VPL: Tanzania Prison vs Simba & Yanga vs Polisi Tanzania

VPL: Tanzania Prison vs Simba & Yanga vs Polisi Tanzania

Yeye ni binadamu hivyo hawezi kukamilika kwa kila kipengele. Ukiangalia huo uzembe ambao ni makosa ya Mara kwa mara yanayozungumziwa ni kufanya timing ya mpira vibaya (kutoka). Haya yanaongozwa na hesabu zake za akili yake kichwani. Tukija katika namba, idadi ya michomo ya wazi aliyofanikiwa kuibeba Simba kupata matokeo ni kubwa kuliko idadi ya makosa yake binafsi aliyoyafanya na kuigharimu timu.
Hakuna kipa mzuri duniani ambaye hana mapungufu ya kibinadamu, makipa wote wanafungwa hata awe bora kiasi gani.
points tulizopoteza zote ligi kuu makosa yametoka kwake ni hatari kwa kipa ,kama leo pale kulikuwa na mabeki wawili na wameshamkabili jamaa kulikuwa na haja gani ye kutoka golini kuwahi mpira kwenye vichwa vya mabeki
 
Ukizoea biriani na soda alafu siku moja ukala ugali na mlenda unaweza kutapika..
 
Huwezi usikia leo best.
Hivi kumbe ni wewe best, tangu ile siku umenikwot nilikuwa bado naona mapicha picha ujue. Kuuliza naogopa, kukaa kimya nashindwa kujizuia. Hatimaye sasa nimdhaniaje kumbe ndiye[emoji122][emoji122]
 
magoli ambayo huwa anafungwa ni ya kizembe utadhani kahongwa na kampuni za kubet ,lakini hiyo michomo aliyofanya unaona hapa kafanya kazi ,ila haya magoli ya kizembe si bure kuna kitu anakijua
Lile goli siyo uzembe wa kipa bali uzembe wa walinzi. Jamaa karuka pamoja na babu onyango huku kuliwa na mabeki wengine 2 wa simba. Halafu kile kichwa cha moto sana huwezi mlaumu golikipa
 
Generalisation ya namna hii ni mbaya sana.... dk 90 zote Simba haikupata bao nayo hiyo tu blame hilo goli moja... Simba ni timu kubwa, imeshatoka kwenye visingizio vya lawama. Sven ameshajibu kila kitu.. Football 1 + 1 sio lazima iwe 2. Simba tumepoteza tunajipanga, wachezaji wetu wote ni mashujaa...wamepambana tupo pamoja nao.
 
Sven Vandoebroek ni bonge la kocha.....tumpe nafasi ameelezea vizuri sana mechi hii..! Kuna Kocha mmoja wa zamani wa upande pili matokeo kama haya alikuwa anajibu 'tumeonewa na REFA' halafu mashabiki wanabeba wimbo wa marefa wamewaonea....mwisho wa msimu nafasi ya 3 ...wanabaki matopeni...!
 
points tulizopoteza zote ligi kuu makosa yametoka kwake ni hatari kwa kipa ,kama leo pale kulikuwa na mabeki wawili na wameshamkabili jamaa kulikuwa na haja gani ye kutoka golini kuwahi mpira kwenye vichwa vya mabeki
Usiwe mtu wa kuangalia makosa au madhaifu tu. Mara ngapi Manula amefanya save za hatari ambazo angelikuwa kipa mwingine lingehesabika ni goli. Nakumbuka mashabiki wa Simba walipiga sana kelele za lawama kwa manula baada ya mechi ya Simba na Yanga kuisha kwa sare 2-2.

Ikapelekea kuwekwa benchi Manula na nafasi yake kuchukuliwa na Kakolanya. Kakolanya kila mechi aliyodaka kashindwa kupata clean sheet, watu watupia tu magoli lakini husikii lawama zinakwenda kwake watu wanyamaza tu kimya.

Au kuanza kulaumiwa mabeki. Anarudi Manula golini Simba wakapata clean sheet. ila mechi anazofungwa Manula hakuna anayeanza kutathmini mpira kwanzia kwa beki. Goli la leo mtu anaruka kichwa mbele ya mabeke, hawasemwi wanakuja kusemwa mtu wa mwisho ambaye ni kipa kisa tu katoka. Je mabeki walikuwa sahihi?
 
