Vurugu zisizoisha kitongoji ninachoishi Afrika Kusini

Vurugu zisizoisha kitongoji ninachoishi Afrika Kusini

Tukumbuke. Ngono ndebele, tswana na nandini wali migrate in 18c toward north kwa sababu ya wazuru.
Wazuru walianza Fujo hata kabla ya wazungu hawajaja south.
Inasemekana san and khoi people walipewa option tatu na wazuru
1.Wajiunge na zuru empire
2.Wahame
3.Wauwawe.
Nasikia wengine walijiunga, wengine waliingia ndani huko karahali desert na wengine waliuwawa.
Waliwaua pilgrim wote(andunje kama wale wa kongo)
Zuru people ni kundi baya zaidi la wabantu hapa Afrika.
Wabantu wa Afrika mashariki tuliweza kuishi bila magomvi ya kuua kwa kughirikisha kizazi.
Tumeweza kuishi na wasomali, nailoti,warabu,wahindi nk.
Tulishindwa kuishi na wazungu tu kutokana na tabia zao mbaya.
Wazuru mpaka leo wameshindwa ku intergrate na kaburu wanatamani aondoke wakati kaburu hana kwao mpaka sasa zaidi ya SA.
Poleni sana watu wa huko.
 
KWani wazawa hawana biashara huko mpaka nyie mkifunga mpaka wafate town bidhaa au huduma??
Kwani kuna Mzaramo mwenye duka kariakoo?

Wamekuja Wakinga juzi tu wameikamata kariakoo.

Sasa Tanzania ingekuwa ni primitive country kama wale mbwa wa kizulu Kariakoo pasingekalika na Wachina wangeuwawa sana.

Shida moja wale primitive nashindwa kuwaelewa mpaka leo wao mgomvi wao ni kwa weusi wenzao, tena wanawaita jina la kibaguzi "Makwelekwele" wanawaogopa wazungu usisikie.
 
Kesho yake pakatulia sio wao wala sisi kuonekana kiwanja cha vitaa

PART THREE-MWISHO

Mji ulikuwa kimya sanaa hiyo kesho yake ambayo walisema ni kiwanja cha vita kitajaa damu- hakikia na yeyote mabarabarani, kulisikika milio ya magari tu na hakuna yeyte nje kila mmoja alijifungia kwake

Kesho kutwa yake tena kimya na wiki nzimaa ilikuwa kimyaa

My friend tukajadiliana hapa haina haja ya kuambiwa tufungue maduka yaani tujifungulieni tu kwani tumeshawaweza na hawawezi fanya chochote kilee

Tukafungua- wakaanza choko choko siku hiyo hiyo tukasema hatufungi ila tunawaudumia wateja wetu nje? Ya bagla yaani , wateja hawatoingia mpaka ndani dukani tutawahudumia kama maduka ya bongo, huku huwa wanaingia dukani wanachagua vitu then wanakuja tunawapigia mahesabu alaf wanalipa dzain kama ya vimin market vilee,haikuwa hivyo ikawa tunawahudumia kama bongo vilee

Ila kuna wabishi walikuwa wanawaachia waingie wajichagulie na ilikuwa fursa tena kwa vibaka katika wiki hiyo hiyo

Kuna duka wameingia vibaka na kupola pesa na kumpiga shaba mtoto wa kiarabu/kiethiopia na kumuua ila walikuwa wezi tu sio hao wenye mgomo hatimaye wakakamatwa wakaenda jela- sema inasemekana kesi ya kuua sio kesi Kwa South Africa kwamba walikuwa wawili katika upelelezi akaachiwa mmoja Kwa maana yeye siyo aliyempiga bunduki ila mwenzake amenyea ila wanasema anaweza akakaa miaka miwili tu then akatoka ila waethiopia waneapa akitoka asirudi mitaa hii kwani nayeye watampeleka alipompeleka mwenzake yaani watampiga bomba nayeye, yule mmoja tunasikia tu ametoka ila hayupo mitaa hii itakuwa amehamishwa mji

Na uwezi amini hao watoto waliomuua huyo jamaa walishawahi kuja dukani kwetu wakataka waibe tukawashitukia, tukataka tuwachape tumewakolomea tu tukawaacha maana kujenga vichuki vidogo vidogo sio inshu kabsa, maana hata ukiwakazia kuwapa sigala wakilalamika hawana kitu wanaweza wakaja kukupiga bomba yaani chuki tu mwananga sio maisha kabsa south africa hapafai kabsa yaani tupo tu Kwa ajili tumeshaanzisha maisha

KIKANUKA TENA SERIOUSLY HIYO WALIOSEMA WANAKINUKISHA

tuliambiana tufunge biashara yukafunga, wakakusanyanaa mitaani na kuanza kuchoma mapira wana mapanga na malungu na Safari hii walikuwa wengi sanaa

