Wa Tz Tutakufa Maskini Kwa Kimbilia Kuchimbia Pesa (Kujenga) Badala ya Kuizungusha Izae Zaidi


umenena vema mkuu, shikamoo nakupa japo mm kaka yako!!!!
 

nimeshindwa kuchagua sentensi ya kupigia mstari, maana kila sentensi imejitosheleza mkuu ikanibidi nipigie mstari comment yako nzima, ahsante sana mkuu......mkuu Kituko once you get a chance win that chance, hili nakuasa liwe mwongozo ako wa kila siku hapa tz, system ya kiuchumi hapa tz ipo very unbalanced!!!!!
 
Last edited by a moderator:
Hii imetulia labda niweke na mimi langu la moyoni,,,
Nipo nje ya nchi kusini mwa africa nina mdogo wangu yeye yupo tz hapo Mbeya ni mwanafunzi wa form 4 kutokana kwamba tupo wawili tu! Huwa namtumia pesa, akaunti yake inasoma kama mil 12,, imekaa tu haina mzunguko wowote, nawaza kama nikija tz nifanye mradi gani pesa iendelee kuzalisha?
Sehemu yenyewe ni Mbeya je wadau mnanishauri vipi?
 

Nipe nikuwekee kwenye misitu ya miti ya mbao, ukija imepanda mara dufu.
 

Sasa unaonaje tukianza na stori yako kwanza na sio ya hao wengine unaowaongelea?
Kuna vitu nakubaliana na wewe na kuna vitu napingana na wewe, Ni kweli Watanzania wengi wanahitaji ukombozi kiakili hasa kwenye swala zima la biashara, hiyo ni sababu kubwa inayofanya biashara Tanzania kua haitabiliki, leo inaweza ikaonekana nzuri, kesho unalala unaamka huna mteja hata moja.. Na ukifikiria idea kubwa saaaana usisahau Tanzania nayo ni nchi masikini, kwa hiyo kama utafikiria vitu ambavyo ni very expensive market yako lazima i-base kwa watu wenye hela, mfano huwezi ukaimport Buggati kumi bongo ukitegemea kuziuza zote kwa kulala na kuamka tu..
Umesema the higher the risk the bigger the profit, ni kweli na pia the higher the risk the greater probability of being very poor hii ni kwa case ya Tanzania, mtu anapoinvest kwenye kampuni kama Twiga, huyo obviously anajua anachofanya maana kampuni kama ile ni moja ambayo zinategemewa sana nchini kwa kua hazina competition, sasa nafasi kama hizo sio kwamba ni nyingi kiasi hicho, tunachohitaji nchini ni Competition, Competition ikiwa kubwa watu watapata vitu kwa bei ya chini, sasa ona watanzania wanavyofikiria, kila kitu cha bei ya chini kwao ni Mchina!! hata kama ni competition, ukitengeneza Cement ukauza 2000 utaambiwa hiyo inadumu miaka 2 hata kabla mtu hajaitest kwa sababu amekalili Twiga Cement tu.... Kuna kazi kubwa sana kufanyika kubadilisha akili za watanzania, baada ya hapo ndiyo hata uoga utapungua..
 

akaunti yako au yake...LoL!!
 

Mkuu Tanzania ni nchi nyingine kabisa, ni nchi ambayo ina system za kipekee za kiuchumi, nimezungukazunguka kwenye nchi kadhaa na nimeshafanya biashara Bongo, na nilichokiona na ndio ukweli ni kuwa ukitaka kutoka bongo kwa biashara basi ni lazima ujitoe fahamu na lazima uwe mwenye roho ya chuma, ni kitu ambacho akiendani kabisa na theory za mtoa mada, sio kama nazipinga ni kitu cha kweli alichokiongea lakini sio kwa Bongo.
unatoka bongo unaenda kufunga contena la used engine Dubai ama Japan, unajua hesabu halali ya ushuru haizidi 10mil, wakati umeshapakia contena kwenye meli ghafla unapata ujumbe kwa waliokuwa bongo kuwa TRA wamepandisha ushuru na sasa ni 20m, sasa ushuru umepandishwa bila notice ya kutosha,
Acha kabisa hapo mzigo unauzia shaurimoyo kwenye kibanda cha less than 10x10 ambacho kodi iko si chini ya laki tano, sasa hili utoe mzigo bandarini na ufike dukani hapo lazima ujitoe fahamu, sasa biashara ganinya hivyo, hiyo 10m inapandaje na kuwa 300mil kwa biashara ya aina hiyo

