Volkswagen yafikiria kufunga viwanda vyake nchini Ujerumani, moja ya sababu ni ushindani kutoka China

Volkswagen yafikiria kufunga viwanda vyake nchini Ujerumani, moja ya sababu ni ushindani kutoka China

Xi Jinping

JF-Expert Member
Joined
Jun 14, 2023
Posts
3,651
Reaction score
11,548
Volkswagen inafikiria iwapo itafunga viwanda nchini Ujerumani kwa mara ya kwanza katika historia yake ya miaka 87 huku ikielekea kuongeza upunguzaji wa gharama huku kukiwa na ushindani unaoongezeka kutoka kwa watengenezaji magari ya umeme nchini China.
–London (CNN)

Mapema wiki hii CNN iliripoti taarifa hiyo kuhusu Volkswagen (VW) moja ya kampuni kubwa duniani ya kutengeneza magari ya nchini Ujerumani.

Tangu mwaka jana mwanzoni VW imekuwa ikipambana kupunguza gharama za uzalishaji bila mafanikio.

Wakati wakipambana na hilo imekutana tena na changamoto nyingine, inazidi kupoteza soko lake kubwa zaidi la magari la China kutokana na ushindani mkali kutoka kwa kampuni za kutengeneza magari za nchini China kama vile BYD.

Pia BYD imekuwa ikizipa ushindani mkali kampuni za Ulaya kutia ndani VW kwenye soko la dunia la magari ya umeme.

Changamoto haiko tu kwa VW bali pia sekta ya viwanda vya magari barani Ulaya kwa ujumla.

"Sekta ya utengenezaji magari barani Ulaya iko katika hali ngumu sana."
–Oliver Blume (Volkswagen C.E.O
)
Kuna sababu gani za kudorora kwa sekta ya viwanda vya magari barani Ulaya?

"Mazingira ya kiuchumi yamekuwa magumu zaidi, na washindani wapya wanaingia kwenye soko la Ulaya. Ujerumani haswa kama eneo la utengenezaji iko nyuma zaidi katika suala la ushindani."
–Oliver Blume (Volkswagen C.E.O)

Mipango ya VW kupunguza gharama itakabiliwa na upinzani mkubwa kutoka kwa wawakilishi wa wafanyakazi na vyama vya wafanyakazi. Moja ya chama cha wafanyakazi chenye nguvu zaidi nchini Ujerumani kimeilaumu VW kwa usimamizi mbovu wa kampuni hiyo na kuapa kupigana kulinda kazi.

Tulitegemea mambo kama haya yaitokee Urusi ambayo Ujerumani na washirika wenzake wameiwekea vikwazo vya kiuchumi.
 
Volkswagen inafikiria iwapo itafunga viwanda nchini Ujerumani kwa mara ya kwanza katika historia yake ya miaka 87 huku ikielekea kuongeza upunguzaji wa gharama huku kukiwa na ushindani unaoongezeka kutoka kwa watengenezaji magari ya umeme nchini China.
–London (CNN)

Mapema wiki hii CNN iliripoti taarifa hiyo kuhusu Volkswagen (VW) moja ya kampuni kubwa duniani ya kutengeneza magari ya nchini Ujerumani.

Tangu mwaka jana mwanzoni VW imekuwa ikipambana kupunguza gharama za uzalishaji bila mafanikio.

Wakati wakipambana na hilo imekutana tena na changamoto nyingine, inazidi kupoteza soko lake kubwa zaidi la magari la China kutokana na ushindani mkali kutoka kwa kampuni za kutengeneza magari za nchini China kama vile BYD.

Pia BYD imekuwa ikizipa ushindani mkali kampuni za Ulaya kutia ndani VW kwenye soko la dunia la magari ya umeme.

Changamoto haiko tu kwa VW bali pia sekta ya viwanda vya magari barani Ulaya kwa ujumla.

"Sekta ya utengenezaji magari barani Ulaya ya iko katika hali ngumu sana."
–Oliver Blume (Volkswagen C.E.O
)
Kuna sababu gani za kudorora kwa sekta ya viwanda vya magari barani Ulaya?