Sisi kama kawaida tukashituana kuwa vita imerudi tena na uzuri mahojiano ya siku ilee halifika sehemu husika so kulikuwa na asikari maalumu wapo doria

Wakawakamata ma- icon wao kama kumi , kumi na mbili hivi, yaani waliwakamata walee waanzilishi wa vurugu wakawatia ndani lakini tulikuwa tayari kwa vita , yaani tulikuwa tayari kwa chochote

Ila binafs nilishukuru kuona pambano lipo off Kwa leo nilishukuru

Walee wengine wafata mkumbo kuona wenzao wamekamatwa wakakimbia

Tukaambizana kilichoendelea tukatudisha silaha kwenye ala zake

Nna mpaka video ila sitaweza kiwawekea hapa mtandaoni

Vitaa ilisimama hivyoo- wajamaa hawajatoka mpaka leo kesi kila siku inapelekwa mbele wanaenda kama wachochezi wa vurugu

ila ninachokiona ili balaha likirudi tena itakuwa nomaa sanaa yaani watakufa watu yaani hapa nna mpango wa kujichanga kama Mil 10 , nitokomee canada/ popote pazur ila ndio nakichanga

Baada ya hili balaa- kuna baadhi ya wabongo ambao hawakuvunjiwa maduka yao, wameuza biashara zao na kwenda Tanzania kuanza maisha mengine nanasikia wengine waneshapata visa wapo zao canada huko , yaani hapa ndonga linauma nitoke hapa SA nitafute kiwanja kingine- ila ilee kutoka moyonisiogopi chochote kilee sio kuhusu tunavyopondwa watu wa SA wala hayaa maisha ya bastola kila siku sihofii chochote kilee

Ninachohofia kupoteza biashara yangu tu I wish nipate mteja niiuze nitokomee zangu makanada huko

Najifunza vingi sana na ukifikiria nna 29 yaani na naendelea kujifunza

Kuhusu kuuza biashara wasomali na waethiopia hawaogopi chochote ukitaka kuuza wao wananunua tu wao wapo tayari kwa lolote nipo kwenye mafikirio ya kuuza ila ngoja kwanza niangalie upepo


MWISHO [emoji1478]

Kuna mengi sijayaweka katika maisha ya kila sikuya South Africa
Nimeshatolewa bunduki mara mbili na kutolewa kisu mara moja ki ukweli ni maisha ya roho mkononi, karibu sanaa SA

ASANTUM- tupo sanaa maisha hayaa ila ikimpendeza M/Mungu atujaalie tutusue twende zetu CANADA HUKO-InshAAllah [emoji1431]
Ndg hakuna chenye thamani zaidi ya maisha.
Maisha hayo ni yakubahatisha, fanya uamuzi wa haraka. Riziki ni popote, amini atapoenda inaweza kuwa ni sababu ya kutokakimaisha
 
Kama unadhani ni lazima ufanye maisha yako South Africa basi hakikisha hauishi location.

Kama unaishi location IPO siku yako utazikoga risasi za kutosha tu, msidanganyane.

Mcongo hawezi kushindana na mbongo Kinondoni eti kisa Kinondoni kuna Wacongo wengi, mnadanganyana, tutaendelea kupokea maiti zenu airport.

Sitaki kudharau maneno mazuri uliyoniambia ila ukweli ni kwamba mtu anakufa popote sio sisi tu ambao tunapigwa risasi hata na wao wenyewe wasouth wanauana Kwa risasi mfano AKA.. so Mungu akikupangia kufa kwa kupigwa risasi hata hapo hapo bongo unaweza ukamiminiwa hata risasi 5 , uwa naamini sanaa kwenye M/Mungu mkuu

Atakachopanga ndicho kitakachokuwa- hivyo tu
 
Sitaki kudharau maneno mazuri uliyoniambia ila ukweli ni kwamba mtu anakufa popote sio sisi tu ambao tunapigwa risasi hata na wao wenyewe wasouth wanauana Kwa risasi mfano AKA.. so Mungu akikupangia kufa kwa kupigwa risasi hata hapo hapo bongo unaweza ukamiminiwa hata risasi 5 , uwa naamini sanaa kwenye M/Mungu mkuu

Atakachopanga ndicho kitakachokuwa- hivyo tu
Vingine anapanga shetani usiwe mjinga.
 
Hizo nchi wataenda kumuuzia nani sembe?

Sio kila mtu aliyekuwa ughaibuni anauza sembe haipo hivyo ni chuki dhidi ya watafutaji walio nje na Tanzania ila nakuhakikishia maneno tupu sio kitu fanya utuue
 
Back
Top Bottom