VVU na UKIMWI: Historia yeke, chanzo cha maambukizi, dalili, kinga na juhudi za kupambana na ugonjwa huu

Kuwa na huruma.
Mkuu nina huruma sana
ndo maana nilisema kwanini wasilete chanjo mbadala wa vidonge kila siku katika maisha ya mtu
kuna mtu nilikuwa namjua anaugua alikata tamaa akasema afadhali niende kuliko kuishi kwa kutegemea ......vidonge
sasa watafute hata sindano ya kuchomwa baada ya miezi kadhaa kama sita au kwa mwaka mara moja
hiyo itakuwa afadhali
 
Hahah huyo alikuwa kakata tamaa na maisha,kuathirika sio mwisho wa maisha,mbona mateja kila asubuhi wako mwananyamala kunywa methadone na hawalalamiki
 
Wamekusudia kuongeza msongo wa mawazo kwa watu au??
Waacheni waishi bila stress!
 
Nafahamu,lakini kwenye maisha kukata tamaa n mwiko
Hawa kina Mshana JR nadhani ni wakati sasa wajitokeze na dawa angalau zinazotibua makali ya VVu
Wengine wanasema wanaongeza CD4 lakini nadhani ni yale ya DK mmoja mwenye kituo cha radio kule Dodoma
 
Hii habari imekaa kibiashara zaidi. Inalazimisha wagu wapime ilo uwape ARV?? Hayo madawa ndo chanzo cha uounfuvu wa kinga mwilini. Haiwezekani MTU una afya halafu uwe unakunywa madawa kila siku. Lazima figo zitashindwa kufanya kazi. Hawa wamarekani wangekuwa wanatupenda sana wangekuwa wanatoa dawa za malaria bure maana ndo inayoongoza kwa kuua watu.
 
Kwaio wakumkuta mtu anao watampa pesa yakununua matunda namsosi au ndo kuachana nastress usawa huu wavyuma!! pima at your own risk
 
Hajar ushawahi kupima wewe? Majibu ulisubiria au uliamua kuondoka?
 
kumbe hauambukizi kwa kugegedana
 
Ndio nshawahi Sesten. Hahaaa. Nilisubiria mpaka mwisho na sikuondoka.

Vp upande wako na wewe? [emoji85] [emoji85]
Hahahaaa hongera bana

Mimi mara ya kwanza nilienda pima kwenye hospitali amabayo nilikua namfahamu dada wa maabara. Baada ya kutolewa damu nikaambiwa nisubiri kidogo nitaitwa kwa majibu. Nisubiri kidogo halafu nikasepa! Baadae nikampigia simu yule dada nikamwambia nimepata dharura nimeondoka akanambia sawa basi ukimaliza ya huko uje uchukue majibu yako. Juhudi zangu zote za kumshawishi anambie kama mambo mazuri au mabaya ziligonga mwamba, alinisisitiza tu nifike mwenyewe pale hospitali

Nilikaa hadi kesho yake mchana nikakaza roho nikasema potelea mbali acha tu nijitose, nikaenda. Sasa ule ushauri nasaha kabda ya majibu ndio unahisi pressure inapanda, inashuka, kiroho kinataka kutoka, jasho jembamba hadi maeneo flani.....mpaka mwisho aliponyoosha mkono kunipa handshake na kunambia hongera nikawa siamini!

Baada ya pale nikarudia tena Muhimbili. Na kuna siku nilikua Morogoro kuna mtu nilienda kumuona hospilali ya mkoa alikua anatakiwa kuongezewa damu nikaomba tu mwenyewe wanicheki, lakini kile kipindi cha kusubiri majibu unapopima mara ya kwanza asikwambie mtu ni kigumu sana Hajar
 
Ndio nshawahi Sesten. Hahaaa. Nilisubiria mpaka mwisho na sikuondoka.

Vp upande wako na wewe? [emoji85] [emoji85]
@Hajar Kama nakuona vile kimoyo kilivyokuwa kinadunda pale kwenye benchi la kusubiria[emoji23][emoji23]
Ile kazi sio mchezo ujue..
Tena kama unakumbukumbu ya faulo zako mbilitatu ulizozipiga kipindi chanyuma[emoji3]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…