuna mnaweza wafanya
 
Airtel nao wamepandizha bei ya vifurushi.

Inamaana haya makampuni awamu huu yanajipandizhia bei wakijihamulia wao wenyewe, hakuna chombo cha kuwasimamia.

Airtel kwa Shilingi 5 000 kwa siku 7 ulikuwa unapata 2.7GB sasa wanakupa 2.4GB.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…