Pre GE2025 Vyama vya siasa vijiongeze kwa kuajiri wataalam ya lugha ya ishara wanapofanya mikutano yao

Pre GE2025 Vyama vya siasa vijiongeze kwa kuajiri wataalam ya lugha ya ishara wanapofanya mikutano yao

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

mwanamwana

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2011
Posts
1,309
Reaction score
4,798
Vyama vya Siasa nchini vinatakiwa kuweka mazingira wezeshi yatakayowasaidia watu wenye changamoto ya kusikia na kuongea ili kutimiza haki yao Kikatiba ya kushiriki katika mchakato mzima wa kushiriki uchaguzi bila kuwepo kwa vikwazo.

Kutokuwepo kwa mazingira rafiki kwa kundi hili maalum, kunaweza kuwa chanzo cha wao kutowapata viongozi ambao watasimamia maslahi yao na ya wengine wenye uhitaji maalum. Watu wenye ulemavu wanapaswa kupewa kipaumbele ikiwemo kuweka mazingira wezeshi yatakayosaidia kushiriki mchakato mzima wa uchaguzi kuanzia hatua za awali.

Hii itawasaidia ushirikishwaji wa kina kwani watapata uelewa zaidi wa hotuba na midaharo itakayokuwa inatolewa na wagombea mbalimbali na vyama vya siasa kwa ujumla, hivyo kuwawezesha kufanya maamuzi wakiwa na taarifa sahihi.

Kwa ajili ya ustawi wa demokrasia nchini, suala hili haliepukiki.

Asanteni.
 
Una hoja. Ni kweli si vyama vya siasa tu bali hata wataalishaji wengi wa maudhui ya televisheni ni kama wamewasahau hawa wenzetu wenye changamoto za kusikia.
 
Vyama vya Siasa nchini vinatakiwa kuweka mazingira wezeshi yatakayowasaidia watu wenye changamoto ya kusikia na kuongea ili kutimiza haki yao Kikatiba ya kushiriki katika mchakato mzima wa kushiriki uchaguzi bila kuwepo kwa vikwazo.

Kutokuwepo kwa mazingira rafiki kwa kundi hili maalum, kunaweza kuwa chanzo cha wao kutowapata viongozi ambao watasimamia maslahi yao na ya wengine wenye uhitaji maalum. Watu wenye ulemavu wanapaswa kupewa kipaumbele ikiwemo kuweka mazingira wezeshi yatakayosaidia kushiriki mchakato mzima wa uchaguzi kuanzia hatua za awali.

Hii itawasaidia ushirikishwaji wa kina kwani watapata uelewa zaidi wa hotuba na midaharo itakayokuwa inatolewa na wagombea mbalimbali na vyama vya siasa kwa ujumla, hivyo kuwawezesha kufanya maamuzi wakiwa na taarifa sahihi.

Asanteni.
Hili linamaana sana na lina umhuhimu wa kipekee kwa wenye mahitaji maalum. Vyama makini zingatieni na kufanyia kazi ushauri huu mujarabu wa kiungwana kabisaa 🐒
 
Leteni hilo deal wajuzi tupo ! Mkitaka na taarifa tuzichape kwa nukta nundu niko hapa mtaalam!!
 
Awa wanao tumia lugha ya arama wachukuliwe wenye uzoefu wasichukuliwe mtoto wa mjomba kahapa
 
Back
Top Bottom