econonist
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 20,189
- 29,663
Vyama vyetu vya siasa nchini vianze kujitofautisha kwenye mirengo ya kushoto au kulia. Hii itasaidia wananchi na wanachama kuvijua vyama hivyo vinasimamia Nini. Pia itasaidia vyama kujua vijikite kwenye maeneo gani na sera zipi.
Mrengo wa kulia unategemea zaidi kwenye ubepari na kuangalia maendeleo ya mtu mmoja mmoja. Ila mrengo wa kushoto unaegemea kwenye ujamaa na maendeleo ya pamoja. Kwa mfano nikipitia katiba ya CHADEMA naweza kukiri CHADEMA inafuata mrengo wa kulia Yani ubepari na nikiangalia katiba ya CCM naweza kukiri ya kwamba inafuata mrengo wa kushoto. Swali ni je, wanachama wa CCM wanajua kuwa chama chao ni Cha mrengo wa kushoto ? na je wanachama wa CHADEMA wanajua ya kwamba chama chao ni Cha mrengo wa kulia?
Nadhani ni muhimu vyama vikajiweka wazi kuhusu mirengo yao na sio kujificha kwenye uwingi wa uanachama, ushabiki na uchawa. Ni vizuri kuweka mirengo ya vyama wazi ili wanachama wawe huru kujiunga na chama kinachosimamia maslahi yao.
Mrengo wa kulia unategemea zaidi kwenye ubepari na kuangalia maendeleo ya mtu mmoja mmoja. Ila mrengo wa kushoto unaegemea kwenye ujamaa na maendeleo ya pamoja. Kwa mfano nikipitia katiba ya CHADEMA naweza kukiri CHADEMA inafuata mrengo wa kulia Yani ubepari na nikiangalia katiba ya CCM naweza kukiri ya kwamba inafuata mrengo wa kushoto. Swali ni je, wanachama wa CCM wanajua kuwa chama chao ni Cha mrengo wa kushoto ? na je wanachama wa CHADEMA wanajua ya kwamba chama chao ni Cha mrengo wa kulia?
Nadhani ni muhimu vyama vikajiweka wazi kuhusu mirengo yao na sio kujificha kwenye uwingi wa uanachama, ushabiki na uchawa. Ni vizuri kuweka mirengo ya vyama wazi ili wanachama wawe huru kujiunga na chama kinachosimamia maslahi yao.