Zamiluni Zamiluni
JF-Expert Member
- Feb 11, 2014
- 13,997
- 15,112
Mbili, tatu za falsafa za siasa ni kuhadaa ummaViumbe hatari zaidi katika ustawi wa nchi yetu siyo bacillus bacteria, wala plasmodium, wala HIV wala corona -- ila ni wale watu wanaotuhadaa kuwa ni viongozi wetu na wapo kwa ajili ya maslahi mapana ya umma, ilhali hata wangepewa miaka elfu ofisini hakuna lolote bora la mafanikio watendalo zaidi tu ya kuendekeza uzembe, rushwa, ufisadi, kujinufaisha, migawanyiko, ugomvi, migogoro na ulevi kwa namna zake mbili.