"Mazingira ya kiuchumi yamekuwa magumu zaidi, na washindani wapya wanaingia kwenye soko la Ulaya. Ujerumani haswa kama eneo la utengenezaji iko nyuma zaidi katika suala la ushindani."
–Oliver Blume (Volkswagen C.E.O)

Mipango ya VW kupunguza gharama itakabiliwa na upinzani mkubwa kutoka kwa wawakilishi wa wafanyikazi na vyama vya wafanyakazi. Moja ya chama cha wafanyakazi chenye nguvu zaidi nchini Ujerumani kimeilaumu VW kwa usimamizi mbovu wa kampuni hiyo na kuapa kupigana kulinda kazi.

Tulitegemea mambo kama haya yaitokee Urusi ambayo Ujerumani na washirika wenzake wameiwekea vikwazo vya kiuchumi.
Ni suala la muda tu kwa severe global financial crisis inayokuja na next severe pandemic hata mchina atanyooka
 
Ford nao naona karibuni watafunga plant yao ya China, biashara yao imeshakuwa ngumu ushindani wa brands za ndani ya China umekuwa mkali
Mitsubishi alishafunga plant nchini China na kusepa mazima

Nissan nao mwaka huu wamekusanya virago

Toyota naye anapambana kibishi anapumulia mipira acha tuone

Moto wanaopelekewa na China-based brands sio poa
 
Umeona hapo mr C.E.O analia ushindani wanaokabili kwa soko lao muhimu la China

It means Wachina wana purchasing power kubwa. Utasemaje uchumi wa China hauko stable?

Kwa nini asilalamike hivyo kuhusu soko la Ulaya na Marekani?


EU na US wakiamua kumpa nafasi ya China apewe Mexico mtashangaa wote hapa jinsi China itanyooka.

Mexico wapo vizuri pia tena sana halafu mshahara wao kwa wastani ni mdogo mara 3 ya China.
 
EU na US wakiamua kumpa nafasi ya China apewe Mexico mtashangaa wote hapa jinsi China itanyooka.

Mexico wapo vizuri pia tena sana halafu mshahara wao kwa wastani ni mdogo mara 3 ya China.
Kwa nini wampe nafasi Mexico wakati kwao mambo magumu? Utaanzaje kupajenga kwa jirani na kwako kunabomoka

Kwanza hapo Mexico Mchina kawekeza sana, makampuni mengi ya China yamewekeza Mexico

Siku hizi hata baadhi ya bidhaa za China zinaingia Marekani kupitia Mexico
 
EU na US wakiamua kumpa nafasi ya China apewe Mexico mtashangaa wote hapa jinsi China itanyooka.

Mexico wapo vizuri pia tena sana halafu mshahara wao kwa wastani ni mdogo mara 3 ya China.


Mexico hakuna skilled cheap labour

Pia population ya mexico ni ndogo sana kuweza kufanya productions ya kutosheleza soko.

China kuna watu zaidi ya bilioni
 
Mitsubishi alishafunga plant nchini China na kusepa mazima

Nissan nao mwaka huu wamekusanya virago

Toyota naye anapambana kibishi anapumulia mipira acha tuone

Moto wanaopelekewa na China-based brands sio poa
Ninachopendea Mchina hakufukuzi

Wewe mwenyewe ukiona moto umekuwa mkali unafunga unasepa.

Umenikumbusha Samsung nao walifunga plant China baada ya kuona ushindani mkali kutoka Xiaomi, Vivo, Huawei, Oppo
 
Kwa nini wampe nafasi Mexico wakati kwao mambo magumu? Utaanzaje kupajenga kwa jirani na kwako kunabomoka

Kwanza hapo Mexico Mchina kawekeza sana, makampuni mengi ya China yamewekeza Mexico

Siku hizi hata baadhi ya bidhaa za China zinaingia Marekani kupitia Mexico
2023 Mexico imeongoza duniani kama topr trade partner wa US ku import in US.

US amepandisha tariffs kwa bidhaa zinazotoka China.
Hivi sasa imefikia hatua baadhi ya kampuni za Chinese wanaitumia Mexico kama route kupeleka vitu US li kukwepa tariffs.

Mambo bado ya moto.
 
Hivi sasa imefikia hatua baadhi ya kampuni za Chinese wanaitumia Mexico kama route kupeleka vitu US li kukwepa tariffs
Mbinu za kibiashara. Marekani asiponunua bidhaa za China kupitia Mexico basi atanunua components za Kichina kupitia Mexico kwenda kutengeneza bidhaa ndivyo mambo yanaenda. The game is the game
 
Back
Top Bottom