Volkswagen yafikiria kufunga viwanda vyake nchini Ujerumani, moja ya sababu ni ushindani kutoka China

Volkswagen yafikiria kufunga viwanda vyake nchini Ujerumani, moja ya sababu ni ushindani kutoka China

Ninachopendea Mchina hakufukuzi

Wewe mwenyewe ukiona moto umekuwa mkali unafunga unasepa.

Umenikumbusha Samsung nao walifunga plant China baada ya kuona ushindani mkali kutoka Xiaomi, Vivo, Huawei, Oppo
Sijajua sana kuhusu future ya iPhone nchini China ripoti ya karibuni inaonyesha imepigwa gap na kampuni za ndani

Kutoka kuwa ya kwanza kwenye soko la China mwaka jana mpaka kufikia kuwa ya 4 mwaka huu

Vivo, Huawei, Honor, iPhone, Xiaomi, Oppo
 
Tulitegemea mambo kama haya yaitokee Urusi ambayo Ujerumani na washirika wenzake wameiwekea vikwazo vya kiuchumi.
20240905_064248.jpg
 
Maneno soko huria siku hizi kwa Marekani na Ulaya siyo ya kweli hawaishi kwenye hayo maneno
Walilazimisha nchi zetu zinazoendelea kuingia katika soko huria wakijua kwamba hakuna wa wakuwazidi katika uzalishaji wa bidhaa za viwandani.
Nakumbuka kwenye hotuba yake moja nyerere alifananisha na boxing kwa mtu ambaye hana utaalam akapambane na Mike iron
 
Volkswagen inafikiria iwapo itafunga viwanda nchini Ujerumani kwa mara ya kwanza katika historia yake ya miaka 87 huku ikielekea kuongeza upunguzaji wa gharama huku kukiwa na ushindani unaoongezeka kutoka kwa watengenezaji magari ya umeme nchini China.
–London (CNN)

Mapema wiki hii CNN iliripoti taarifa hiyo kuhusu Volkswagen (VW) moja ya kampuni kubwa duniani ya kutengeneza magari ya nchini Ujerumani.

Tangu mwaka jana mwanzoni VW imekuwa ikipambana kupunguza gharama za uzalishaji bila mafanikio.

Wakati wakipambana na hilo imekutana tena na changamoto nyingine, inazidi kupoteza soko lake kubwa zaidi la magari la China kutokana na ushindani mkali kutoka kwa kampuni za kutengeneza magari za nchini China kama vile BYD.

Pia BYD imekuwa ikizipa ushindani mkali kampuni za Ulaya kutia ndani VW kwenye soko la dunia la magari ya umeme.

Changamoto haiko tu kwa VW bali pia sekta ya viwanda vya magari barani Ulaya kwa ujumla.

"Sekta ya utengenezaji magari barani Ulaya iko katika hali ngumu sana."
–Oliver Blume (Volkswagen C.E.O
)
Kuna sababu gani za kudorora kwa sekta ya viwanda vya magari barani Ulaya?

"Mazingira ya kiuchumi yamekuwa magumu zaidi, na washindani wapya wanaingia kwenye soko la Ulaya. Ujerumani haswa kama eneo la utengenezaji iko nyuma zaidi katika suala la ushindani."
–Oliver Blume (Volkswagen C.E.O)

Mipango ya VW kupunguza gharama itakabiliwa na upinzani mkubwa kutoka kwa wawakilishi wa wafanyakazi na vyama vya wafanyakazi. Moja ya chama cha wafanyakazi chenye nguvu zaidi nchini Ujerumani kimeilaumu VW kwa usimamizi mbovu wa kampuni hiyo na kuapa kupigana kulinda kazi.

Tulitegemea mambo kama haya yaitokee Urusi ambayo Ujerumani na washirika wenzake wameiwekea vikwazo vya kiuchumi.
Urusi wanatengeneza magari gani
 
Walilazimisha nchi zetu zinazoendelea kuingia katika soko huria wakijua kwamba hakuna wa wakuwazidi katika uzalishaji wa bidhaa za viwandani.
Nakumbuka kwenye hotuba yake moja nyerere alifananisha na boxing kwa mtu ambaye hana utaalam akapambane na Mike iron
Walikuwa na nguvu ya kuhubiri kuhusu soko huria wakati hawana ushindani

Imagine Marekani chini ya utawala wa Biden imeiwekea China tariffs kwenye EVs kufikia 100%

Hii ni kuonyesha wameshindwa ku-compete na China
 
Nilijua hili lingetokea tu muda si mrefu. Biashara ya viwanda vya Ujerumani iliweza kushindana sokoni kutokana na kupata nishati ya bei ya kishkaji kutoka Urusi, sasa leo kaingia kiboya kwenye vikwazo dhidi ya Urusi na Mchina anazalisha magari bora kwa gharama nafuu lazima Ujerumani alambe sakafu.
 
