Mkuu Tanzania ni nchi nyingine kabisa, ni nchi ambayo ina system za kipekee za kiuchumi, nimezungukazunguka kwenye nchi kadhaa na nimeshafanya biashara Bongo, na nilichokiona na ndio ukweli ni kuwa ukitaka kutoka bongo kwa biashara basi ni lazima ujitoe fahamu na lazima uwe mwenye roho ya chuma, ni kitu ambacho akiendani kabisa na theory za mtoa mada, sio kama nazipinga ni kitu cha kweli alichokiongea lakini sio kwa Bongo.
unatoka bongo unaenda kufunga contena la used engine Dubai ama Japan, unajua hesabu halali ya ushuru haizidi 10mil, wakati umeshapakia contena kwenye meli ghafla unapata ujumbe kwa waliokuwa bongo kuwa TRA wamepandisha ushuru na sasa ni 20m, sasa ushuru umepandishwa bila notice ya kutosha,
Acha kabisa hapo mzigo unauzia shaurimoyo kwenye kibanda cha less than 10x10 ambacho kodi iko si chini ya laki tano, sasa hili utoe mzigo bandarini na ufike dukani hapo lazima ujitoe fahamu, sasa biashara ganinya hivyo, hiyo 10m inapandaje na kuwa 300mil kwa biashara ya aina hiyo
Ushuru wa bidhaa Tanzania ni wa ku- bargain tu, unafungua contena mtu wa TRA anaangalia anakutajia ushuru bila vigezo vya maana, ilinutoe mzigo ndio hivyo tena lazima ujitie uchizi, sasa ni biashara ya aina gani hiyo?
hata mfano huo wa juice ya mtoa mada, hata kama juice imepimwa ilipotoka na ina viwango vyote lakini unapoileta Tanzania lazima uandae pesa ya kumpa mtu wa TFDA pamoja na TBS, sasa hiyo ni biashara kweli?
unaenda Bank kukopa na vigezo unavyo, lakini lazima ufanye deal na watu wa banki, sasa hapo kuna biashara kweli kama sio kijitoa fahamu na kijivika roho ya kutu