Asalaleee.....Vyura mmeitana huku...mmejazana....! yaani nyuzi hizi siku za karibuni vyura huwa wanazikimbia na kudai wanatumia uzi wao Yanga Afrika kwa woga na kutojiamini. Sasa muwe mnaanzisha nyuzi na nyie ili kilinge kinoge.....mnavyokimbia sio poa,sie ni watani tu.
Mdosi bando limeisha mmeshindwa kuwanunua Prisons.. nasikia Mdosi hajachangia chama chake kwenye kampeni wanamuwinda akibugi Segerea
 
Manula apewe kalipio kali.
Tatizo sio Manula bali kocha wa makipa haiwezekani Manula awe anafungwa magoli ya aina moja na anashindwa kumrekebisha hapo ndio utaeleea kwanini Ausem aliwaponda viongozi wa simba kwani alishawaambia huyo kocha akasome aongeze ujuzi
 
Usiwe mtu wa kuangalia makosa au madhaifu tu. Mara ngapi manula amefanya save za hatari ambazo angelikuwa kipa mwingine lingehesabika ni goli. Nakumbuka mashabiki wa Simba walipiga sana kelele za lawama kwa manula baada ya mechi ya Simba na Yanga kuisha kwa sare 2-2.

Ikapelekea kuwekwa benchi Manula na nafasi yake kuchukuliwa na Kakolanya. Kakolanya kila mechi aliyodaka kashindwa kupata clean sheet, watu watupia tu magoli lakini husikii lawama zinakwenda kwake watu wanyamaza tu kimya.

Au kuanza kulaumiwa mabeki. Anarudi Manula golini Simba wakapata clean sheet. ila mechi anazofungwa Manula hakuna anayeanza kutathmini mpira kwanzia kwa beki. Goli la leo mtu anaruka kichwa mbele ya mabeke, hawasemwi wanakuja kusemwa mtu wa mwisho ambaye ni kipa kisa tu katoka. Je mabeki walikuwa sahihi?
Lile goli ni kosa la wazi la kipa ametoka bila kuangalia beki yukoje matokeo yake amewacha goli wazi labda tulaumu timu kwanini imeshindwa kufunga maana kulikuwa hakuna dalili yoyotenya timu kupata bao
 
magoli ambayo huwa anafungwa ni ya kizembe utadhani kahongwa na kampuni za kubet ,lakini hiyo michomo aliyofanya unaona hapa kafanya kazi ,ila haya magoli ya kizembe si bure kuna kitu anakijua
Mo anaendesha timu kihindi hivi anakuwaje na kocha wa makipa hana cheti
 
Duuh!! Hadi nimesikitika best.
Nilikua naomba dua Shadeeya usitokeze kwenye huu uzi maana utavunja amani na utulivu. Naona dua yangu bado haijapokelewa. Ila ipo siku na nyie mtalia machozi tena ya damu na wala haiko mbali, November 07
 
magoli ambayo huwa anafungwa ni ya kizembe utadhani kahongwa na kampuni za kubet ,lakini hiyo michomo aliyofanya unaona hapa kafanya kazi ,ila haya magoli ya kizembe si bure kuna kitu anakijua
Mchezesheni Kakolanya mwone mambo!!!
 
Yeye ni binadamu hivyo hawezi kukamilika kwa kila kipengele. Ukiangalia huo uzembe ambao ni makosa ya Mara kwa mara yanayozungumziwa ni kufanya timing ya mpira vibaya (kutoka). Haya yanaongozwa na hesabu zake za akili yake kichwani. Tukija katika namba, idadi ya michomo ya wazi aliyofanikiwa kuibeba Simba kupata matokeo ni kubwa kuliko idadi ya makosa yake binafsi aliyoyafanya na kuigharimu timu.
Hakuna kipa mzuri duniani ambaye hana mapungufu ya kibinadamu, makipa wote wanafungwa hata awe bora kiasi gani.
Degea kipa bora kabisa alipigwa 6 na Totenham, hilo hawajui. Mwacheni Manula bhana kafanya kazi nzuri mno.
 
Nilikua naomba dua Shadeeya usitokeze kwenye huu uzi maana utavunja amani na utulivu. Naona dua yangu bado haijapokelewa. Ila ipo siku na nyie mtalia machozi tena ya damu na wala haiko mbali, November 07
Hadi ifike nyie mshaumia sana. 😂😂

Alinichekesha Mtani Faru Kabula eti akasingizia yuko chimbo halafu hakuna umeme nikawa najikumbuka mie msimu uliopita. 😂😂

Ama kweli kipigo noma.
 
Back
Top Bottom