Vurugu zaibuka msiba wa watoto matajiri wa Arusha, mwandishi wa Ayo TV anyang'anywa camera

Vurugu zaibuka msiba wa watoto matajiri wa Arusha, mwandishi wa Ayo TV anyang'anywa camera

Hawa waandishi wa udaku hovyo sana, watu wana majonzi wewe unakwenda kuwahoji na kuwarekodi ili upate udaku wa kupeleka kwa mange kimambi. Amekipata alichokistahili na liwe fundisho kwa wadaku wengine
 
😁Haya bana mrembo kwakuwa umesema wewe wacha nisikupinge, lakini nikukumbushe ,misiba ya Magufuli , Nyerere ,Mkapa nk hakukuitwa mtu ila huwa wandishi wanaenda, hata Mimi kwenye ukoo wetu Kila Mara akifa mtu mkubwa huwa tuna record

Nadhani hapo ingetumika tu busara hao vijana wangefuta Kama Kuna picha za msiba na wamuambie mwandishi amekosea

Kwa sisi wasukuma taratibu zetu, hao vijana wangepaswa kutandikwa viboko hapo hapo msibani
Kuna misiba ya kitaifa na misiba private unapaswa kutofautisha
 
Wiki chache zilizopita nilikwenda kwenye kifo kimoja cha utata pale Arumeru kuna bibi alifia kisimani nilipofika nataka anza coverage akaja ndugu mmoja wa marehemu akataka vifaa vyangu maswali mengi then wakanigomea asee watu wa Arusha wakorofi sana hususan kwenye mambo yao hawapendi publicity
Kuna tofauti kati ya 'kifo' na 'msiba' - wewe ilienda kwenye 'msiba' na sio kwenye 'kifo'
 
Nimeshapiga wengi sana. Siku moja nilizua vurugu kwenye club maarufu inaitwa PICNIC...kwa nje nilikwidana na jamaa akaja na ndugu yake. Nikaamua kuanza kurusha makonde. Niliwapasua vibaya wachaga wale wanaojinasibisha na wamasai. Hamna kitu vijana wa arusha maneno mtupu!
Kila anaefariki Arusha utaskia mtoto wa tajiri ina maana mji mzima hakuna maskini. Ule mji wa kiboya Sana wanapenda kusifiana ujinga mda wote. kama kweli wanaweza waje mjini apa DSM tuoneshane umwamba
 
Acha wivu wako tajiri utajiri haufichiki mkuu!, usemalo sio kweli.
Sijajua umenisoma vipi mkuu, lakini nimewahi kutembelea na hata kukaa mikoa hiyo ya Wachaga. Ukimtendea wema hasa ukimnunulia pombe mara kwa mara atakusifu kuwa wewe ni tajiri kila sehemu. Hakuna wivu hapo na wala sijamaanisha huko hakuna matajiri.
 
Wiki chache zilizopita nilikwenda kwenye kifo kimoja cha utata pale Arumeru kuna bibi alifia kisimani nilipofika nataka anza coverage akaja ndugu mmoja wa marehemu akataka vifaa vyangu maswali mengi then wakanigomea asee watu wa Arusha wakorofi sana hususan kwenye mambo yao hawapendi publicity
Ni sawa, publicity ya nini mambo ya huzuni
 
Habari haijasema Kama mwandishi alikuwa ameanza coverage Bali alikuwa ndio anafika msibani, au Mimi ndio nimewaka ?

Kama Ni hivo nilivoelewa Basi Ni kosa kumnyang'anya vifaa vyake
Unaenda msikitini na nguruwe uachwe sababu hujaanza kujenga banda lake?
 
Mimi naona kama kuna taarifa zinafichwa,kwanza ajali haijaripotiwa
na jeshi la polisi,pili familia kuteketeza memory card ya mwandishi,tatu kama kuna watu wengine wamejeruhiwa katika ajali hiyo na hawana wa kuwasemea,hapo taarifa za mwandishi huviamsha vyombo vingine kuchukua hatua.
Taarifa za ajali zinapatikana eneo la ajali na Trafic. Sio kusumbua watu msibani ikiwa hawapo tayari.
 
Hapa ndipo mzee wetu kinana nadharia yake ina bounce, nafikir ni muhimu trafik wamepo mpaka night ...
Tatizo ni mwendo kasi. Kama abiria na madereva tukijilinda bila kusubiri serikali itulazimishe ajali zinaepukika na kupungua.
 