Ushuru wa bidhaa Tanzania ni wa ku- bargain tu, unafungua contena mtu wa TRA anaangalia anakutajia ushuru bila vigezo vya maana, ilinutoe mzigo ndio hivyo tena lazima ujitie uchizi, sasa ni biashara ya aina gani hiyo?

hata mfano huo wa juice ya mtoa mada, hata kama juice imepimwa ilipotoka na ina viwango vyote lakini unapoileta Tanzania lazima uandae pesa ya kumpa mtu wa TFDA pamoja na TBS, sasa hiyo ni biashara kweli?

unaenda Bank kukopa na vigezo unavyo, lakini lazima ufanye deal na watu wa banki, sasa hapo kuna biashara kweli kama sio kijitoa fahamu na kijivika roho ya kutu
 
katika siku zoote leo umeongea.........
 

MUHESHIMIWA KITUKO NIMEKUSOMA NA NIMEKUELEWA.... UNACHOZUNGUMZA NI KITU AMBACHO KILITAKA KINIRUDISHE NJE TENA BAADA YA KUAMUA KUJA KUFANYA BIASHARA TZ.. Ila hii mimi sitaki kuitumia kama excuse.. kuna watu wanafanikiwa katika mazingira hayo... INGIA... SOMA RAMANI/MCHEZO.. THEN CHEZA KAMA WAO.. ukishi roma ishi kama waroma...
 

mkuu na gharama za kuuhifadhi mzigo(mbuzi) kabla hawajanunuliwa je??
una mabanda?lol
au una wateja tayari ni kiasi cha kudeliver?kusambaza wakishafika dar
 


Kaka kwa biashara mara nyingi lazima ufanye risk, lakini kwa biashara ya Tanzania risks zinadouble, serikali makini inapokuja madarakani, biashara zile zote za magumashi zinakufa, mfano halisi ni lile anguko lililowakumba wafanyabiashara hizo za kuungaunga wakati Mkapa anampokea Mwinyi, Huyo dada aliyezaliwa kinondoni sijuhi kama anamkumbuka Juma ngida ama Abdul msomali pale maeneo ya kwa Manyanya/ now Casablanca

Mkuu wala sikukatishi tamaa ila unapokuja kufanya biashara Tanzania lazima uwe mtu wa risk mara mbili, huwezi amini serikali ya Tanzania haina kumbukumbu rasmi ya matajili wote na kipato wanachomiliki, kwa maana nyingine serikali haijuhi mzunguko wake wa pesa, sasa anapokuja raisi kama alivyokuwa Mkapa kwenye kucontrol mzunguko ndio balaa linapoonekana
 
mkuu na gharama za kuuhifadhi mzigo(mbuzi) kabla hawajanunuliwa je??
una mabanda?lol
au una wateja tayari ni kiasi cha kudeliver?kusambaza wakishafika dar

Dada hizo ndio biashara zetu Tanzania, hakuna insurance, hakuna registration hakuna nini ni full risk mwanzo mwisho,
hao mbuzi kuna dalali wanakukusanyia, then wewe unakuwa ni mwendo wa kuonga kuanzia ulipowatoa mbuzi mpaka wanafika sokoni, mara mtu wa Vet/bwana mifugo, mara trafiki, mara nini sijuhi, na bahati mbaya gari ikianguka ndio 10m imekwenda na ndogo ya kufikia 300m inayeyuka, yaani ni full risk
 
mkuu na gharama za kuuhifadhi mzigo(mbuzi) kabla hawajanunuliwa je??
una mabanda?lol
au una wateja tayari ni kiasi cha kudeliver?kusambaza wakishafika dar

Dada hizo ndio biashara zetu Tanzania, hakuna insurance, hakuna registration hakuna nini ni full risk mwanzo mwisho,
hao mbuzi kuna dalali wanakukusanyia, then wewe unakuwa ni mwendo wa kuonga kuanzia ulipowatoa mbuzi mpaka wanafika sokoni, mara mtu wa Vet/bwana mifugo, mara trafiki, mara nini sijuhi, na bahati mbaya gari ikianguka ndio 10m imekwenda na ndoto ya kufikia 300m inayeyuka, yaani ni full risk
 
Unakoelekea lazima siku moja uwe mkwepa kodi wewe
 

LAZIMA WEWE Lara 1 siku moja utakuwa mwizi wa kodi ya serikali,,, tupinge???? Na mwizi hataenda mbinguni
 
hiki tunakiita kiburi, hufai kuwa kiongozi wewe, atakayekuoa ana taaaabu!!!!
 
nitajie tajiri mwanamke kati ya wale mia wa tanzania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…