Point haikuwa kulenga viwanda vya magari tu bali uchumi kwa ujumla. Ilitakiwa kwa sasa tuone -ve impacts za vikwazo ilivyowekewa Russia

Ila cha kusahangaza licha ya vikwazo ni kwamba uchumi wa Russia unakua kuliko mataifa yote ya Ulaya
Russia inauza gas na wateja wake ni nchi za Ulaya.
Halafu vikwazo huwa haviathiri uchumi labda nchi iwekewe vikwazo na dunia nzima
Angalia nchi kama Iran, Noth Korea
 
Nilijua hili lingetokea tu muda si mrefu. Biashara ya viwanda vya Ujerumani iliweza kushindana sokoni kutokana na kupata nishati ya bei ya kishkaji kutoka Urusi, sasa leo kaingia kiboya kwenye vikwazo dhidi ya Urusi na Mchina anazalisha magari bora kwa gharama nafuu lazima Ujerumani alambe sakafu.
Umesema vyema, na hili limeumiza sekta ya viwanda vya Ujerumani kwa ujumla
 
Volkswagen inafikiria iwapo itafunga viwanda nchini Ujerumani kwa mara ya kwanza katika historia yake ya miaka 87 huku ikielekea kuongeza upunguzaji wa gharama huku kukiwa na ushindani unaoongezeka kutoka kwa watengenezaji magari ya umeme nchini China.
–London (CNN)

Mapema wiki hii CNN iliripoti taarifa hiyo kuhusu Volkswagen (VW) moja ya kampuni kubwa duniani ya kutengeneza magari ya nchini Ujerumani.

Tangu mwaka jana mwanzoni VW imekuwa ikipambana kupunguza gharama za uzalishaji bila mafanikio.

Wakati wakipambana na hilo imekutana tena na changamoto nyingine, inazidi kupoteza soko lake kubwa zaidi la magari la China kutokana na ushindani mkali kutoka kwa kampuni za kutengeneza magari za nchini China kama vile BYD.

Pia BYD imekuwa ikizipa ushindani mkali kampuni za Ulaya kutia ndani VW kwenye soko la dunia la magari ya umeme.

Changamoto haiko tu kwa VW bali pia sekta ya viwanda vya magari barani Ulaya kwa ujumla.

"Sekta ya utengenezaji magari barani Ulaya iko katika hali ngumu sana."
–Oliver Blume (Volkswagen C.E.O
)
Kuna sababu gani za kudorora kwa sekta ya viwanda vya magari barani Ulaya?

"Mazingira ya kiuchumi yamekuwa magumu zaidi, na washindani wapya wanaingia kwenye soko la Ulaya. Ujerumani haswa kama eneo la utengenezaji iko nyuma zaidi katika suala la ushindani."
–Oliver Blume (Volkswagen C.E.O)

Mipango ya VW kupunguza gharama itakabiliwa na upinzani mkubwa kutoka kwa wawakilishi wa wafanyakazi na vyama vya wafanyakazi. Moja ya chama cha wafanyakazi chenye nguvu zaidi nchini Ujerumani kimeilaumu VW kwa usimamizi mbovu wa kampuni hiyo na kuapa kupigana kulinda kazi.

Tulitegemea mambo kama haya yaitokee Urusi ambayo Ujerumani na washirika wenzake wameiwekea vikwazo vya kiuchumi.
Kila chenye Mwanzo 😁😁
 
Sijajua sana kuhusu future ya iPhone nchini China ripoti ya karibuni inaonyesha imepigwa gap na kampuni za ndani

Kutoka kuwa ya kwanza kwenye soko la China mwaka jana mpaka kufikia kuwa ya 4 mwaka huu

Vivo, Huawei, Honor, iPhone, Xiaomi, Oppo
Nadhani hata ile issue ya kuzuia watumishi kutumia iphone katika ofisi za umma inaweza kuwa mojawapo ya sababu.
 
Back
Top Bottom