Vurugu Umbwe-Lyamungo: Miaka 12 baadae

Vurugu Umbwe-Lyamungo: Miaka 12 baadae

Ni MILAMBO sio Mirambo. TUliwapiga sana Tabora Boys. Kuna siku ilikuwa Jmosi tuliwachapa yaaani tuliwavamia kwao then Jpili tukaenda kusali Joint-Mass, Ilikuwa Mwaka 1999-2000, nilikuwa EGM Form Six
Ila kudadeki mlikuwa wakorofi sana hadi mkachoma maabara
 
Hasa hasa kwny kuchagua masterfood ndo hua wanaangalia mwenye manguvu hata kama ni zero brain
Hahaha tunarudi kwenye midahalo ya co education is better than single sex education. Sitasahau hizi balehe. Tulikaa muda mrefu sana shule. Hiyo wiki tuko mabwenini akicheka huyu anapokea huyu. Yaan hamna sabaabu. Watu mabwenini ni vicheko tu aisee.. nilikua kiongozi wa chakula. Niliona kwa macho yangu mafuta ya taa yakimiminiwa kwenye makande[emoji23][emoji23][emoji706]
Nilichofanya niliagiza kiepe nje ya shule. Watu kula wakalisikia hilo wese. Wacha walalamike. After a week ikaonekana jambo halijaisha ikabidi wadanganye kwamba hakuna chakula shule imeshindwa kulisha wanafunzi hivyo imefungwaaa.... weuweee mabasi kesho yake haya hapaa[emoji23][emoji23] kuna ticha wa kiume akanambia mkakunwe salama mkirudi tusisikie tena vicheko vya hovyo
 
poleni lakini sina hakika kama huu ugomvi wenu ulifikia tulichokuwa tunakifanya MUSOMA TECH
tulikuwa na ugomvi mkubwa na MARA SEC na tumepigana Mara nyingi. kadhalika tulikuwa na ugomvi na SONGE SEC mpk wavulana wakatawanywa mashule mengine ikabakia SONGE GIRLS wake zetu. pia ugomvi na makundi ya vijana wakorofi wa Musoma mfano: JAMAICA MOKERS, MBIO ZA VIJITI, WEST LAWAMA, MDOMO WA FURU N.K
 
Hahaha tunarudi kwenye midahalo ya co education is better than single sex education. Sitasahau hizi balehe. Tulikaa muda mrefu sana shule. Hiyo wiki tuko mabwenini akicheka huyu anapokea huyu. Yaan hamna sabaabu. Watu mabwenini ni vicheko tu aisee.. nilikua kiongozi wa chakula. Niliona kwa macho yangu mafuta ya taa yakimiminiwa kwenye makande[emoji23][emoji23][emoji706]
Nilichofanya niliagiza kiepe nje ya shule. Watu kula wakalisikia hilo wese. Wacha walalamike. After a week ikaonekana jambo halijaisha ikabidi wadanganye kwamba hakuna chakula shule imeshindwa kulisha wanafunzi hivyo imefungwaaa.... weuweee mabasi kesho yake haya hapaa[emoji23][emoji23] kuna ticha wa kiume akanambia mkakunwe salama mkirudi tusisikie tena vicheko vya hovyo
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
kwa kuzuia hizi bangi zisistawi tena ndio maana akina chalamila wakaingilia kati kuchapa watoto stick.

mob ni mbaya sana,kundi la watu ni jeshi linaweza fanya chochote kibaya kabisa.
 
Binafsi nimesoma mlama sec huo mwaka umbwe sec waliogopeka miaka hiyo na nina kumbukumbu mimi huo mwaka 2009 nilikuwa Mlama sec. Pale.
 
Machame inatenganishwa na mto. Hivo kwa ninavojua mimi lyamungo ipo kibosho machame ni mpaka uvuke mto uliopo chin ya lyamungo kutoka kijiweni so sidhani kama lyamungo ipo machame
Kuna vitu viwili unachanganya hapo mkuu. Kumbuka Kibosho ni wilaya ya Moshi vijijini na Machame ni wilaya ya Hai. Sasa Lyamungo iko wilaya ya Hai.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
sitaki kukumbuka nyakati zile, hasa maiv ya yule mama na sauti ya mkuu wa wilaya akitangaza kifo cha mshkaji alisema hivi, 'mtoto akililia wembe mpe ajikate, vijana mmeenda kuchezea wembe mmejikata mmempoteza mwenzenu kwa upumbavu wenu' RPC utawaletea maiti ya mwenzao waje waione kabla ya mazishi yake' aisee ni bahati familia iliona si busara, nyakati zote mwili ulikua kama umepata ganzi hivi.
.
.
miaka michache imepita sasa nimegundua mwanaume akikaa mwenyewe kwa muda mrefu anakua na hasira za ajabu sana, dogo aliefariki alipigwa na slesha iliyonolewa kama jambia.. huku wa lyamungo amechinjwa kwa seng'enge.
.
.
kisa uhasama ambao tumeukuta toka kitambo, pale nahisi umachame na ukibosho umo ndani ya zile shule, umbwe tuliona ufahari sana kukuta viti vya shule ya lyamungo tumeviiba na tunavisomea.
.
.
mkuu wa wilaya akasema nimeskia skia kuna viti vinasababisha haya sasa WANAUME LETENI KITI KIMOJA TUWAKABIDHI KAMA ALAMA YA USULUHISHI, likapikwa pilau shule tule na lyamungo, wakaja viongoz wa lyamungo wadau wanataka watie sumu kwenye chakula, mara wawafungie ndani ya darasa wapige ambush,
.
.
unapigwa wimbo wa shule mtu anaimba kwa hisia, kama vile anaitetea nchi yake!
.
.
Mr financial asante kwa kumbukumbu, apumzike kwa Amani mwana Umbwe mwenzetu na Mwanalyamungo, Mola atusamehe kwa dhambi zile, ilikua ni mbaya sana yale mambo!
Amina,hii makitu imetokea nimeshamaliza hapo mti msafi
 
Kipindi Cha makange umbwe ilifika hatua tukaiita college kulikua na ufree uliopitiliza, migomo isiyoisha, walikua kupigwa ilikua ni mwendo wa uharamia, watu mda wowote wanaenda kulewa mpaka wanazima wanaletwa shuleni hawajielewi

Lyimo nae shule ilikuja mshinda tatizo ni wapigaji wa hela, shule ikawa na matatizo mengi kwa migomo ikawa kila uchwao

Kipindi hicho form one mpaka six sare moja ya kaki ukija mgeni ukikaa vibaya unaingizwa mjini sababu huwezi tofautisha uyu ni form one au form four
Uyo makange siasa yake ndio iliiharibu umbwe muongo sana, stori mia
 
Umesahau ile fujo ya mwaka 2003 mlipokuja mpirani pale Umbwe mzee.?
Hii walitoboa mpira na bisibisi kilichofatia ilikuwa ni kichapo kwa wanafunzo wote wa lyamungo hadi walimu walitoka nduki
 
Kukata mkia maana yake ni kukaribishwa,wanachokifanya ni kuwaogesha wageni wote form five or form one kwenye maji ya mtaro yatokayo mlima Kilimanjaro saa sita kamili usiku,huku wakisindikizwa na kipigo
Nb.hayo maji yana baridi kinoma!
Hii ilikuwepo sana Geita Secondary (Geseco) ile shule ilikuwa zaidi ya kambi ya jeshi
 
Back
Top Bottom