Katika hali isiyo ya kawaida vurugu zimeibuka katika msiba wa watoto wawili wa matajiri jijini Arusha ambao walikuwa ni wachumba waliofariki ajalini jana ambapo zimepelekea mwandishi wa habari kutoka AyoTV kunyang’anywa camera.

Mbali na kunyang’anywa camera mwandishi huyo alinyang’anywa kadi (memory card)na kisha kuvunjwa na ndugu wa karibu akiwemo mdogo wa marehemu,Brighton Temu maarufu kama “Bonge “.

Vurugu hizo zimefuatia mara baada ya mwandishi huyo,Gedfrey Thomas kutinga msiba
ni kwa marehemu, eneo la KwaMrefu majira ya saa 10:30 leo jioni kufuatilia tukio la kifo cha mtoto wa Tajiri Denso.

Taarifa zimeeleza kwamba mara baada ya mwandishi huyo kutinga msibani hapo akiwa ameshikilia camera yake mkononi ndipo kundi la vijana waliojitambulisha ndugu wa karibu akiwemo mtoto wa mfanyabiashara anayemiliki mgahawa wa Uzunguni City Park ,Kevin Masuwa alimvamia na kutishia kumpiga mwandishi huyo.

Taarifa kutoka msibani zimeeleza kuwa kundi hilo la vijana wanaodaiwa kuwa katika hali ya ulevi ndipo lilimuamuru mwandishi huyo akabidhi camera na baada ya kuwakabidhi walichomoa kadi na kisha kuivunja na kisha wakamrejeshea camera yake.

Hatahivyo,taarifa zimedai kuwa mara baada ya vurugu hizo ndipo baba wa marehemu tajiri....maaarufu kama “Denso “ndipo alipomfuata mwandishi huyo na kumuuliza gharama za kadi hiyo ili amlipe lakini mwandishi huyo alikataa na kudai anahitaji kadi pekee.

Akihojiwa na waandishi wa habari Mwandishi huyo kwanza alilaani tukio hilo na kudai anawatambua vijana waliomfanyia fujo na kumyang’anya vifaa vyake vya kazi.

Mwandishi huyo alisema kwamba yeye alifika msibani hapo kufuatilia tukio la ajali lililopekea mauti ya kijana huyo kama Mwandishi na ghafla alipoingia ndani ya eneo la tukio alishangaa kuvamiwa na kundi la vijana mbalimbali.

“Mimi baada ya kufika msibani niliingia moja kwa moja eneo la tukio nikiwa nasogea ndani ghafla walitokea vijana ninaowatambua kwa sura wakaniamuru niwakabidhi camera nilipotaka kukataa walitishia kunipiga ndipo nikawakabidhi wakachomoa kadi na kisha kuivunja “alisema Mwandishi huyo

Hatahivyo,alisisitiza kuwa kitendo kilichofanyika sio cha uungwana na anajiandaa kutoa taarifa mbele ya jeshi la polisi mkoani Arusha.

WATOTO wawili wa Matajiri wakubwa katika jiji la Arusha,wanaodaiwa kuwa ni wachumba , Estomi Temu na mpenzi wake Nice Mawala(24)Mkazi wa Njiro walifariki dunia jana kwa ajali mbaya eneo la kwa Mrefu katika jiji la Arusha .

Kwa mujibu wa shuhuda wa tukio hilo ,ajali hiyo iliyotokea majira ya saa 7 usiku katika eneo hilo wakati gari la kifahari walilokuwa wakitumia lilikuwa kwenye mwendo kasi.

Katika tukio hilo linalodaiwa walitoka Klabu ,Nice alipasuka kifua na kuvunjika mkono wa kulia huku Estomi akiumia kwa ndani na kuvuja damu masikioni puani na mdomoni.

Watu mbalimbali wameendelea kufurika katika msiba huo ambao umeibua gumzo ambapo idadi kubwa ya magari ya kifahari imeibua gumzo kufuatia kupangana kuanzia nyumbani mpaka barabarani katika kituo cha KwaMrefu baada ya kukosekana eneo la maegesho.

Mwisho.

View attachment 2310353View attachment 2310357
Bladifaken hawa waandishi wa online tv,unaenda kuhoji msibani mtu kafiwa ili upate nini?wakamhoji january makamba kwanini umeme unakatika hovyo kila siku
 
Huwezi kwenda msibani hata kama ni mwandishi wa habari bila ya idhini ya wenye msiba.
 
Back
Top Bottom