Vyakula tunavyolishwa kwenye Baa, Hotelini, Migahawa nk

Vyakula tunavyolishwa kwenye Baa, Hotelini, Migahawa nk

kuna siku calabash nimekaa karibu na jikoni, mhudumu kaja kuchukua chakula kwa bahati mbaya akadondosha paja ya kuku kwenye sahani hadi chini, ile kiroho safi kabisa kamwambia mwenzie embu niokotee. kashika na mikono toka kwenye sakafu moja kwa moja kwenye sahani.. inaenda kwenye meza! nilisikitika sana..
 
aisee kuhusu vyakula hapa mjini ni tatizo kuu,uweza shangaaa unakula nyama ya kuku lakini husikiii ladha yoyote ya nyama,kwa ndugu zangu wapenda kachumbari na juisi ndo shida zaidi,nyanya zinazo itwa masalo ndo hutumika zaidi kutengenezea hiyo kachumbali omba tu kusikia hayo masalo kuliko uyaone.kwa wapenda juisi zinazotengenezwa mtaani na kuwekwa kwenye chupa za maji zinazo okotwa mitaani nitabu tupu,nyingi za chupa hizi huokotwa mitaroni zikiwa na mikojo ambapo siamini kama zinasafishw kwa maji ya moto,ndo hizohizo huwekewa hizo juisi
uzi huu mkuu haupaswi kutolewa humu moja kwa moja.unapaswa kudondoshwa humu hata kila baada ya wiki mbili.Umetukumbusha mambo mengi saaana.Binafsi nimejihurumia na wakati mwingine comments zimenichekesha sana.Ni mizoga,Masalo na chupa za juice zilizookotwa mitaroni zikiwa na mikojo.
Aiseee hii ni hatari saaaana
 
na wapishi wa mandazi na chapati wako ktk mashindano ya nani atauza zaidi
upload_2016-7-11_14-26-8.jpeg
 

Attachments

  • Uchawi wa mapishi.jpg
    Uchawi wa mapishi.jpg
    36.6 KB · Views: 107
Kwanza lazima tukubaliane kuwa hakuna mfanyabiashara anayependa hasara iwe ni hotel mgahawa au bar kubwa zikiwemo take aways. Wote hawa hutulisha ndaza na viporo.

Ni mara chache nno kuona chakula kinamwaga. Kikibaki kinahifadhiwa kwenye friji mpaka siku inayofuata. Shida inakuja kwenye umeme wetu ambao hukatika mara kwa mara ambapo husababisha chakula kuharibika.

lakini shida nyingine kubwa ni aina ya mafuta yanayotumika ,hii hasa ni kwenye hizi bar na hotel za kawaida ,kwa ajili ya kutaka faida kubwa hutumia mafuta ya bei poa ambayo yamejaa lehemu ,mbaya zaidi mafuta hayohayo hutumika kupikia chakula zaidi ya kimoja yatakaangia chips hayohayo yatakaangia mayai kuku samaki nk.

Viungo vingi ni vya kuokoteza kwenye masoko na vya bei poa ,kwa wale wapenzi wa kachumbari na salad mnalishwa minyoo mitupu kwa wale wapenzi wa tomato sauce nyingi ni feki za kutengenezwa mtaani.

Nyamachoma ,rost michemsho supu kuku na samaki vingi huwa vibudu na mizoga!!!tunalishwa vitu vya ajabu mno kuku wengi hawajachinjwa wamenyongwa nyama nyingi huwa hao wanyama wamekufa kwa ugonjwa nk samaki wengi huvuliwa kwenye mito na mabwawa ya mitaani full uchafu full sumu.

Nyama nyingine ni za mbwa paka nk.
Epuka michemsho mishkaki na roast za usiku supu za makongoro mkia ulimi nazo ndio hizohizo.

Tunakulaga vyakula ambavyo havina ladha au tunaharisha au kuumwa matumbo tujue tu kuwa siku hiyo tumelishwa ndaza vibudu au mizoga
Tuwe makini tunapoagiza hivi vyakula jamani
blaza nakula hapa umenikata moto asee
 
Kuna baa moja Kaloleni Arusha wanauza firigisi za kusaga na mayai
Hakuna firigisi pale ni nyama za miguu ya kuku na utumbo wake
 
Ukiacha mbwa na paka hata punda nyama yake watu wanalishwa bila kujua. Dodoma kuna kiwanda cha kuchinja nyama ya punda halafu minofu inapelekwa China lakini mabaki mengine kama makongoro, kichwa, matumbo na masalia ya nyama kama mbavu yanapikwa mitaani na watu wanakula bila kujua. Hata nyama yenyewe watu wamechanganyiwa bila kujua na kwenda kuipika nyumbani. Zamani watu wanaposafiri walikuwa na tabia ya kuandaa chakula cha safari wenyewe nyumbani ikiwa ni pamoja na kutembea na maji. Siku hizi wanajifanya wameendelea kila kitu ni kununua njiani matokeo yake tutalishwa hata nyama ya binadamu bila kujua
 
point yako ni nn watu wasiende baa na hotel au? tukale wap sasa kwa mfano hata kama unakula home je mchana ukiwa ktk mishe zako usile kisa utalishwa ndaza! cha msingi ni kula sehem makin tu si vinginevyo
 
Ukiacha mbwa na paka hata punda nyama yake watu wanalishwa bila kujua. Dodoma kuna kiwanda cha kuchinja nyama ya punda halafu minofu inapelekwa China lakini mabaki mengine kama makongoro, kichwa, matumbo na masalia ya nyama kama mbavu yanapikwa mitaani na watu wanakula bila kujua. Hata nyama yenyewe watu wamechanganyiwa bila kujua na kwenda kuipika nyumbani. Zamani watu wanaposafiri walikuwa na tabia ya kuandaa chakula cha safari wenyewe nyumbani ikiwa ni pamoja na kutembea na maji. Siku hizi wanajifanya wameendelea kila kitu ni kununua njiani matokeo yake tutalishwa hata nyama ya binadamu bila kujua
Nimekula ile nyama ya punda miezi mitatu mfululizo pale kiwandani

Sent from my SM-N910X using JamiiForums mobile app
 
point yako ni nn watu wasiende baa na hotel au? tukale wap sasa kwa mfano hata kama unakula home je mchana ukiwa ktk mishe zako usile kisa utalishwa ndaza! cha msingi ni kula sehem makin tu si vinginevyo
bona naona umeanza kwa kuniuliza lakini ukaishia kujijibu
 
Kwa kweli ni shida, mama nitilie wengi wali ukabaki kesha anapika mwingine kidogo. Ukiisha iva anaupakua nusu ya sufuria halafu anauweka ule wa jana katikatoti kisha ule wa leo alioupkua anauweka juu ili ule wa jana pale kati upate joto. Ndio maana wakati wa kupakua anachanganya changanya wa chini na wa juu. Unapewa mixa yako maisha yanaenda.
 
Hii ni kazi ya maPublic health inspector.

sema mabwana afya wetu Waendekeza njaa tu.

hili jipu nalo rais alitumbue. wafutiwe leseni kabisa, watu wakapike nyumbani.

hivi kati ya uchafu barabarani na hii migahawa/mama ntilie/wauza matunda ni wapi hasa watu wanapata kipindupindu na typhoid!
 
Hapo kwenye supu ya mkia umenipata kuna bar moja maeneo ya ubungo kila jiioni nikirudi kutoka kwenye mishe zangu lazima nipitie hapo kupiga hiyo supu ya mkia ila hii habari yako imenishtua sana

yenu bar hiyo bila shaka
 
Back
Top Bottom