Wa Protestant wa kweli ni SDA church na Mashahidi wa Jehova, hawa hawaku copy chochote kutoka RC.Chrstimass ni kwa ajili ya Catholic

kwa nini ikawa 25? ni Scam kubwa sana ilifanikiwa
 
Na kanisa Katoliki halijakataa hilo.Nongwa imekuwa kwa wayahudi/wafarisayo aka wasabato.
Ni mbinu ambayo ilitumia kujiongezea wafuasi, hata sanamu kuingizwa kwenye mambo ya kiibada iliwaongezea wafuasi wengi sana.
Ni kama walokole kutumia miujiza na ushuhuda feki kuvuta watu, na wanawapata. Watu wanatakiwa wavutwe na Neno la Mungu.

Katika mambo ya krismass sina shida na wakatoriki maana ni maamuzi yao ya kidini qmbqyo hayana uhusiano na maamuzi ya dini yangu.
 
Basi ni ujinga na hii ndio Scam kubwa kuliko Scam zozote zile.
Scam wapi acheni ujuaji wa kijinga,
Wewe sherehekea kumbukumbu ya kuzaliwa Mwokozi Tarehe waachie Warumi namna gani bwana Farisayo?
au hauna hela ya kupiga mvinyo na kitimoto sikukuu hii?

Shetani hapendi watu wafurahie kuzaliwa Mwokozi na ndio maana siku zile akamtumia Herode akajifanya anawapa mawaidha Mamajusi kumbe ana agenda za siri mwisho akaua watoto leo hii huyo kinyamkera Ibilisi anawatumia nyie kupinga Happy birthday party ya Mwokozi wetu Yesu Kristo

Tumestukia hila za mwovu maana leo iliwapasa mtumie siku kueneza habari njema za ujio wa Mwokozi badala yake mmejifungia maghetoni mnamkana dawa yenu inachemka!

Au nasema uongo johnthebaptist?

#Mkisusa sie twala!
😁😁
 
Hawa SDA na mashahidi wa Yehova ni vichaa. Huwezi kuacha kusherekea Christmass na unamuamini Jesus, usherekee January, February nk lakini lazima usherekee hyo sikukuu.

Ni maadhimisho hata na pasaka ni hvyo hvyo, tarehe na mwezi Wala siyo matter of fact, ni ukichaa tu.

Hizi Imani zimefifisha sana akili za watu, Imani ni kitu simple sana, ni swala la Imani tu, hutakiwi kukompliketisha Mambo.
 
SDA na RC uzi wenu huu. Njooni mtwangane
SDA wameshavurugana kuhusu Utatu Mtakatifu. Mwanzo walikuwa wanakataa concept ya Utatu Mtakatifu (Trinity), sasa hivi wanabishana kuhusu maandiko ya Ellen White. Wapo wanaosema aliukubali Utatu Mtakatifu, wapo wanaokataa na kusema kuwa alichoandika hakumaanisha kuukubali Utatu Mtakatifu
 
Fact!
Kikubwa tuishi katika misingi hii hii tuliyojiwekea,
Maana ukiangalia kila kitu kilitengenezwa na watu tu
Kutokana na mazingira yao
Kila mtu yupo sahihi kwa upande wake hivyo kila mtu afurahie kwa nafasi yake
Maisha ni zawadi

Au nasema uongo?
 
Ukiamua kuipa akili yako ifanye kazi Kwa uhuru kuhusu dini utagundua, kitu muhimu ni Imani na kuabudu, na Wala siyo mashindano. Akili iliyokata tamaa na mashindano ya kiimani inaona Imani za kidini ni Mambo ya kutungwa, Naam Mambo Historia nyingi Duniani ni Mambo yaliyotungwa au kuongezewa chumvi.

Imani Iko overated sana.
 
sio swala la wema au kuto kuwa wema ila ni sikukuuza kipagani na ni moja wapo ya Scam kubwa sana ilio fanikiwa Dunia ino kote
Chagua tarehe ambayo unadhani sio ya kipagani, ndio maana ya uhuru wa kuabudu. Usitumie nguvu kuwazuia wengine waliochagua hiyo, bali tumia uhuru wako kuchagua tarehe ambayo unadhani haitaangukia kwenye Gregorian Calendar, maana Gregorian Calendar ililetwa na wapagani wa Kiroma πŸ˜€
 
Wapumbavu nyie, hamkucopy wakati mnatumia mafundisho ya biblia Yao ambayo mmeichukua direct bila kuhoji humo ndani maandiko ndivyo yalivyotakiwa kuwa?

Yaani huyo mrumi afanikiwe kuharibu mifumo ya kidini then ashindwe kuharibu maandiko mnayoita matakatifu?

Kwa bahati mbaya sana mkatoric hamuwezi kumkwepa kirahisi hivyo mpaka mkatae Kila kitu mlichokikuta kwake, kuanzia mifumo ya kidini, mifumo ya maisha ya kawaida na hesabu za calendar, maandiko mkatafute ambayo yako sahihi na sio biblia ambayo imeshachezewa na hapa huwa hamtaki kukubali ukweli kuwa biblia nayo ni TAKATAKA imeshachezewa sana, imebadirishwa Kila kitu, mambo karibu yote ktk biblia ni uongo, yameandikwa kuwakuza hao hao watunzi wa dini na mataifa Yao bandia ya uroma, Israel feki, na wazungu kiujumla.

Narudia Tena, ni ngumu kwa hayo makanisa uchwara kushindana na babayao sijui mama Yao RC aliyewapa mbinu zote za kidini, huu ndio ukweli mchungu
 
Ha ha ha! Hili swali umelisuka kweli kweli! Halijibiki kwa namna yoyote ile.

Wanatamani maandiko yasingeandika habari za kuzaliwa kwa Yesu ila ndio hivyo imeshakuwa. Kwa ujinga wao wanasahau kwamba siku, miezi., miaka na nyakati zote ni mali ya Mungu including hiyo 25 Desemba.

In my opinion hao waliochagua kuzaliwa kwa Yesu kusherehekewa hiyo tarehe walifanya la maana sana; kuwaonesha wapagani kwamba yupo Mungu wa kweli na siku zote including hii ni mali yake! And for sure na ule upagani ukapotea kwa walioiamini Injili Mungu akatukuzwa! Hili hawalioni.

Lau sasa mmesimamia misimamo yenu - Yesu alizaliwa au hakuzaliwa? Kama alizaliwa; pendekezeni tarehe - hawataki! Aaah; hebu wasibabaishe watu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…